Asalaam Aleiykum,
Limekuja swali linasema hivi, Nini hukumu ya wale ambao wanaimba, wanocheza kamari na kufanya mengine ya haramu halafu wakatajirika kutokana na vitu hivyo(Yaani)wakapata pesa halafu ikatokea wakagundua kama walikuwa wanakosea mbele ya Allah, ikisha wakarudi kwa Mollah wao kwa dhati, vipi hapa Sheria inasemaje, Juu ya Mali zao walizozichuma huko Nyuma kwa njia ya Haramu?.
Toba Tubi yoyote anataraji jawabu iwe nzuri yenye kumridhisha, iwe inampa tamaa yeye kuwa ulivofanya sio tatizo na unaweza kubakia na Mali hizo pasi kupata tatizo lolote, kwani wanadhani haramu ni lile tendo lakini hiyo Mali ishavuka daraja ya hilo tendo, Hivyo ndio Akili zetu zinavyotutuma nipate hapa ulimwenguni raha mustarehe na huko mbinguni Akhera kadhalika niwe pia mimi Bwana, Hiyo ndio Akili ya mfanya biashara anayedhulumu, hiyo ndio Akili ya kila anopata chumo la Haramu, anafanya (Bussiness) na Mollah wake mimi nitadhulumu, halafu tene nitakula haramu, ikisha nitabakia na Mali yangu ya Haramu, na Wewe Mollah wangu upande wako fanya kimoja tu nisamehe.
Nini Anasema Mollah wako kuhusu kadhia hii ya Toba?(Al-Imran.135)
"وَٱلَّذِينَ إِذَا فَعَلُواْ فَـٰحِشَةً أَوۡ ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَہُمۡ ذَكَرُواْ ٱللَّهَ فَٱسۡتَغۡفَرُواْ لِذُنُوبِهِمۡ وَمَن يَغۡفِرُ ٱلذُّنُوبَ إِلَّا ٱللَّهُ وَلَمۡ يُصِرُّواْ عَلَىٰ مَا فَعَلُواْ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ"
"Na(wale)ambao wanapofanya uchafu, au Kudhulumu nafsi zao,humkumbuka Mollah na kuomba msamaha kwa dhambi zao, Na nani anayeghufuria dhambi isipokua Mwenye enzi Mungu?Na hawaendelei na (Madhambi)waliyoyafanya, hali wanajua(Hayo ni Haramu)?"
Hapo juu swali limeanza wakagundua kama walikua wanakosea, na hapa chini aya inataja wazi, wala haikubana maneno,(Hawaendelei na Madhambi hayo)hiyo ndio kusudio la msamaha, Msamaha umekusanya mambo matatu, la kwanza (Kujuta)kwanini nikadhulumu, ilikuaje nikatenda haramu ile, sikufanya yale isipokua ama nilikua nimekusahau Mollah wangu au nilikua sijui, sasa mimi naomba Ridhaa yako unisamehe "Ewe" Muumba wa Roho yangu.
La pili Kuchukia, kwanini mimi ilinipelekea kuchukua mali ya watu kwa hadaa au kwa nguvu, kwanini nikachuma mali hii kwa njia ya Haramu na mpaka sasa naishi nayo, na kila nikiiona inanikumbusha Dhambi zako na yote niliyoyafanya, kutokana na hali hiyo mimi sasa sitaki hata kuziona mali hizi za Haramu, chukueni zote mimi hazinihusu hata chembe, sitaki kuwa Mmiliki wake abadan.
Na la Tatu kuwa hutotenda tena kosa hilo, sasa vipi utaendelea kubakia na Mali ya Haramu halafu useme umetubu, ndio maana nimekwita Toba tubi, maana yake unaitaka mali ya haramu na pepo ya halali, vipi viwili hivyo vitakaa pamoja, Madamu umechagua kubakia na mali ya haramu basi jijue umeshajiamulia wewe mwenyewe kwenda kuteseka kwenye Jela ya Mwenye enzi Mungu huko Akhera, na Kwa hilo halina mbadala kabisa, kwa yakini litatokea mapema pale utakapofunga macho tu, huku Ulimwenguni mali inaendelea kudumu, na huko Akhera wewe unaendelea kuchomeka, Shauri na uamuzi unao wewe, waachie wanao au ndugu zako mali ya haramu halafu wewe jichukulie dhamana ya moto.
Endelea Part 2
No comments:
Post a Comment