Sunday, July 13, 2014

BARAKA TANO ZA RAMADHAN PART 2

Asalaam Aleiykum,

wengine wakisikia kuangaliwa wanaanza kuleta ishara zao za maajabu, labda jicho kubwa linangara, au hivi na vile wanaleta mifano ya ajabu ajabu, Mollah wako hana haja hata ya kukuangalia yeye ni mwenye kujua na anaelewa kuwa Mja wake kaingia katika bahari ya kujulikana, Na ile dhamira au (Nia) uliyoiweka ndio inakufanya uchukuliwe dhamana ya kutokupewa adhabu yoyote, ni kwa ajili ya Nia tu na wala si jengine, Na hata ukifa usiku huo basi wewe ushasamehewa Dhanmbi zako, Na Mja ukijua umesamehewa Dhanmbi zako furaha iliyoje kwako wewe Kiumbe.
Baraka ya Pili (2)"Kila siku katika Mwezi huu Malaika wanawaombea Msamaha walofunga" Wenye Akili za ubishi wanaweza kuuliza mbona mambo yanajichanganya, huku hutoadhibiwa, hapa unaombewa msamaha inakuaje, Inatakiwa ujijue katika Maumbile yake wewe Binaadamu una (Past) na (Future) ambayo ukiambiwa huadhibiwi kwa yale yalopita, lakini haya yajayo ambayo unaendelea kuyatenda ndani ya Mwezi wa Ramadhan Mamia ya madhanbi, basi haya ndio hao Malaika wamewekwa kazi yao kukuombea Maghfira, Na kwa hilo basi zidi kuingia Furahani kwa kuijua Baraka hii ya kuombewa na Malaika.
Baraka ya Tatu (3) Hakika Mwenye enzi Mungu anaiamrisha Pepo na kuiambia," Ewe Pepo Mpambie Mja wangu mwenye kufunga aje kustarehe kwa zile taabu alozipata kwenye dunia ili apate yalo mazuri yaliyopo kwenye Nyumba ya peponi".
Asije kushangaa Mtu akaona mbona inasemezwa Pepo, kwani Pepo ni yenye kufahamu, Naam kila kilichoumbwa na Mollah kina (Degree of Consciousness).
Baraka ya Nne (4) Na harufu zao zitokazo vinywani mwao zinakua nzuri kuliko hata hiyo Misk(Manukato)
Na Baraka ya tano (5) Na kila ufikapo mwisho wa usiku  Mwenye enzi Mungu husamehe wote walofunga, na vile vitendo vyao walivyotenda, vitawafaa katika malipo ya ujira wao.
Hizo ndio Baraka tano zilizomo kwenye mwezi huu unazitaka zifanyie kazi, ondosha uvivu wa Ibada upate yalo mema, jitahidi kufunga uwe karibu na Mollah wako.

No comments:

Post a Comment