Sunday, May 26, 2013

ALAMA ZA MWENYE KUIPATA SALA PART 2

Asalaam Aleiykum,

Unaweza kuwa Muumin kwa njia mbili. ya kwanza una chupa moja kwa moja kwenye Imani, hutaki maelekezo, huna haja ya vigezo, na hiyo sana huwa zawadi kutoka kwa Mollah wako, na hii ya pili ambayo sote tupo hivi sasa ni ile ya jitihada ili tupate Kufuzu, na hii inaanzia wapi? hii inaanzia kwenye Akili(Mind) kwa hivi sasa Imani yako bado inaelea kichwani, haijaanguka Moyoni ndio maana utaona ukenda kwenye Sala hakuna unyenyekevu wowote unaoupata, vipi utaupa unyenyekevu wakati unakwenda kusali viatu umeweka (kwapani)nimetokea (Tanzania) hivi karibuni mambo niloyakuta huko imeniingia huruma sana kuziona vipi Sala za huko Nyumbani zinasaliwa, kuanzia kwenye Udhu unaanza kuvifikiria viatu, vipi leo utakua na (Unyenyekevu) katika Sala, vipi utakua na (Unyenyekevu)wakati Imam anasalisha kasujudu anasubiri watu wamalize kutia Udhu wapate kuwahi Sala, vipi utakua na unyenyekevu wakati unaingia katika Sala mawazo yote yapo kwenye (Sex), vipi  utapata unyenyekevu wakati unajiunga katika hiyo Sala umejaa hasira na hamaki na chuki vimetawala Sala nzima, madeni na mikopo yote inakuja hapo, hotuba za Siasa unaandika hapo, hesabu zote unafunga hapo, majibu ya mtihani unayapata kwenye Sala hiyo hiyo, vipi leo useme umepata unyenyekevu.
Hiyo unayofanya sasa hivi ni jitihada na ndio vizuri kufanya jitihada wakati huu umri unapotea, zidisha juhudi sana, Sasa nini ufanye ili kuipata hiyo Imani? anza kuitumia hiyo (Mind) Akili, fanya uchunguzi Mollah kakupa mifano, kama kwenye aya hii ya sura ya Dhaariyat aya ya 20 "وَفِى ٱلۡأَرۡضِ ءَايَـٰتٌ۬ لِّلۡمُوقِنِينَ"
"Na Katika ardhi zimo(dalili chungu nzima)kwa wenye yakini"
fanya uchunguzi upate hiyo yakini, ukiipata hiyo yakini ndio ushapata Imani, na ukipata Imani utaanza kujiuliza mie nani, kwanini niko hapa, vipi inakua mimi na kinyama sote tunalala usiku, kinyama kikiumwa nani anakitibu, na kwanini kinapona, na nani anawaponesha,mbona vinyama vina akili kama zetu, vinatafuta chakula na vikishiba havina hata haja ya kuweka akiba, ina maana vinyama vina Imani kuliko mimi, vina muamini Mollah kushinda mimi, na mengine kama Mollah wetu alivotuwekea Rada mbinguni za hizo nyota tukawa tunajua huku mashariki na huku magharibi, na utapata mengi ukianza kutafakari mpaka utafika ukingoni hapo Akili itasimama, na Akili ikisimama hapo ndipo pahala unapoweza kuchupa ukawa Muumin, na ukiogopa ukarejea nyuma unakua unabakia kuwa Muislam, na Sala yako inaendelea kuwa kama ilivyo hivi sasa.
Sasa ukichupa ukawa Muumin nini kinatokea?
Yanatokea mabadiliko makubwa, sababu unakuwa unaishi moyoni(Through heart) na sio akilini (Through Mind). Na unapoishi moyoni unaona mambo kwa njia nyengine kabisa, unakua katika hali mpya kabisa, na kama unataka kujua hali hiyo inakuaje basi muulize yule anopenda, yule alo (Fall in Love)au mtizame mwenye kupenda hata akipewa kikombe cha sumu na mpenzi wake, na wewe uwe shahidi umeona sumu imetiwa, na upige kelele hiyo sumu, hiyo sumu, basi utaona yule anopenda anakamata kikombe na kumimina chote mdomoni kwa ajili ya Imani aliyonayo, sasa ikiwa hilo ni penzi la kumpenda mwanaadamu mwenzio, nini habari yako wewe ukiyagundua mapenzi ya kumpenda Mollah wako, una hali gani sasa ushajitaarisha kusimama mbele ya yule umpendaye, vipi leo katika penzi hilo unatoa nafasi ya kuingia kitu chengine.
Sura ya Muumin aya ya 2 "ٱلَّذِينَ هُمۡ فِى صَلَاتِہِمۡ خَـٰشِعُونَ"
"Ambao katika Sala zao huwa wanyenyekevu"
Unaingia katika hiyo Sala kwa njia ya moyo, siyo njia ya Akili tena, kabla ya kuanza Sala lazima mambo yote yasimame, fikra zote mbaya zipotee, heshima ya Sala yako ibadilike, ukisoma aya ndani ya Quraan sio kwa kupita ni lazima uzame na huku unaifasiri taratibu huku machozi yanakutoka kwa  kuujua ukweli wa maneno hayo na kufahamu kwa  ukamilifu unachokisoma na kukiabudu. Na hapo ndipo kwa mara ya mwanzo utapata utulivu na unyenyekevu mkubwa wa hiyo Sala. Endelea part 3

No comments:

Post a Comment