Saturday, May 11, 2013

TOBA TUBI NA MALI YA HARAMU PART 2

Asalaam Aleiykum,

Wengi katika wanaadamu wanadhani mambo yapo rahisi huko kesho Akhera, wanafikiri hukumu itatolewa kutokana na muono wake unavomtuma, na wengi tushajidhulumu kutokana na dhana hizo yakuwa bakia na mali ya haramu na Mollah wako keshakusamehe, hebu itupie macho aya ya Quraan inayokuonesha vipi ukimkufuru Mollah wako na kujidhulumu nafsi yako unakuaje, hukuanza wewe fikra hizo wameanza tokea walopita kabla yako, Quraan Al Kahf 35-36,

"وَدَخَلَ جَنَّتَهُ ۥ وَهُوَ ظَالِمٌ۬ لِّنَفۡسِهِۦ قَالَ مَآ أَظُنُّ أَن تَبِيدَ هَـٰذِهِۦۤ أَبَدً۬ا"
"Na akaingia katika Bustani yake na hali yakuwa anajidhulumu nafsi yake, akasema (Mimi)sidhani abadan kuwa (Bustani-Mali)hili litaharibika"
Na hivi pia unavodhani wewe, aah si nishasamehewa, vipi tena niadhibiwe kwa sababu nakaa kwenye Nyumba ya haramu, natumia  vilivyo vya Haramu, muda wake ushapita mie sifanyi haramu tena, sasa itakuwaje nipewe adhabu.

"وَمَآ أَظُنُّ ٱلسَّاعَةَ قَآٮِٕمَةً۬ وَلَٮِٕن رُّدِدتُّ إِلَىٰ رَبِّى لَأَجِدَنَّ خَيۡرً۬ا مِّنۡهَا مُنقَلَبً۬ا "
"Wala sidhani kuwa kiyama kitatokea, na kama (kitatokea hicho Kiyama)nikarudishwa kwa Mollah wangu, bila shaka nitakuta kikao chema kuliko hiki(Nilichopata Ulimwenguni)(huku nipate na kule nipate)"
Hivi ndio sote tunavodhani, kula rushwa, chuma haramu, nyanganya hapa, kaibe kule, kwani hicho kiyama kipo, mbona mpaka leo hakijatokea, na hata kikitokea wewe ushasamehewa na huko utakuta (Jumba la Ghorofa na Swimming Pool)pembeni. Hasara kubwa na jambo zito sana unalofikiria, Shetani anakupigia muzeka wa usahaulivu, nyimbo inazidi kukupepea ulale uzuri, nasikia unakoroma mpaka huku nilipo, hebu acha kunifanyia zogo kwa usingizi usofaida, jaribu kujikumbusha nini Toba?
Wakiristo wanaita (Born Again)hawajakosea ni kama Mimba, hakuna anoendelea kubakia na Mimba lazima izaliwe, na uchungu wa kuzaa anaujua mwanamke, na wewe lazima upitie uchungu huo, lazima kama mali hiyo kachuma mzee wako au wewe mwenyewe basi lazima upate uchungu wakuitoa kama ulivopata Raha ya kuichuma, Usimame useme Mali hii si haki yangu na mimi naitoa yote kwa ajili ya Mollah wangu yeye ndio atakua Hakimu wa jambo hilo, majumba chukueni, magari chukueni, mapesa (bank yote yenu)mimi nataka niwe msafi kama siku nilozaliwa, au kama nguo nyeupe isiyokua na doa.
Hiyo ndio Toba wala sio Tubi, itamke sawa sawa upate kutubu kikweli, upate kutubu moja kwa moja haifai kubakia na chochote kile cha Haramu, Toba maana yake kujitua mizigo, sasa vipi leo umebakia umeibeba, halafu unasema nimetubu, Nini Toba?
Toba lazima upate uchungu, unaachia huku mate yanakutoka, kama unakula shubiri, upande chungu upande dawa, Toba lazima umungunyuke kama udongo ubakie mchanga, Toba lazima upotee ndani ya Nafsi yako, ikisha uzaliwe mwengine ndani kwa ndani, alotubia, hana tamaa, alotubia hafanyi tena, alotubia hadumu na kumbukumbu, anafuta vyote kama ulozaliwa Zanzibar, Ukaishi China, jee utaikumbuka Zanzibar, hiyo ndio maana ya Toba potea kabisa kazaliwe Dubai Rasulhema, hiyo ndio Toba ya Kweli na kama unazuia Mali yako ya haramu, wewe utakua Shahidi kwa hilo Mbele ya Mollah wako. Namuomba Mollah atukinge na yote ya Haramu.

No comments:

Post a Comment