Asalaam Aleiykum
Ukifahamu Elimu ya Dini kwa undani utajua kuwa Dini ni msingi mzima wa maisha katika Ulimwengu huu, Bila ya Dini Mwanaadamu hana pakushika, hajui pakwenda, maisha kwake hayana umuhimu wowote na mwisho anamalizikia kupoteza (Akili).
Halafu kuna kinachofatia ni kile kilicho simamisha (Jengo) hili la Dini nayo ni hayo Matofali ya (Elimu) ya Sayansi, sasa nini wanasayansi wanafanya , kazi yao ni kuchunguza hili tofali limetengenezwa kwa kitu gani, kwa kuwa Nyumba imejengwa kwa Matofali mengi, na kila Tofali limetengenezwa kwa (Material) tafauti, wafanyacho wao Wanasayansi ni kuchambua, ambapo kwenye fani hii (Waislam) wamechangia pakubwa katika upatikanaji wa maelezo ya matofali hayo.
Viumbe tumepewa uwezo wa (Uchambuzi) ikisha tukaambiwa msije mkaringa na kuvimba kwa viburi (Hamkupewa ila Elimu chache sana). Kwa kuwa Ulimwengu huu ni mkubwa na mambo yake ni mengi yasokua na mwisho inatubidi kila kukivumbuliwa mambo mepya lazima tuyaseme, ili angalau wale walokua bado na Imani dhaifu linaweza kuwatingisha jambo kama hili na kuwashukia kitu katika nyoyo zao.
Ndio maana leo nikasema vikutanapo dini na sayansi sisi wenye matumaini ni lazima tufurahie jambo hili kwa sababu sayansi imetupa ushahidi wa kile tunachokiamini, japokua ushahidi wenyewe umepatikana kwa tabu lakini hatuna budi kuwaarifuni ili mpate uyakinifu wa jambo hili. Jambo hili limesemwa zamani na (Dini) zote lakini kwa kuwa Imani zetu ni dhaifu Mtu anasema inaweza kuwa kweli au uongo, hivyo ndivyo Imani zetu zilivyo.
Sasa matokeo kama haya ya Mkutano wa dini na sayansi kutokezea ni mara chache sana katika umuri wa mwanaadamu, wangapi wamekufa hawajawahi kuona (computer) na venginevyo, ndio maana nikasema mara chache sana, sasa hii ni nafasi kwa wale watopenda waijaze mioyo yao kwa Imani madhubuti ili ipate kuwarejesha kwa Mollah wao.
Nini Kimetokezea?
Endelea Part 2
Sunday, February 15, 2015
VIKUTANAPO DINI NA SAYANSI PART2
Asalaam Aleiykum
Mwanzoni mwa mwezi wa January wanasayansi wametangaza kupiga hatua japo kwa (Theory)na kutangaza kwamba kutokana na hesabu zao za uhakika sasa wanaamini kuna uwezekano mkubwa kuwa kuna Mlango Mbinguni ambao ikiwa tutaweza kuufikia kuutumia basi tunaweza kupita na kutokezea kwenye Ulimwengu mwengine(Usianze kukuna Kichwa ntakupa Link, ambayo unaweza kuzisoma habari hizo).(Http//Uk.news.yahoo.com/space-time-tunnel-milk-way-161910082.
hicho kiungo utazipata habari hizo na ripoti kamili.
Dini inasema nini kuhusiana na uvumbuzi huo. Kabla ya kutaja (Milango ya Mbingu) wacha kwanza tuihudhurie aya ya (12) ya sura ya (Talaq) tuone inatwambia nini kuhusu jambo hili.
ٱللَّهُ ٱلَّذِى خَلَقَ سَبۡعَ سَمَـٰوَٲتٍ۬ وَمِنَ ٱلۡأَرۡضِ مِثۡلَهُنَّ يَتَنَزَّلُ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنَہُنَّ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ قَدِيرٌ۬ وَأَنَّ ٱللَّهَ قَدۡ أَحَاطَ بِكُلِّ شَىۡءٍ عِلۡمَۢا
"Mwenye enzi Mungu ni Yule ambaye ameumba Mbingu saba, Na Ardhi kwa mfano wa hizo(Mbingu), Amri (zake) zinashuka baina yao, ili mjue kwamba Mwenye enzi Mungu amekizunguka kila kitu kukijua(Kwa elimu yake)".
Kwa Mwenye kutaka kusoma au kujua au kuongeza nguvu ya Imani yake, basi katika aya hii na habari hizo za wanasayansi kuna mazingatio makubwa kabisa yenye kukupa tamaa kwamba hicho unacho kiamini sio jambo la mzaha.
Mwenye Enzi Mungu ameumba Mbingu saba na Ardhi mfano kama huo, jamani mambo makubwa, Mtume s.a.w "Katika kisa cha (Miraji)" anasema nimetembea mimi katika mbingu zote Saba, Na nimepita katika Miji nikakuta watu wanateswa(Rejea Quraan aya ya Mwanzo sura ya Israa) iliposema na nukuu karibu ya mwisho "Ili Tumuoneshe baadhi (Tu) ya Alama zetu". Alikua yeye anatutajia mambo aloyakuta huko na kuyaona kwa macho yake katika hizo Ardhi zilizotajwa katika Quraan.
Lakini wapi wanaadamu ni wagumu kukubali au kuamini maelezo kama hayo, na wamesimama wengi katika hao wenye Imani ya Dini hii na kusema(Zilikua ndoto) za kisa cha Miraji, imekua leo hata hakizungumzwi kisa hichi kwa ajili baadhi ya kundi linaona hilo jambo haliwezekani.
Sasa Wanasayansi wanasema nini?
wasikize wanavosema kwa lugha yao(A Giant door way to another galaxy or universe may exist at the centre of the Milky way).
Quraan inasema kwenye sura ya Nabaa aya ya 19
"وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٲبً۬ا " Na Mbingu zitafunguliwa ziwe milango (Kwa) Milango.(A Wormhole in Milky way could lead to another Galaxy)(There could be a huge "Wormhole" at the centre of the Milky way).
Scientist Believe it would be possible to navigate through the wormhole.
