Sunday, July 20, 2014

DUA YA TOBA PART 3

Asalaam Aleiykum

"Ewe Mollah wangu" Nabii Yunus a.s aliyakimbia majukumu yake ukamtia kwenye Tumbo la Chewa kwa siku tatu tu, akawa anaita na kuomba atolewe, akakubali makosa yake na ukamsamehe na kumtoa kwenye tumbo la Chewa, Nini habari yangu mie ambaye nakwenda kukaa kwenye tumbo la Ardhi mpaka siku ya Kiyama, Mollah wangu na mie kiumbe chako nimeyapuuza majukumu yangu mengi uliyonipa, nimeshindwa mimi hata kuitizama Familia yangu na kuwahimiza wakutii Wewe Mollah wangu, Marafiki wangu wanatenda maasi namie nimo kuwapigia makofi, Nashindwa hata kuhimiza kizazi changu kukuabudu Wewe Mollah wangu, itakuaje hali yangu mimi nitakapokamilisha Umuri wa kuishi hapa ulimwenguni, Mollah wangu mimi siziwezi adhabu zako, Nauomba msamaha wako, nisamehe kiumbe chako, niepushe mimi na Moto wa jahannam na adhabu zengine ulizowaandalia wafanyao maovu wasokuogopa Wewe Muumba wa kila kitu.
"Ewe Mollah wangu" Wewe ndiye uliyemnyanganya Nabii Suleiman a.s Ufalme kwa ajili ya kukusahau Wewe mara moja tu, ikisha akaomba Toba na Wewe ukamsamehe, Basi nina hali gani mie nisie kukumbuka kabisa, Yaa Raab mimi nimeshughulika kutafuta cheo na Utajiri kwa waganga na majini, nakushirikisha Wewe katika Shirk kubwa kabisa, Basi Sasa nakuomba Mollah wangu nisamehe usinijaalie tena kurejea makosa hayo makubwa, Nakuomba Mollah wangu niridhie niipate Toba itokayo kwako, nipe mimi Faraja ya kusamehewa na Wewe na uniepushe na Adhabu za siku ya kufa, adhabu za kaburi, adhabu za siku ya kufufuliwa, adhabu za siku ya hukumu, niepushe na adhabu za Ulimwengu huu na Adhabu za Akhera, Nijaalie afya unishushie mapenzi ya kukuabudu wewe kila saa na dakika, Mollah wangu wasamehe Wasilam wenzangu na viumbe wako kwa jumla walo hai na walotangulia mbele ya haki. AAMIN.

No comments:

Post a Comment