Sunday, July 13, 2014

BARAKA TANO ZA RAMADHAN PART 1

Asalaam Aleiykum

Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wenye kuja na zawadi nyingi sana ambazo hazina idadi maalum, Miongoni mwa zawadi hizo zimo hizi za Baraka tano ambazo wanapewa Umma huu wa Kiislam (Special) kwa sababu moja tu nayo ni ile kuitikia kwa pamoja wito wa Mwenye enzi Mungu na kukubali kufunga mwezi huu wa Ramadhan, Basi kwa ajili hiyo mnapewa na kuongezewa Baraka hizi Tano ambazo ukizipata Mja unakua umeshafanikiwa mafanikio makubwa katika uhai wako na mauti yako.
Napenda uelewe Baraka ziko chungu nzima, lakini hizi tano ni (Special)kwa ajili yenu Mlofunga. Nini Baraka?
Baraka ni ngumu kufasirika kilugha ya kawaida, lakini midamu tuko katika Darsa ya kuichambua Baraka basi itabidi nijitahidi kuileza ili tupate kuifahamu, lakini elewa hata sifiki karibu na kuifasiri Baraka, kwa sababu baraka haina tafsiri, naweza kuileza baraka kwa neno moja tu nikaita Baraka ni Furaha kwa anaeijua, Na ama kwa yule asiyeijua kwake yeye Baraka ni kitendo, vitu viwili tafauti huyu kwake ni furaha na yule kwake ni kitendo, ndio maana yule asiyejua husema (I'm counting my blessing).
Huyu yeye tayari akipata Mali anasema kabarikiwa, ndio sawa, wala sio kosa, lakini huyu anakua kabakia kwenye kitendo na anasahau maana yenyewe ya Baraka, na kuakiangalia kitendo ni sehemu ya chini kabisa na yenye mtihani mkubwa.
Lakini mwenye kujua yeye akipewa Furaha tu anajua kapewa Baraka kubwa kabisa, kwani unaweza kupewa hiyo Mali (Utajiri)ukanyimwa Baraka za Furaha, kwa hiyo ndio maana nikasema Baraka ni Furaha, bila ya furaha huo ni mtihani wa Baraka, sasa vipi ikawa Furaha jitizame wewe ukipewa Watoto unafurahi (Hiyo Baraka) Ukipewa Afya unafurahi, angalia unakuwaje yakikufika maradhi, mambo yote yanomalizikia kwenye furaha jua hiyo ni (Baraka). Sasa kama ushalijua hilo Mwenye enzi Mungu mwenye kutoa hizo Baraka kwa viumbe vyake kawashushia ndaniya mwezi huu Tano rasmi kwa wale wenye kufunga kweli, na pia napenda uelewe Baraka huwezi kuilazimisha, unachoweza kufanya usubiri ikushukie ndio tunajikuta katika mwezi huu wa Ramadhan Baraka zinamiminika.
Baraka ya Mwanzo(1) "Anasema Bwana Mtume s.a.w" Umma wangu umepewa Mambo matano hawajapata kupewa Umma zengine kabla ya hapo, Jambo la mwanzo ikiwa utatia nia kwa mapenzi ya kufunga Ramadhan kwa ajili ya Mollah wako, ukanuia  kuwa utaifanyia ihsan funga yako iwe ya haki na Iman ya kweli, "Basi Mwenye enzi Mungu ule usiku wa mwanzo wa Ramadhan anakuangalia na mwenye kuangaliwa na Mollah wake basi haitomfika adhabu, (Hayatomkuta mateso) .
Endelea part 2

No comments:

Post a Comment