Huku Mwenye enzi Mungu anasema Kaumba Mbingu saba na Ardhi mfano wake, Yeye ndiye aloleta hiyo dini na sayansi na anavikutanisha vitu viwili hivi ili kukuzidisha Imani wewe unaye kubali kuwa Mwenye enzi Mungu yupo na hayo yalosemwa na wajumbe wake ni kweli na wala huna shaka nayo.
Endelea part 3
Mwanzoni mwa mwezi wa January wanasayansi wametangaza kupiga hatua japo kwa (Theory)na kutangaza kwamba kutokana na hesabu zao za uhakika sasa wanaamini kuna uwezekano mkubwa kuwa kuna Mlango Mbinguni ambao ikiwa tutaweza kuufikia kuutumia basi tunaweza kupita na kutokezea kwenye Ulimwengu mwengine(Usianze kukuna Kichwa ntakupa Link, ambayo unaweza kuzisoma habari hizo).(Http//Uk.news.yahoo.com/space-time-tunnel-milk-way-161910082.
hicho kiungo utazipata habari hizo na ripoti kamili.
Dini inasema nini kuhusiana na uvumbuzi huo. Kabla ya kutaja (Milango ya Mbingu) wacha kwanza tuihudhurie aya ya (12) ya sura ya (Talaq) tuone inatwambia nini kuhusu jambo hili.
ٱللَّهُ ٱلَّذِى خَلَقَ سَبۡعَ سَمَـٰوَٲتٍ۬ وَمِنَ ٱلۡأَرۡضِ مِثۡلَهُنَّ يَتَنَزَّلُ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنَہُنَّ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ قَدِيرٌ۬ وَأَنَّ ٱللَّهَ قَدۡ أَحَاطَ بِكُلِّ شَىۡءٍ عِلۡمَۢا
"Mwenye enzi Mungu ni Yule ambaye ameumba Mbingu saba, Na Ardhi kwa mfano wa hizo(Mbingu), Amri (zake) zinashuka baina yao, ili mjue kwamba Mwenye enzi Mungu amekizunguka kila kitu kukijua(Kwa elimu yake)".
Kwa Mwenye kutaka kusoma au kujua au kuongeza nguvu ya Imani yake, basi katika aya hii na habari hizo za wanasayansi kuna mazingatio makubwa kabisa yenye kukupa tamaa kwamba hicho unacho kiamini sio jambo la mzaha.
Mwenye Enzi Mungu ameumba Mbingu saba na Ardhi mfano kama huo, jamani mambo makubwa, Mtume s.a.w "Katika kisa cha (Miraji)" anasema nimetembea mimi katika mbingu zote Saba, Na nimepita katika Miji nikakuta watu wanateswa(Rejea Quraan aya ya Mwanzo sura ya Israa) iliposema na nukuu karibu ya mwisho "Ili Tumuoneshe baadhi (Tu) ya Alama zetu". Alikua yeye anatutajia mambo aloyakuta huko na kuyaona kwa macho yake katika hizo Ardhi zilizotajwa katika Quraan.
Lakini wapi wanaadamu ni wagumu kukubali au kuamini maelezo kama hayo, na wamesimama wengi katika hao wenye Imani ya Dini hii na kusema(Zilikua ndoto) za kisa cha Miraji, imekua leo hata hakizungumzwi kisa hichi kwa ajili baadhi ya kundi linaona hilo jambo haliwezekani.
Sasa Wanasayansi wanasema nini?
wasikize wanavosema kwa lugha yao(A Giant door way to another galaxy or universe may exist at the centre of the Milky way).
Quraan inasema kwenye sura ya Nabaa aya ya 19
"وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٲبً۬ا " Na Mbingu zitafunguliwa ziwe milango (Kwa) Milango.(A Wormhole in Milky way could lead to another Galaxy)(There could be a huge "Wormhole" at the centre of the Milky way).
Scientist Believe it would be possible to navigate through the wormhole.
Huku Mwenye enzi Mungu anasema Kaumba Mbingu saba na Ardhi mfano wake, Yeye ndiye aloleta hiyo dini na sayansi na anavikutanisha vitu viwili hivi ili kukuzidisha Imani wewe unaye kubali kuwa Mwenye enzi Mungu yupo na hayo yalosemwa na wajumbe wake ni kweli na wala huna shaka nayo.
Endelea part 3
VIKUTANAPO DINI NA SAYANSI PART 3
Asalaam Aleiykum
Kwa hiyo pata uhakika kuwa Mbingu ziko Saba na Ardhi ziko Saba, Na kwamba Safari ya wewe kwenda Mbinguni ipo, na utakwenda kwenye Ulimwengu mwengine kama inavothibitisha Quraan Adh-Dhaariyat aya ya 22.
وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزۡقُكُمۡ وَمَا تُوعَدُونَ
Na Katika hiyo Mbingu kuna Riziki zenu na mliyoahidiwa.
Yaani kuhaidiwa huku ni hiyo Pepo au Moto katika huo Ulimwengu mwengine, sasa kama Imani yako inakupelekea kuwa maisha au Uhai wako unamalizikia hapa hapa Duniani basi tia shaka sana kwa jambo hilo, kwani ziko Ulimwengu nyengine na hatujui makaazi yetu yatakua wapi baada ya kuondoka kwenye Ulimwengu huu.
Wanasema wanasayansi ikiwa tunaweza kufanikiwa kupenya kwenye hiyo (Tunnel) tunaweza kutokezea kwenye Ulimwengu mwengine kabisa, Dini inasema tumeziumba hizo mbingu mnazoziona Tabaka baada ya Tabaka, hata mkifanikiwa kupenya kwenye hiyo ya pili basi kuna sita nyengine mfano wa hiyo mnoiona ambayo hamjafikia hata chembe katika uchunguzi wenu.
Na huo Mlango mnaousema kweli upo na wala hamkukosea, kuna viumbe wenzenu husogea karibu kusikiliza Amri zilizotolewa lakini huwapiga kwa (Missile)na kukimbia (Sura ya Mulk aya ya 5)
وَلَقَدۡ زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِمَصَـٰبِيحَ وَجَعَلۡنَـٰهَا رُجُومً۬ا لِّلشَّيَـٰطِينِۖ وَأَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابَ ٱلسَّعِيرِ
Kwa hakika tumeipamba Mbingu ya karibu hii kwa mataa, na Tumeyafanya ili kuwapiga mashetani, Na tumeweka tayari adhabu ya moto uwakao.
