Sunday, May 26, 2013

ALAMA ZA MWENYE KUIPATA SALA PART 1

Asalaam Aleiykum,

Umeshawahi kumuona Mtu kalala kwenye ngoma chini ya spika? watu wanaimba kwa mayoe, bibi harusi ndio anaingia na huku ukitizama pembeni Mtu kalala sio usingizi tu, bali anakoroma na anaweza kuota ndoto kabisa akiamka akakuhadithia, au unaingia senema unalipa pesa halafu unalala mwanzo mpaka mwisho, basi ukiyajua hayo kama yanatokea na hili jengine pia linatokea, unasimama kusimamisha Sala na  huku unaota ndoto za ajabu ajabu, umo kwenye usingizi mzito na kama utaamshwa ghafla unaweza kumpiga mtu kibao kwanini kakushitua, sisemi haya ikawa nazua, au nimeyapanga, bali itizame Sala yako ikoje, halafu ufanye hima kuzingatia haya nitakayo kufahamisha kwenye Darsa yetu ya leo ili ukurupuke utoke usingizini. Wengi katika sisi tunaitundika Sala kwa Maringo tukiwa na viburi yakwamba nisha Sali, na ishaandikwa, Nasisi tumekubali umesha sali lakini jee imekubaliwa? na Jee Mwenye enzi Mungu kataja mifano yoyote ya kukubaliwa hiyo Sala,? pata habari hii ili ujijue unasimamisha Sala au unasimama mwenyewe tu na ndoto zako.
Nini Sala?
Sala ni Maombi maalum ambayo madhumuni yake unaomba ukubaliwe kukaribishwa, kupokelewa, kuruhusiwa kuingia na kuwa karibu katika Utukufu wa Ufalme wa Mwenye enzi Mungu na ukisha kuruhusiwa katika (Matuka-Saabur)hapo tena Sala inapatikana kwa ukamilifu,( na Sala  ikipatikana kwa Ukamilifu hakuna siri tena utakua unajua ama mimi Mollah wangu anazipokea Ibadah zangu)ndio maana ikawekwa wazi kama tutavosoma huko mbele, Naam yaweza kuwa unatuma maombi haya (Sala zako mara tatu au mara tano au mara elfu kwa siku)Lakini tamaa yako unataka ukubaliwe maombi haya ili upate marejeo mazuri kwa Mtukufu Mollah wako yule aloumba Mbingu na Ardhi na yule alokukirim wewe huu Uhai wa kuweza kumkumbuka.
Nikitaja Sala au (Maombi) sina maana ya ile Sala yako ya kuomba cheo au kuomba ubunge, sikusudii yale maombi yakuomba Mke au Mume na mengineyo, laa Sala nilokusudia hapa ni ile unayokwenda kwa Mollah wako na Moyo mweupe ulojisalimisha, Hutaki Mali au kutaka Pepo, huna choyo au kuwa na wivu, hujenda na hasira wala chuki yoyote, Umekwenda Msafi hujabeba mambo ya kipuuzi, umekwenda kwa Mollah wako huna munkar wala Fawahisha kwenye kichwa chako, unasimama na kutamka Maneno ya yakini Allahu Akbar: Nani mwenye kutamka maneno hayo yatupasa tuulize Quraan sura ya Muumin aya ya (1)"
"قَدۡ أَفۡلَحَ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ"
"Wamefuzu Waloamini"
Kwanini Wakafuzu? Sababu mwanzo walikua kama mimi na wewe, wamepita katika daraja ya kwanza ya kusikia, halafu wakapita katika safu ya pili ya kukubali, ikisha wakaingia katika hii sehemu ya tatu  yakuwa waumini, Unapewa habari kama hizi pengine mwanzo zilikua hazijakufikia, Na sasa zimekufikia ili upate kubadilisha mwenendo wa kuingia katika Sala yako, upate Imani ya kweli na upate kuipata Sala na wewe uingie katika kundi lilotajwa kwenye hiyo aya "Wamefuzu Waloamini".
Usije ukajidanganya hivi sasa kudhani umefuzu, yakupasa ujiangalie upo katika kundi gani hivi sasa ili uzidishe juhudi.Nini Kufuzu? kufuzu kuna mambo mawili lazima yatokee ndio ujue umefuzu, la kwanza ima uwe umeshindwa ukajaribu tena, na la pili ukajitahidi na kuzidisha juhudi  mpaka ukapata sifa ya kufuzu(Kufanikiwa)."Wamefuzu Waloamini" na ukifika (Stage)hii moja kwa moja unakua Muumin, na Muumin maana yake kila jambo lako linakua kwenye mstari, Muumin wa kweli hana nafasi ya makosa kwenye moyo wake.
Sasa Vipi unakua Muumin? Endelea part 2

No comments:

Post a Comment