Sunday, May 26, 2013

ALAMA ZA MWENYE KUIPATA SALA PART 3

Asalaam Aleiykum,

Ukisha kupata unyenyekevu, ndio unaweza kuyapata maneno ya Hekima ya kumuomba Mollah wako, (Mfano) Mollah wangu nikubali kuwa kipenzi chako, nifungulie mie miujiza yako niwe shahidi kwa hilo, nipe zaidi ukuruba huu katika Sala ili nipate ladha ya kumilikiwa na wewe Mollah wangu, usinijaalie mimi kukusahau na kutoka katika hali hii nilonayo ya Sala, kumbe hivi ndivyo ilivyo Sala, basi nipe mimi kila saa na dakika niwe nimo katika Sala nasali kwa ajili yako. Na huko ndiko kumkumbuka Mollah wako, ukiwa umesimama, umekaa au hata ukiwa umelala, umo usingizini(Body)Mwili umelala wewe umacho una msabahi Mollah wako, na hiyo ndio daraja ya Muumin aliyefuzu, na hapo tena ikimalizika hiyo Sala ya wakati wewe unaendelea nayo ile yako ya kudumu, na ukiipata hiyo ya kudumu unakuwa vipi? vipi inakua ukishamaliza Kusali, aya ya 3 "وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَنِ ٱللَّغۡوِ مُعۡرِضُونَ"
"Na ambao hujiepusha na mambo ya Upuuzi"
Ukishamaliza kusali inabidi uendelee na maisha, na kuendelea na maisha inabidi ukutane na vishawishi vingi, kwa hiyo kama kweli wewe Muumin na unaipata Sala, basi unajiepusha na mambo ya upuuzi, Mollah wako hataki kipenzi chake kiwe kichepe chepe, hakuzuii usifurahi, ila anakukinga na mambo ya kijinga, sababu anajua mambo ya kipuuzi yameandaliwa na shetani ili kukusahaulisha, mazungumzo ya vibaraza, na hivi na vile, fulani kafanya hivi yule kafanya vile, yote hayo mambo ya kipuuzi hayakuhusu, na ni vitu vyenye kukupunguzia Imani, sio kwamba ukimbie watu, au uanze kupanda kiburi, umeambiwa ujiepushe, sio ujikinge, kujikinga maana yake unajilinda, hukutani nao, kujiepusha maana yake upo nao lakini wewe mizizi ya Imani imeshaota wao wanazungumza siasa wewe unamdhukuru Mwenye enzi Mungu, huko ndiko kufuzu, na huko ndiko kuipata Sala. Na mengine yalotajwa katika sura hiyo ambayo tutayazungumza siku za mbeleni za kufuzu kwa Muumin) lakini ukumbuke Muumin bado yumo kwenye Mtihani  mpaka upite katika daraja hiyo na ufike katika daraja nyengine za (Swalihina na Mukhlisina)hapo tena ushakua mtu mwengine kabisa, unaishi Duniani lakini ushawasili Akhera. Mollah wangu tujaalie tuwe katika kundi la wale wanokubaliwa Sala zao, tupe sisi faida ya Sala kuijua na kuishi nayo Daima kama walivofanya waja wako wema walotangulia, wewe Wajua Mollah wetu Dunia imetuzonga katika karne hizi tunazo ishi hivi sasa, basi tufanye wateule wa zama hizi watakaokuwa wambele katika enzi yako siku hiyo utakayo tuhitaji. Amin.

No comments:

Post a Comment