Naam hivyo ndivyo mambo yalivyo hapiti mtu kwenye hiyo Milango, wala hakuna awezaye kusikia Amri na siri za huko kwenye Ulimwengu wa Ajabu, kwenye Viumbe wengine wa Ajabu, Sasa Ikiwa Milango ishagunduliwa, jee wewe mpitaji ushajiandaa kwa safari ya huko, Na kama unasema safari ya (Miraji) ni ndoto, sasa tukuulize na Wanasayansi wanaota "Mchana" basi ikiwa habari hii imekushitua moyo wako basi nakuhimiza anza safari ya kumjua na kumtii Mollah wako ili upate furaha ya Milele, na Mapokezi yenye neema katika Ulimwengu mwengine wa Ajabu uliopo huko Juu kwenye Mbingu saba na Ardhi saba.
Kwa hiyo pata uhakika kuwa Mbingu ziko Saba na Ardhi ziko Saba, Na kwamba Safari ya wewe kwenda Mbinguni ipo, na utakwenda kwenye Ulimwengu mwengine kama inavothibitisha Quraan Adh-Dhaariyat aya ya 22.
وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزۡقُكُمۡ وَمَا تُوعَدُونَ
Na Katika hiyo Mbingu kuna Riziki zenu na mliyoahidiwa.
Yaani kuhaidiwa huku ni hiyo Pepo au Moto katika huo Ulimwengu mwengine, sasa kama Imani yako inakupelekea kuwa maisha au Uhai wako unamalizikia hapa hapa Duniani basi tia shaka sana kwa jambo hilo, kwani ziko Ulimwengu nyengine na hatujui makaazi yetu yatakua wapi baada ya kuondoka kwenye Ulimwengu huu.
Wanasema wanasayansi ikiwa tunaweza kufanikiwa kupenya kwenye hiyo (Tunnel) tunaweza kutokezea kwenye Ulimwengu mwengine kabisa, Dini inasema tumeziumba hizo mbingu mnazoziona Tabaka baada ya Tabaka, hata mkifanikiwa kupenya kwenye hiyo ya pili basi kuna sita nyengine mfano wa hiyo mnoiona ambayo hamjafikia hata chembe katika uchunguzi wenu.
Na huo Mlango mnaousema kweli upo na wala hamkukosea, kuna viumbe wenzenu husogea karibu kusikiliza Amri zilizotolewa lakini huwapiga kwa (Missile)na kukimbia (Sura ya Mulk aya ya 5)
وَلَقَدۡ زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِمَصَـٰبِيحَ وَجَعَلۡنَـٰهَا رُجُومً۬ا لِّلشَّيَـٰطِينِۖ وَأَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابَ ٱلسَّعِيرِ
Kwa hakika tumeipamba Mbingu ya karibu hii kwa mataa, na Tumeyafanya ili kuwapiga mashetani, Na tumeweka tayari adhabu ya moto uwakao.
Naam hivyo ndivyo mambo yalivyo hapiti mtu kwenye hiyo Milango, wala hakuna awezaye kusikia Amri na siri za huko kwenye Ulimwengu wa Ajabu, kwenye Viumbe wengine wa Ajabu, Sasa Ikiwa Milango ishagunduliwa, jee wewe mpitaji ushajiandaa kwa safari ya huko, Na kama unasema safari ya (Miraji) ni ndoto, sasa tukuulize na Wanasayansi wanaota "Mchana" basi ikiwa habari hii imekushitua moyo wako basi nakuhimiza anza safari ya kumjua na kumtii Mollah wako ili upate furaha ya Milele, na Mapokezi yenye neema katika Ulimwengu mwengine wa Ajabu uliopo huko Juu kwenye Mbingu saba na Ardhi saba.
Sunday, February 8, 2015
ALAMA TANO ZA ROHO PART 1
Asalaam Aleiykum
Binaadamu sote tuna uchu na hamu ya kujijua mimi ni nani, hivyo mimi ndio huu Mwili(Body)au kuna kitu chengine cha ziada kimejificha ndani ya Mimi ambacho sikijui, Na kama kipo Jee naweza kukijua?.
Utakaposema waweza kukijua unakua ushakipoteza zamani, lazima ujipe matumaini kuwa kinaweza kujulikana, kama inavo kufahamisha(Tawhid)siku zote uwezekano huo upo, lakini tatizo lake ni wewe unaogopa, unatishika huitaki kabisa elimu hii ya (Tawhid). Na sababu kubwa unajua elimu hii itakuonesha ukweli na siku utakapo uona ukweli, uongo wote utapotea, kwa sababu hivi sasa umo katika kuishi ndani ya uongo, umo katika kujificha unasubiri mpaka siku yako ya kufa ndio ujijue wewe nani?.
Siku ambayo itakapofika utatenganishwa na Mwili wako(Body) na kukumbuka Alaa kumbe mimi ni Roho, kumbe mimi sio mwili kama nilivokua najiona na kuringa nao, pengine utajiuliza hivyo kuna haja gani kuijua Roho yako hivi sasa? Haja iliyopo kwamba ukijijua kuwa wewe ni Roho kutabadilisha maisha yako na kuwa mtu mwengine kabisa, hutotenda dhanmbi kwa kusudi tena, na hiyo ndio khofu yako kubwa hutaki kubadilika.
Kwani Ukibadilika itabidi usithamini mali yako, dunia itakua haina umuhimu kwako, kiburi kitapeperuka kisionekane, kwa sababu ukiigundua Roho yako utakua mtupu, mweupe(Pure) hivyo ndivyo ilivyo Roho. Sasa wacha tuiweke upande Roho na tuzungumzie nguo za hiyo Roho ili tupate kukuonesha hizo Alama tano upate kuzifahamu. Kuzifahamu nguo hizo (Tawhid) inatufahamisha tusome sura ya Muuminun aya ya(12 mpaka 14).
" وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن سُلَـٰلَةٍ۬ مِّن طِينٍ۬ "
Hakika tulimuumba mwanaadamu kwa udongo ulio safi.
Asili yake ya mwanzo Mwanaadamu ni udongo msafi ambayo ndio hii ardhi, huna chengine ulicho valishwa isipokua hii Ardhi.
