Sunday, May 5, 2013

BARUA YA UKUMBUSHO PART 3

Asalaam Aleiykum,


" قَالَتۡ يَـٰٓأَيُّہَا ٱلۡمَلَؤُاْ إِنِّىٓ أُلۡقِىَ إِلَىَّ كِتَـٰبٌ۬ كَرِيمٌ "
"Akasema (Yule Malkia kuwaambia washauri wake)hakika nimeletewa Barua Tukufu"
Namkumbushe yoyote kuhusu barua yako Tukufu, kwani ukimkumbusha umemwita kwenye utiifu, na ukimwita kwenye utiifu maana yake umemleta kwenye Taqwa, na ukimleta kwenye Taqwa inakua Roho mbili zimependana kwa ajili ya Mwenye enzi Mungu.

"إِنَّهُ ۥ مِن سُلَيۡمَـٰنَ وَإِنَّهُ ۥ بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ "
"Imetoka kwa Suleiman a.s, nayo ni kwa jina la Mwenye enzi Mungu mwingi wa Rehma Mwenye Kurehemu"
Na hii imetoka kwangu, na Barua yoyote ikianza kwa Jina la Mollah wako inakua Tukufu, na ndani ya Utukufu huo ndio unazikuta hizo Wingi wa Rehma na Wingi wa Kurehemu, akiikamata Barua hii Tukufu yoyote yule ikiwa mja mwenye Fahamu basi pale pale Rehema zinaanza kumshukia na anakua Mwenye Kurehemewa, na kama akipuuza basi ujue huyo kesha, huyo kamalizika subiri muda mdogo utaona yepi yatakayo mfika, lakini na wewe usiwache kumuombea dua.

" أَلَّا تَعۡلُواْ عَلَىَّ وَأۡتُونِى مُسۡلِمِينَ"
"Wala msinifanyie Jeuri, na fikeni(Njooni)kwangu na hali ya kuwa mumekwisha kusilimu"
Wala usiifanyie mzaha Barua yangu hii, Ikiwa Mtume Suleiman a.s kamuandikia mtu aliyekua anasujudia Jua kumwita arejee kwa Mollah wake, vipi mimi leo nitakua mkosa kukwita wewe kwenye njia ya kheri, wewe ni Muislam huna haja ya kunijia, ila unachotakiwa uzinduke kutoka usingizini, ibadilishe nafsi yako, kamata Barua hii enyi vipenzi vyangu, isomeni kwa shauku, inatosha hayo mlotenda, sasa Rejeeni kwa Mollah wenu mtamkuta mwenye kusubiri na Mwenye kusamehe, Nakala ifike kwako enyi wanangu, kwako wewe mshirika wangu, pamoja na nyote mlo karibu na mimi kwa mahusiano ya Udugu, napenda pia kuwafikishia  wote ndugu zangu katika Uislam.


No comments:

Post a Comment