Sunday, July 1, 2012

VAZI LA UCHA MUNGU(PART 2)

Asalaam-Aleiykum. Inaendelea kutokea sehemu ya kwanza: "Walipokwisha kula tu hilo tunda hapo wakapata fahamu, ikawa sasa ni wenye kujua wamechukua madaraka mikononi mwao(wamezima ile taa)wao wenyewe wamejitumbukiza katika giza, na ukiingia katika kiza sasa ndio unaanza safari ya kuitafuta taa tena, na ukianza kutafuta inabidi utumie akili yako kurejea kwenye muangaza na kwa kuwa unajua kutafuta njia ya kurudi basi hapo unakua unafahamu kila kitu, Ndio maana mpaka leo ikawa mtoto akifikia (Umri)wa Baleghe anaanza kuwa na dhamana ya maisha yake, Hapo tena Bwana Adam a.s na Bibi Hawa wakapata fahamu wakaziona tupu zao wakajua tafauti waliyonayo na vilowazunguka wakajisitiri kwa majani,Na ukisha kujua au kufahamu unapoteza ile (Innocent)yako hapo ndipo aya iliposema:(An-Nisaa-17), إِنَّمَا ٱلتَّوۡبَةُ عَلَى ٱللَّهِ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسُّوٓءَ بِجَهَـٰلَةٍ۬ ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٍ۬ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ يَتُوبُ ٱللَّهُ عَلَيۡہِمۡ‌ۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَڪِيمً۬, Hakika ya toba inayokubaliwa na Mollah ni yale wale wanofanya maasi kwa ujinga(kutokufahamu)ikisha wakatubia kwa haraka, Hao ndio Mollah huipokea toba yao, Mollah(wako)ni mjuzi na mwenye hekima. Lakini hakuna toba inayopokelewa baada ya kujua kwako kama aya ya 18 inavoendelea mpaka ukasubiri tena ushakua mzee unataka kufa halafu useme umetubu, hakuna kabisa maadam umefanya jeuri subiri chamte-makuni kikufike,na hivi ndio maana mpaka hii leo inakua taabu kwetu sisi kuipata pepo,sote tunahangaika kurejea peponi hakuna asotaka lakini na maasi hatutaki kuyaacha na kwa kuwa tunae mpinga amri zake ndie alotuumba basi tutateseka mpaka mwisho wa umri wetu tulopangiwa kuishi kwenye Ulimwengu huu. Kutokana na madhila na tafrani na uzito tunaojipa sisi wenyewe wa kuipata hiyo pepo ndio maana wanaadamu wengi wetu tunachagua basi bora turejee katika hiyo jinsia ya (Unyama,)bora niwe mnyama ili nijifiche kwa kujitoa fahamu, sasa nifanye nini?Wengine wanaamua kutumia pombe,wengine wanatumia (Drugs)madawa ya kulevya,wengine wanatumia (sex)ili anadhani mtu atajishughulisha na kusahau apate usingizi apate (relief)ya matafrani lakini yote hayo kwa kuwa ni kinyume na mwenendo ano utaka Mollah wako yanakua (Temprory)dharura kwa muda mfupi tu, pombe ikisha au madawa ya kulevya ya kisha au hamu ya (ngono) ikisha unarejea pale pale katika hali ya njia ya kuelekea (Ukhalifa)au (Taqwa)Ucha Mungu. Mwanaadamu ni lazima uchague njia ya Ucha Mungu ndio njia pekee itakayo kufanya upate salama na amani na hayo unayo yataraji hapa duniani huko peponi, Na Mollah wetu hajatufukuza moja kwa moja ila katuwekea njia ya kurejea kwake hakutufungia mlango, akatwambia mkifanya (Taqwa)Ucha Mungu utiifu,basi mtaipata ile hali walokua nayo wazee wetu Nabii Adam a.s Na Bibi Hawa huko peponi. Sasa Mollah wetu katushushia Vazi la ucha Mungu na nini hasa kitacho kujulisha hilo vazi la ucha Mungu,sasa nakutaka urudi nyuma ukaitizame ile aya uzuri zaidi ilosema huko mwanzoni"wasiukaribie ule mti wakala hilo tunda, walipokwisha kula hilo tunda wakajitupa kwenye (Dhuluma)kiza, sasa ikabidi tuletewe mavazi ya Aina mbili kama inavosema (sura-ya-Aaraf-aya-ya-26)"ـٰبَنِىٓ ءَادَمَ قَدۡ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمۡ لِبَاسً۬ا يُوَٲرِى سَوۡءَٲتِكُمۡ وَرِيشً۬ا‌ۖ وَلِبَاسُ ٱلتَّقۡوَىٰ ذَٲلِكَ خَيۡرٌ۬‌ۚ ذَٲلِكَ مِنۡ ءَايَـٰتِ ٱللَّهِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ (٢٦). "Enyi Wanaadamu tumekuteremshieni vazi ili mpate kusitiri (Uchi)tupu zenu na vazi la Ucha Mungu(Utawa) na hilo ndio bora zaidi,Hayo ni katika dalili(Neema)za Mollah wenu ili wapate kukumbuka". Hebu tuitupie macho nguo imetokana na nini, nguo imetokana na (Chakula)iwe ngozi au miti vyote hivyo vimetokana na ardhi,(Abasa-30) وَحَدَآٮِٕقَ غُلۡبً۬ا "Na miti ilosongana",ndio inayofanya nguo hizi tunazo zivaa hivi sasa,hili ndio vazi la kuhifadhi miili yetu, Halafu kuna nguo nyengine hii Wanaadamu tunaivaa ndani ya Mwili wetu na hii ndio inayotupelekea kuupata huo Ucha Mungu na vazi hili limewekewa fundi wake lazima upitie kwa fundi ndio akuvishe guo hili, endelea sehemu ya tatu ya Maudhui hii ili ukakutane na huyo fundi hususan mwezi mtukufu uko njiani unakaribia usije ukakosa nguo yako, pata japo kidogo na wewe kufahamu.

No comments:

Post a Comment