"ثُمَّ جَعَلۡنَـٰهُ نُطۡفَةً۬ فِى قَرَارٍ۬ مَّكِينٍ۬ "
Kisha tukamuumba kwa tone la manii(Mbegu ya Uzazi)lilowekwa katika makao yalohifadhika.
Kisha ukawekewa(System)kuwa nguo hizi kwa njia ya kuumbwa utakua unazivalia kwenye Tumbo la Mwanamke.
" ثُمَّ خَلَقۡنَا ٱلنُّطۡفَةَ عَلَقَةً۬ فَخَلَقۡنَا ٱلۡعَلَقَةَ مُضۡغَةً۬ فَخَلَقۡنَا ٱلۡمُضۡغَةَ عِظَـٰمً۬ا فَكَسَوۡنَا ٱلۡعِظَـٰمَ لَحۡمً۬ا ثُمَّ أَنشَأۡنَـٰهُ خَلۡقًا ءَاخَرَۚ فَتَبَارَكَ ٱللَّهُ أَحۡسَنُ ٱلۡخَـٰلِقِينَ "
Kisha tukalifanya tone hilo kuwa pande la damu, na tukalifanya pande la damu hilo kuwa pande la nyama, kisha tukalifanya pande la nyama hilo kuwa mifupa, na mifupa Tukaivika nyama, kisha tukamfanya kiumbe mwengine, Basi Ametukuka Mwenye enzi Mungu Mbora wa waumbaji.
Endelea part 2
Binaadamu sote tuna uchu na hamu ya kujijua mimi ni nani, hivyo mimi ndio huu Mwili(Body)au kuna kitu chengine cha ziada kimejificha ndani ya Mimi ambacho sikijui, Na kama kipo Jee naweza kukijua?.
Utakaposema waweza kukijua unakua ushakipoteza zamani, lazima ujipe matumaini kuwa kinaweza kujulikana, kama inavo kufahamisha(Tawhid)siku zote uwezekano huo upo, lakini tatizo lake ni wewe unaogopa, unatishika huitaki kabisa elimu hii ya (Tawhid). Na sababu kubwa unajua elimu hii itakuonesha ukweli na siku utakapo uona ukweli, uongo wote utapotea, kwa sababu hivi sasa umo katika kuishi ndani ya uongo, umo katika kujificha unasubiri mpaka siku yako ya kufa ndio ujijue wewe nani?.
Siku ambayo itakapofika utatenganishwa na Mwili wako(Body) na kukumbuka Alaa kumbe mimi ni Roho, kumbe mimi sio mwili kama nilivokua najiona na kuringa nao, pengine utajiuliza hivyo kuna haja gani kuijua Roho yako hivi sasa? Haja iliyopo kwamba ukijijua kuwa wewe ni Roho kutabadilisha maisha yako na kuwa mtu mwengine kabisa, hutotenda dhanmbi kwa kusudi tena, na hiyo ndio khofu yako kubwa hutaki kubadilika.
Kwani Ukibadilika itabidi usithamini mali yako, dunia itakua haina umuhimu kwako, kiburi kitapeperuka kisionekane, kwa sababu ukiigundua Roho yako utakua mtupu, mweupe(Pure) hivyo ndivyo ilivyo Roho. Sasa wacha tuiweke upande Roho na tuzungumzie nguo za hiyo Roho ili tupate kukuonesha hizo Alama tano upate kuzifahamu. Kuzifahamu nguo hizo (Tawhid) inatufahamisha tusome sura ya Muuminun aya ya(12 mpaka 14).
" وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن سُلَـٰلَةٍ۬ مِّن طِينٍ۬ "
Hakika tulimuumba mwanaadamu kwa udongo ulio safi.
Asili yake ya mwanzo Mwanaadamu ni udongo msafi ambayo ndio hii ardhi, huna chengine ulicho valishwa isipokua hii Ardhi.
"ثُمَّ جَعَلۡنَـٰهُ نُطۡفَةً۬ فِى قَرَارٍ۬ مَّكِينٍ۬ "
Kisha tukamuumba kwa tone la manii(Mbegu ya Uzazi)lilowekwa katika makao yalohifadhika.
Kisha ukawekewa(System)kuwa nguo hizi kwa njia ya kuumbwa utakua unazivalia kwenye Tumbo la Mwanamke.
" ثُمَّ خَلَقۡنَا ٱلنُّطۡفَةَ عَلَقَةً۬ فَخَلَقۡنَا ٱلۡعَلَقَةَ مُضۡغَةً۬ فَخَلَقۡنَا ٱلۡمُضۡغَةَ عِظَـٰمً۬ا فَكَسَوۡنَا ٱلۡعِظَـٰمَ لَحۡمً۬ا ثُمَّ أَنشَأۡنَـٰهُ خَلۡقًا ءَاخَرَۚ فَتَبَارَكَ ٱللَّهُ أَحۡسَنُ ٱلۡخَـٰلِقِينَ "
Kisha tukalifanya tone hilo kuwa pande la damu, na tukalifanya pande la damu hilo kuwa pande la nyama, kisha tukalifanya pande la nyama hilo kuwa mifupa, na mifupa Tukaivika nyama, kisha tukamfanya kiumbe mwengine, Basi Ametukuka Mwenye enzi Mungu Mbora wa waumbaji.
Endelea part 2
ALAMA TANO ZA ROHO PART 2
Asalaam Aleiykum
Vipi ukafanywa kuwa kiumbe Mwengine kwa kuwa sasa "Akampulizia Roho yake"(Sajjad aya ya 9)(ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِۦۖ) Alipopuliziwa hiyo Roho sasa Mwanaadamu akawa na sehemu mbili moja kutoka Ardhini na nyengine kutoka kwa Allah nao ni huo Utukufu wa Roho yako ulotokea kwa Mollah wako. Kukijua kitu hicho ni haki yako kwa sababu kama hujakijua wakati huu unaishi, basi jua utakijua siku ile ya kutolewa Roho yako, Na hakuna njia nyengine ya kujijua isipokua uzame kwenye Ibada, upotee kabisa sio kitendo cha mguu ndani mguu nje.
