Sunday, May 5, 2013

BARUA YA UKUMBUSHO PART 2

Asalaam Aleiykum,

Sababu kubwa imetuhusu mimi na wewe, na mimi nadhani mahusiano yetu si ya nyama na mifupa bali yamekwenda mbali(Deep)Kiroho, na nimetambua mimi mahusiano yetu haya ni ya (Thamani)kubwa na yatakayo endelea kuishi milele,  Na kutokana na uhusiano huu ndio imekua sababu ya mimi na wewe kukutana hapa Ulimwenguni, na kutokana na sababu hiyo mimi sina shaka makutano yetu yatatokezea tena huko Akhera tuendako, napenda uelewe yametukutanisha Mapenzi yake Mollah wetu, wewe ulikua haupo katika Ulimwengu huu wala mimi sijaumbwa. sote sisi  tukapita katika Mlango wa Rehma wa Mwenye enzi Mungu ikisha tukazaliwa katika nchi moja ama tafauti, hapo tena tukaja kuungana na kuunganisha Udugu ulio imara kabisa, ikawa huyu mtoto, wewe dada, yule kaka, hawa wajomba, shangazi nk, sasa kilicho nipelekea kuandika Barua hii ni muono wangu mimi juu ya matendo yako, naona si ya kumridhisha Mwenye enzi Mungu.
Na mimi nina khofu kubwa ya wewe kwenda kuwekwa kwenye Jela(Shimo)la Jahannam, Na ninayo yakini kwa kuwepo kwa Moto huo kwa sababu Mitume yoote wametaja kuwepo kwake Jela hii, na mimi sina shaka kwamba woote wawe wenye kusema jambo ambalo halipo. Na Mollah katuhimiza katika sura ya At-Tahrim aya ya 6 "يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ وَأَهۡلِيكُمۡ نَارً۬ا وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُ عَلَيۡہَا مَلَـٰٓٮِٕكَةٌ غِلَاظٌ۬ شِدَادٌ۬ لَّا يَعۡصُونَ ٱللَّهَ مَآ أَمَرَهُمۡ وَيَفۡعَلُونَ مَا يُؤۡمَرُونَ"
"Enyi Mloamini jiokoeni Nafsi zenu na watu wenu(Wakaribu)na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe, Wanousimamia(Walinzi wake)Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Mollah (Wao)kwa amri zake, na wanatenda wanayo amrishwa".
Nimehimizwa nikupe ujumbe huu na yule anokujaalia kulala ikisha akakuamsha kwa Uwezo wake, anokujaalia kuhema bila ya kufanya juhudi yoyote upande wako, na akizuia pumzi kidogo tu unapaparika, huyo ndio alonipa mimi nguvu za kuandika Barua hii kukumbusha ujitahidi sana kama unampenda Mollah wako na mie mwenzio, basi sasa nakwambia acha kulewa, acha kuvuta bangi, acha mambo ya mirungi, jiepushe na kudhulumu, jizuie na kuzini, na ikisha nakutaka ujiepushe na mambo yote ya haramu, halafu najitolea mimi mwenyewe muhanga acha kuninunulia dhahabu au majumba na hizo pesa au mali ulonayo tulee mayatima, tuwatizame wajane,tuwalishe maskini, tukifanya hivyo jambo la kwanza hapahapa Ulimwenguni Mollah wetu atatueremshia mapenzi, atatupa baraka, tutapewa tahfif za maradhi, atatufanya wafalme kwa walotuzunguka, kwa hayo yote sijioni kuwa mimi mkosa katika kukuandikia barua hii Adhimu ambayo nataraji itakufika katika hali ya kuufahamu ujumbe huu wa kheri.
Nakwita mwenzangu urudi kwa Mollah wetu, mimi nishatangulia kamata mkono wangu tuwe pamoja, usiniache nikazama kwenye Nuru wewe ukabakia kichochoroni kwenye kiza totoro nini itakua hali yako,  Na kumbuka hakuna yoyote anorejea kwa Mollah wake ila hufunguliwa Neema zote na Rehma za Mwenye enzi Mungu, na kwa ushahidi wa hilo tujikumbushe barua ya Nabii Suleiman a.s alyomuandikia (Malkia Bilkis)kumwita kwenye Uislam. alifanya nini? sura ya Naml aya ya 28 mpaka 31.

"ٱذۡهَب بِّكِتَـٰبِى هَـٰذَا فَأَلۡقِهۡ إِلَيۡہِمۡ ثُمَّ تَوَلَّ عَنۡہُمۡ فَٱنظُرۡ مَاذَا يَرۡجِعُونَ"
Nenda na Barua yangu hii na (Wadondoshee)uwafikishie, kisha uwaache, na utazame watarudisha(Maneno) gani"
Na wewe kama unaogopa kumpa mkononi barua yako Ipost au weka kwenye mto usiku halafu kimbia ukalale ukumbini.

Endelea Part 3

No comments:

Post a Comment