Sunday, July 1, 2012

VAZI LA UCHA MUNGU (PART 1)

Asalaam Aleiykum. Leo tunaingia katika mada ambayo pengine yaweza kuwa ufahamu wako haujawahi kukutana na maelezo kama haya ikawa hichi kinacho andikwa kipya kwako, Basi nakuomba ufanye hisani ya kuyazingatia na kuyasoma kwa utulivu mkubwa ili upate kufahamu kwa uzuri haya yaloandikwa. Binaadamu tumebahatika sana kupewa (Rehma)na Mollah wetu katika mambo haya mawili yaliyohusiana na maumbile yetu, La kwanza (Nature)au Umbile letu halina tafauti na Mnyama, Halafu la pili tukapewa nafasi sisi ni viumbe pekee tulopewa uwezo wa kupanda daraja kutoka katika hali ya Wanyama na kwenda zaidi hata kufikia upeo wa juu kabisa ambao ndio huo (Ukhalifa)au Ucha Mungu katika ardhi hii. Katika maudhui hii tutaziangalia njia zote mbili ili tuweze kujua vipi unaweza kutoka njia moja ukajiunga na njia nyengine itakayo kukupeleka katika huo Ucha Mungu,(Mimi hapa nataja hiyo source)wewe una hiyari yako vipi unataka kuifanyia kazi ikiwa za kheri au shari uamuzi ni wako mwenyewe. Sasa haiwezekani kabisa kuzungumzwa mada hii bila kwanza kugusia kisa cha Nabii Adam a.s na Bibi hawa kilichotokea hapo mwanzoni ili upate kufahamu vyema maana hususia ya (Vazi la Ucha Mungu)huwezi kuhadithia kisa ukaanza mwisho na ukaacha mwanzo wake, Sasa huo mwanzo ulikuwaje? jikumbushe na aya za Quraan sura ya Baqarah-aya-35: وَقُلۡنَا يَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ وَكُلَا مِنۡهَا رَغَدًا حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَـٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ (٣٥) "Na tulimwambia "ewe Adam kaa wewe na mkeo katika bustani(peponi),kuleni humo mmeridhiwa popote mpendavyo,lakini msiukaribie mtii huu,msije mkawa katika waliodhulumu(kuto kutii amri ya Mwenye-enzi-Mungu)". Katika aya hii ndio tunasoma yale maneno unayosikia kila siku yakitajwa ndoa zinafungwa au zinaandikwa mbinguni, Mollah wako mwanzo kabisa anawaambia "Ewe Adam kaa na mkeo"sio hawara,au mchuchu,au girlfriend,au kimada kaa wewe na mkeo,ukifanya vyengine basi wewe umo katika makosa,huna hiyo (Taqwa)hata chembe na wala hutoipata mpaka mauti yatapokukuta, Na sababu kubwa umepiga mbizi katika dhuluma,unaishi kinyume na mwenendo alokupangia Mollah wako.Naam kaeni wewe na mkeo,lakini sharti ni moja msije kula katika mti huu,(kwani mkitenda hivyo mtajitia katika giza,kwani neno dhulumu limetokana na asili ya neno kiza, Na neno kiza mwenzie katika tafauti ni Nuru)Na hii nuru ndio kawaida yetu tunaishi ndani ya hii nuru na hii nuru ndio hiyo(Taqwa)kama tutavosoma huko mbeleni.Wawili hawa wakakaa salama kila kitu chao wanakipata wapendavyo,Shetani akawaingia kuwashawishi na kuwafanya wale katika ule mti kama inavyoendelea katika aya ya (36-sura-ya Baqarah)mpaka mwisho wake, Sasa nini kilitokea?. Wlipokula tu lile tunda hapo wakawa wenye kwenda kinyume na amri ya Mollah wao wakatumbukia (Gizani)Nini kiza?wanasayansi wanasema (Darkness is Absencess of light)ikawaondokea ile (privilage)haki ya Utiifu na kupata wanachokitaka katika maraha ya peponi ikatoeka ile(Blissfull life)hapo taa ya (Ucha)Mungu ikawzimikia na hapa ndio inaingia ile aya ya (27-sura-ya-Al-Aaraf)يَـٰبَنِىٓ ءَادَمَ لَا يَفۡتِنَنَّڪُمُ ٱلشَّيۡطَـٰنُ كَمَآ أَخۡرَجَ أَبَوَيۡكُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ يَنزِعُ عَنۡہُمَا لِبَاسَہُمَا لِيُرِيَهُمَا سَوۡءَٲتِہِمَآ‌ۗ إِنَّهُ ۥ يَرَٮٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُ ۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَہُمۡ‌ۗ إِنَّا جَعَلۡنَا ٱلشَّيَـٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ (٢٧) "Enyi wanaadamu asikufitinini Shetani,Kama alivyo watoa wazee wenu peponi,(alifanya nini shetani)Akawavua nguo zao(Taqwa-Utiifu-Nuru)ili awaoneshe tupu zao, Hakika yeye pamoja na kabila lake wanakuoneni, na hali yakuwa (nyinyi)hamuwaoni,Sisi tumwajaalia mashetani kuwa marafiki wa wale wasoamini". Naam hiyo nguo hususan ndio inalenga maudhui yetu, tunataka kujua nguo hii ni ya aina gani na kwanini walipokwisha kula hilo (Tunda) mara wakaziona tupu zao, na vipi imehusiana na chakula hayo yote tutayafahamu huko mbele ikiwa utasoma kwa njia ya utulivu na kutanguliza fahamu mbele, Na kwanini isiwe chakula wakati Mollah wetu Amesema katika sura ya (Abasa-aya-ya-24) فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَـٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦۤ "Basi Na atizame mwanaadamu chakula chake". Katika karne yetu hii tunajua kwa ukamilifu vipi chakula kinavyofanya kazi zake katika mwili wetu, tunaelewa kuwa (Akili-au-Brain)inachukua 85%ya vitamin zote zinazoingia mwilini, Sasa ilikuaje baada ya kula tu hilo tunda wakapoteza zile haki zote na neema zote walokua nazo,nini kilitokezea mpaka ikawa mpaka hii leo vigumu kwetu kuipata hiyo pepo, inakuaje safari hii inakua nzito sana, upo katika uchambuzi wa Vazi la Ucha Mungu endelea sehemu ya pili upate faida zake ili ukifunga saumu yako safari hii iwe ya aina nyengine kabisa.

No comments:

Post a Comment