Kazi yangu mimi hapa kukuonesha hizo Alama kuwa kitu hicho kiitwacho Roho kipo na Alama zake ni hizi zitakazo kufanya ujijue wewe nani?. Alama hizo zenye kuonesha au kuashiria kuwapo kwa Roho ni zile bila ya wewe kuwa nazo ina maana wewe huna mahusiano na haya maisha kama tuyajuavyo. Alama zenyewe ni(1)Kuona(2)Kusikia(3)Kugusa(4)Kuhisi(5)Kunusa.
Ikitokea ukapoteza Alama hizo tano hapo Madaktari wa Ulimwengu huu wanatangaza na kutia saini kwamba wewe sasa ni (Maiti) na hufai kukaa na sisi tena, utatupa maudhi, ni lazima tuchukue dongo lako tukalifukie Ardhini, kwani kile kilichokua kina mahusiano na sisi kishaondoka(Sajjad aya 11)(قُلۡ يَتَوَفَّٮٰكُم مَّلَكُ ٱلۡمَوۡتِ ٱلَّذِى وُكِّلَ بِكُمۡ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُمۡ تُرۡجَعُونَ)."Sema; Atakufisheni Malaika wa Mauti aliyewakilishwa kwenu, kisha mtarejeshwa kwa Mollah wenu.
Kwa hiyo hapo inakujulisha huo Mwili ni Koti ambalo Roho linavaa na ukikamilika muda wake linavuliwa, (Unapata Elimu ya Tawhid ya juu kabisa isije ikakujia fikra naandika kwa matamanio yangu).
Naam, hiyo ndio Roho yenye kupita kwenye Uhai na Umauti, lakini kwenye (Life) Roho inaishi milele, ili hiyo Roho ihusiane na huo Mwili(Body) Mwenye Enzi Mungu akakupa vitu hivyo vitatu kwa vitano(Sajjad 9)ili upate kuwasiliana na Uhai huu tulo nao Mollah kakupa(وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَـٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ ) (Masikio)kusikia, Na (Macho)kuona, Na(Nyoyo)Kugusa,kuhisi,na kunusa.
Vipi vinafanya kazi vitu hivi?
Ndipo pale tunapata hizo Alama tano za kuwapo kwa Roho kutokana na zinavotuashiria kuwapo kwa (Mfalme) Mwenye kuutawala Mwili huu, Na huyo Mfalme yeye ndie mwenye uamuzi wote wa alitakalo kwenye Mji wake, sasa wacha tuingie kuzipekua Alama hizi tano ili zipate kutupa ishara za hicho kilojificha chenye Umiliki wa mambo yote haya ya nje na ndani. Kutokana na sifa hiyo lazima Utukufu wa kitu hichi utakurejesha kwa Mollah wako na kujijua kumbe mie Khalifa, kumbe mie nina uwezo kama huu kwanini siku zote nilikua Mtumwa natumikia Alama tano hizi, wakati kumbe hizi zipo kwa ajili ya kunitumikia mimi.
endelea part 3
Vipi ukafanywa kuwa kiumbe Mwengine kwa kuwa sasa "Akampulizia Roho yake"(Sajjad aya ya 9)(ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِۦۖ) Alipopuliziwa hiyo Roho sasa Mwanaadamu akawa na sehemu mbili moja kutoka Ardhini na nyengine kutoka kwa Allah nao ni huo Utukufu wa Roho yako ulotokea kwa Mollah wako. Kukijua kitu hicho ni haki yako kwa sababu kama hujakijua wakati huu unaishi, basi jua utakijua siku ile ya kutolewa Roho yako, Na hakuna njia nyengine ya kujijua isipokua uzame kwenye Ibada, upotee kabisa sio kitendo cha mguu ndani mguu nje.
Kazi yangu mimi hapa kukuonesha hizo Alama kuwa kitu hicho kiitwacho Roho kipo na Alama zake ni hizi zitakazo kufanya ujijue wewe nani?. Alama hizo zenye kuonesha au kuashiria kuwapo kwa Roho ni zile bila ya wewe kuwa nazo ina maana wewe huna mahusiano na haya maisha kama tuyajuavyo. Alama zenyewe ni(1)Kuona(2)Kusikia(3)Kugusa(4)Kuhisi(5)Kunusa.
Ikitokea ukapoteza Alama hizo tano hapo Madaktari wa Ulimwengu huu wanatangaza na kutia saini kwamba wewe sasa ni (Maiti) na hufai kukaa na sisi tena, utatupa maudhi, ni lazima tuchukue dongo lako tukalifukie Ardhini, kwani kile kilichokua kina mahusiano na sisi kishaondoka(Sajjad aya 11)(قُلۡ يَتَوَفَّٮٰكُم مَّلَكُ ٱلۡمَوۡتِ ٱلَّذِى وُكِّلَ بِكُمۡ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُمۡ تُرۡجَعُونَ)."Sema; Atakufisheni Malaika wa Mauti aliyewakilishwa kwenu, kisha mtarejeshwa kwa Mollah wenu.
Kwa hiyo hapo inakujulisha huo Mwili ni Koti ambalo Roho linavaa na ukikamilika muda wake linavuliwa, (Unapata Elimu ya Tawhid ya juu kabisa isije ikakujia fikra naandika kwa matamanio yangu).
Naam, hiyo ndio Roho yenye kupita kwenye Uhai na Umauti, lakini kwenye (Life) Roho inaishi milele, ili hiyo Roho ihusiane na huo Mwili(Body) Mwenye Enzi Mungu akakupa vitu hivyo vitatu kwa vitano(Sajjad 9)ili upate kuwasiliana na Uhai huu tulo nao Mollah kakupa(وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَـٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ ) (Masikio)kusikia, Na (Macho)kuona, Na(Nyoyo)Kugusa,kuhisi,na kunusa.
Vipi vinafanya kazi vitu hivi?
Ndipo pale tunapata hizo Alama tano za kuwapo kwa Roho kutokana na zinavotuashiria kuwapo kwa (Mfalme) Mwenye kuutawala Mwili huu, Na huyo Mfalme yeye ndie mwenye uamuzi wote wa alitakalo kwenye Mji wake, sasa wacha tuingie kuzipekua Alama hizi tano ili zipate kutupa ishara za hicho kilojificha chenye Umiliki wa mambo yote haya ya nje na ndani. Kutokana na sifa hiyo lazima Utukufu wa kitu hichi utakurejesha kwa Mollah wako na kujijua kumbe mie Khalifa, kumbe mie nina uwezo kama huu kwanini siku zote nilikua Mtumwa natumikia Alama tano hizi, wakati kumbe hizi zipo kwa ajili ya kunitumikia mimi.
endelea part 3
ALAMA TANO ZA ROHO PART 3
Asalaam Aleiykum
Vipi Alama hizi zinakujulisha itabidi ufanye juhudi Mwenyewe ya kugundua hicho kilicho kusudiwa, Alama zinaashiria kwa mfano huu!!, Wakati ule unapotizama unajua nani anaona?, Na kwanini nikataja kutizama na kuona? Kwa sababu kutizama ni (Action) na kuona ni (Attention)"Mfano" kwenye (Match) ya mpira unatizama wachezaji wote lakini (Attention) yako iko kwa yule mwenye mpira.
Na Kusikia hali kadhalika unasikia kila kitu, mtoto analia, gari inapita, ndege wanaimba, lakini (attention) yako yote iko kwenye (Nyimbo)yako unayosikiliza. Hiyo ndio maana ya neno (Nia) kwa lugha yetu ya kiswahili ambayo pia inahusu mengine yalosalia ya Kugusa na kuhisi(Mfano)ikiwa utapewa Halua unakula na huku unakanyaga msumari jiangalie (attention) yako itahamia wapi, nina hakika itahamia kwenye msumari kwa sababu Roho haipendi machungu, utaacha utamu wa halua ukashughulikie maumivu kwanza, sasa swali la kujiuliza nini hicho chenye kuhama kutoka katika jambo moja kwenda kwenye jambo la pili.
Na Harufu kadhalika mpaka ipatikane (Nia yako ya kunusa) ndio uvute harufu nzuri au sivyo mtu atajitia Udi mpaka apande shetani wewe husikii chochote umezama kwenye (Match) ya mpira au mkutano wa siasa.
Kwa hiyo kama ushalijua hilo la (Nia) muhimu sasa kuifanyia kazi nia yako mpaka ikufunulie Miliki yake ya Fahamu na kuijua kumbe hii ndio Roho, Na ukishajitambua hapo tena wewe utakua unaishi Ulimwengu mwengine kabisa wa hicho kitu kiitwacho (Bliss) na (Joy) na (Happiness) utakua Mfalme wa (Body) yako unatawala (sense) zote za kuona, kusikia, kusikia, kunusa na kuhisi.
Lakini kwa hivi sasa usihangaike bado hujawa mfalme, umo bado unatumikia hizo Alama za macho, unatumikia kusikiliza, unatumikia kugusa, unatumikia kunusa pamoja na kuhisi, umetawanyika kila sehemu unataka utumike wewe, hujatulia kabisa mara unazidiwa na kutamani, mara unazidiwa na kutizama, jitizame utaona vipi umetawaliwa na (sense) pengine nyimbo huwezi kuzikosa, labda vyakula vinakutesa, na mambo mengi ya kilimwengu yanakutesa yamekutawala huna uwezo wa kuyatawala mpaka ujigundue, Yakwamba wewe ni Roho na una uwezo wa kuyatawala hayo yote yakafata amri yako. Kumbuka zote hizo ni Alama zinaashiria jambo la kuwapo kwa Roho, kwa hiyo ifate alama moja baada ya moja ikupeleke kwenye Ufalme wako ili uwe mtulivu wa kufanya na kuamua mambo yako kwa umakini na hekima ulopewa na Mollah wako, Hiyo nia ndio itakufanya upate utulivu wa sala, kuepuka madhanbi, na hiyo ndio itakayoweza kukunusuru na adhabu na kuipata pepo.
Wacha zifanye kazi zote Alama tano lakini wewe Baki kwenye hicho chenye Umiliki wa hayo mambo matano, (Mfano) Umefunga Sala, wacha mawazo yaje, wacha uso ukuwashe wewe bakia kwenye sura ya (Fatiha) huku harufu zinanukia, wewe yapuuze yote ukiweza kufanya hivyo baada ya muda utajijua kumbe mimi sio vitu hivyo vyote ni kitu Maalum ambacho ukikijua utanyamaza kimya huku ukishangaa maajabu yake.
Vipi Alama hizi zinakujulisha itabidi ufanye juhudi Mwenyewe ya kugundua hicho kilicho kusudiwa, Alama zinaashiria kwa mfano huu!!, Wakati ule unapotizama unajua nani anaona?, Na kwanini nikataja kutizama na kuona? Kwa sababu kutizama ni (Action) na kuona ni (Attention)"Mfano" kwenye (Match) ya mpira unatizama wachezaji wote lakini (Attention) yako iko kwa yule mwenye mpira.
Na Kusikia hali kadhalika unasikia kila kitu, mtoto analia, gari inapita, ndege wanaimba, lakini (attention) yako yote iko kwenye (Nyimbo)yako unayosikiliza. Hiyo ndio maana ya neno (Nia) kwa lugha yetu ya kiswahili ambayo pia inahusu mengine yalosalia ya Kugusa na kuhisi(Mfano)ikiwa utapewa Halua unakula na huku unakanyaga msumari jiangalie (attention) yako itahamia wapi, nina hakika itahamia kwenye msumari kwa sababu Roho haipendi machungu, utaacha utamu wa halua ukashughulikie maumivu kwanza, sasa swali la kujiuliza nini hicho chenye kuhama kutoka katika jambo moja kwenda kwenye jambo la pili.
Na Harufu kadhalika mpaka ipatikane (Nia yako ya kunusa) ndio uvute harufu nzuri au sivyo mtu atajitia Udi mpaka apande shetani wewe husikii chochote umezama kwenye (Match) ya mpira au mkutano wa siasa.
Kwa hiyo kama ushalijua hilo la (Nia) muhimu sasa kuifanyia kazi nia yako mpaka ikufunulie Miliki yake ya Fahamu na kuijua kumbe hii ndio Roho, Na ukishajitambua hapo tena wewe utakua unaishi Ulimwengu mwengine kabisa wa hicho kitu kiitwacho (Bliss) na (Joy) na (Happiness) utakua Mfalme wa (Body) yako unatawala (sense) zote za kuona, kusikia, kusikia, kunusa na kuhisi.
Lakini kwa hivi sasa usihangaike bado hujawa mfalme, umo bado unatumikia hizo Alama za macho, unatumikia kusikiliza, unatumikia kugusa, unatumikia kunusa pamoja na kuhisi, umetawanyika kila sehemu unataka utumike wewe, hujatulia kabisa mara unazidiwa na kutamani, mara unazidiwa na kutizama, jitizame utaona vipi umetawaliwa na (sense) pengine nyimbo huwezi kuzikosa, labda vyakula vinakutesa, na mambo mengi ya kilimwengu yanakutesa yamekutawala huna uwezo wa kuyatawala mpaka ujigundue, Yakwamba wewe ni Roho na una uwezo wa kuyatawala hayo yote yakafata amri yako. Kumbuka zote hizo ni Alama zinaashiria jambo la kuwapo kwa Roho, kwa hiyo ifate alama moja baada ya moja ikupeleke kwenye Ufalme wako ili uwe mtulivu wa kufanya na kuamua mambo yako kwa umakini na hekima ulopewa na Mollah wako, Hiyo nia ndio itakufanya upate utulivu wa sala, kuepuka madhanbi, na hiyo ndio itakayoweza kukunusuru na adhabu na kuipata pepo.
Wacha zifanye kazi zote Alama tano lakini wewe Baki kwenye hicho chenye Umiliki wa hayo mambo matano, (Mfano) Umefunga Sala, wacha mawazo yaje, wacha uso ukuwashe wewe bakia kwenye sura ya (Fatiha) huku harufu zinanukia, wewe yapuuze yote ukiweza kufanya hivyo baada ya muda utajijua kumbe mimi sio vitu hivyo vyote ni kitu Maalum ambacho ukikijua utanyamaza kimya huku ukishangaa maajabu yake.
Sunday, February 1, 2015
SIRI YA KUSOMA PART 1
Asalaam Aleiykum
Nini Kusoma? Ushapata kujiuliza swali hili na kupata jawabu lake, basi kama bado wacha nikuchukue katika safari hii ya kushangaza ambayo inakutoa kwenye kiza kukupeleka kwenye Nuru, Safari ambayo ikiwa mwenye upeo wa kufahamu italeta Mapinduzi kwenye maisha yako. Binaadamu umeumbwa kila kitu chako kinafanya kazi kwa mwenendo wa aina mbili (Mfano)kama vile kuvuta pumzi na kuzitoa, kulala na kuamka na mengi mengine yenye kujulikana na yasojulikana. Na hili la kusoma pia lina mwenzie, na hapa leo ndio msingi wetu mzima wa darsa hii ili upate kumsaidia kila mmoja wetu apate faida na maana halisi ya kusoma.
Ikiwa utafata Muongozo huu basi utakua mwenye kufahamu kwa urahisi kila unacho fundishwa, utapata kitu kiitwacho hekima na kuyajua mambo mengi kwenye Ulimwengu huu.
Darsa hii itawasaidia wale wlioko (Ma-School)kwenye vyuo, nyumba za Ibada na kwengineko, Na kwa wale wenye kutaka kuhimili(Nyenzo)hii kwa manufaa yao wenyewe. Itabidi mnipe Ruhusa nikupeni changa moto ya kuifanyia kazi kabla ya kuendelea na ufafanuzi wetu, na changa moto ya leo ni kukuuliza hivyo ushawahi kujiuliza kwanini(Mtoto mdogo anafahamu haraka)?Na vile vile kwanini watu wazima hawazungumzi sana?. Ukipata majawabu mawili hayo wewe ushaingia katika siri ya kusoma, na kama bado, wacha sasa tuingie kwenye darsa yakusoma na moja kwa moja naazima neno kutoka katika kitabu cha (Injili-John-16-13)"(Nina mengi ya kusema kwenu nyinyi,Lakini hamuwezi kufahamu hivi sasa, Lakini yule (Spirit)Mjumbe wa ukweli atakapokuja,atakuongozeni katika Ukweli Mtupu,Kwa sababu yeye hatosema kwa matamanio ya (Nafsi) yake, lakini atakwambieni chochote atakachosikia, atakwambieni na kukupeni habari za mambo yajayo, atanitaja kwa kuninyanyua(jina langu)) atachukua yalo yangu na kukufungulieni nyinyi)".Sasa narejea kwenye Quraan nipate kuiliza nayo inasema nini kuhusu Mjumbe huyu wa kweli?, sura ya (Najm aya ya 3-4)"وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ ""Wala hasemi kwa matamanio(Ya nafsi)""Hayakua haya (anayosema)ila ni Wahyi ulofunuliwa(Kwake)".
Sasa kwanini nikataja aya mbili hizo kutoka katika vitabu viwili tafauti, kwa sababu ndio msingi mzima wa kukuonesha hiyo siri ya kusoma imetokea wapi. Sasa nataka utupie macho hilo neno la kwenye (Injili) linalosema "Lakini atakwambieni chochote atakachosikia", anasema Mtume s.a.w unapokuja huo (Wahyi)"(Nasikia kama sauti inanijaa kwenye Kichwa changu na unapomalizika hiyo (Sound)(Wahyi) tayari nakua nishasoma), Hiyo ndio maana ya (Iqraa)"Sio kwamba Mollah hakujua Mtume wake hajui kusoma kama wanavosema wengine" Bali alikua anapewa Amri ya kusikiliza hicho atakachosomewa, Na kusikiliza ndio mwenza wa kusoma, bila ya kusikiliza tabu sana kusoma, Na"Hapo kuna hiyo siri yenyewe, nayo ni hiyo kusikia" na hii kila Mwanaadamu anao uwezo huu wa kusikia, ndio utaona hata hiyo (System) ya (Wahyi) inamjia Mtume s.a.w kwa njia ya kusikia, na ndio maana na nyinyi mkaambiwa katika Quran aya ya (204)sura ya (Aaraf)"وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ"
Inaposomwa Quran isikilizeni nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Kwanini mkaambiwa sikilizeni na Nyamazeni? Kwa Sababu (Method) hiyo hiyo inayotumika kwenye Quraan na ilosemwa kwenye (Injili) inatumika pia kwenye masomo mengine yote.
Sasa kwanini mkaambiwa sikilizeni? Endelea part 2
Nini Kusoma? Ushapata kujiuliza swali hili na kupata jawabu lake, basi kama bado wacha nikuchukue katika safari hii ya kushangaza ambayo inakutoa kwenye kiza kukupeleka kwenye Nuru, Safari ambayo ikiwa mwenye upeo wa kufahamu italeta Mapinduzi kwenye maisha yako. Binaadamu umeumbwa kila kitu chako kinafanya kazi kwa mwenendo wa aina mbili (Mfano)kama vile kuvuta pumzi na kuzitoa, kulala na kuamka na mengi mengine yenye kujulikana na yasojulikana. Na hili la kusoma pia lina mwenzie, na hapa leo ndio msingi wetu mzima wa darsa hii ili upate kumsaidia kila mmoja wetu apate faida na maana halisi ya kusoma.
Ikiwa utafata Muongozo huu basi utakua mwenye kufahamu kwa urahisi kila unacho fundishwa, utapata kitu kiitwacho hekima na kuyajua mambo mengi kwenye Ulimwengu huu.
Darsa hii itawasaidia wale wlioko (Ma-School)kwenye vyuo, nyumba za Ibada na kwengineko, Na kwa wale wenye kutaka kuhimili(Nyenzo)hii kwa manufaa yao wenyewe. Itabidi mnipe Ruhusa nikupeni changa moto ya kuifanyia kazi kabla ya kuendelea na ufafanuzi wetu, na changa moto ya leo ni kukuuliza hivyo ushawahi kujiuliza kwanini(Mtoto mdogo anafahamu haraka)?Na vile vile kwanini watu wazima hawazungumzi sana?. Ukipata majawabu mawili hayo wewe ushaingia katika siri ya kusoma, na kama bado, wacha sasa tuingie kwenye darsa yakusoma na moja kwa moja naazima neno kutoka katika kitabu cha (Injili-John-16-13)"(Nina mengi ya kusema kwenu nyinyi,Lakini hamuwezi kufahamu hivi sasa, Lakini yule (Spirit)Mjumbe wa ukweli atakapokuja,atakuongozeni katika Ukweli Mtupu,Kwa sababu yeye hatosema kwa matamanio ya (Nafsi) yake, lakini atakwambieni chochote atakachosikia, atakwambieni na kukupeni habari za mambo yajayo, atanitaja kwa kuninyanyua(jina langu)) atachukua yalo yangu na kukufungulieni nyinyi)".Sasa narejea kwenye Quraan nipate kuiliza nayo inasema nini kuhusu Mjumbe huyu wa kweli?, sura ya (Najm aya ya 3-4)"وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ ""Wala hasemi kwa matamanio(Ya nafsi)""Hayakua haya (anayosema)ila ni Wahyi ulofunuliwa(Kwake)".
Sasa kwanini nikataja aya mbili hizo kutoka katika vitabu viwili tafauti, kwa sababu ndio msingi mzima wa kukuonesha hiyo siri ya kusoma imetokea wapi. Sasa nataka utupie macho hilo neno la kwenye (Injili) linalosema "Lakini atakwambieni chochote atakachosikia", anasema Mtume s.a.w unapokuja huo (Wahyi)"(Nasikia kama sauti inanijaa kwenye Kichwa changu na unapomalizika hiyo (Sound)(Wahyi) tayari nakua nishasoma), Hiyo ndio maana ya (Iqraa)"Sio kwamba Mollah hakujua Mtume wake hajui kusoma kama wanavosema wengine" Bali alikua anapewa Amri ya kusikiliza hicho atakachosomewa, Na kusikiliza ndio mwenza wa kusoma, bila ya kusikiliza tabu sana kusoma, Na"Hapo kuna hiyo siri yenyewe, nayo ni hiyo kusikia" na hii kila Mwanaadamu anao uwezo huu wa kusikia, ndio utaona hata hiyo (System) ya (Wahyi) inamjia Mtume s.a.w kwa njia ya kusikia, na ndio maana na nyinyi mkaambiwa katika Quran aya ya (204)sura ya (Aaraf)"وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ"
Inaposomwa Quran isikilizeni nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Kwanini mkaambiwa sikilizeni na Nyamazeni? Kwa Sababu (Method) hiyo hiyo inayotumika kwenye Quraan na ilosemwa kwenye (Injili) inatumika pia kwenye masomo mengine yote.
Sasa kwanini mkaambiwa sikilizeni? Endelea part 2
SIRI YA KUSOMA PART 2
Asalaam Aleiykum
Kusikiliza ndio (Mama) wa masomo nataraji mliopo kwenye madarsa na vyuoni mtachukua (siri) hii ili ikusaidieni na kupata faida kubwa kabisa.
Mwanaadamu una nyenzo mbili za ufanyaji kazi kwa kutumia Sauti, nyenzo ya kwanza ni ile ya kusema kwa kutumia sauti, Na ya pili ni ile ya kusikiliza, moja unatoa sauti na ya pili unatia sauti, unaposema au kuzungumza huwezi kusikiliza wakati mmoja, lazima unyamaze ndio uweze kusikiliza, Sasa kwanini ukaambiwa utulie unaposomewa kitu, kwa sababu (Any Movement inside) inatingisha Akili, Na Akili ikitingishwa ina mambo mengi ya mawazo. Nini Mawazo ? Mawazo ni mzungumzaji wako wa ndani, ukikosa Mtu nje unamualika rafiki yako mawazo mnaanza kuongea, unaweza kuwa nje umenyamaza kumbe ndani ya Akili yako una hutubia mkutano wa hadhara, Mwalimu anasomesha na wewe huko mawazoni unasomesha inakua hapo wewe husomi ila unashindana na Mwalimu kusomesha, na huku unabakia kusindikiza Darasa.
Kwa kuwa (University) au taasisi nyengine umelipa pesa basi hawawezi kukufelisha kwa hiyo wanakupa (cheti) Shahada ambayo haina faida yoyote huwezi kuleta maendeleo kwa sababu hujasoma,
Na kichwani umebaki mweupe. Sasa Siri yenyewe ni lazima ujifundishe kunyamaza kimya ndani ya kichwa chako kwenye Akili.
Endelea part 3
Kusikiliza ndio (Mama) wa masomo nataraji mliopo kwenye madarsa na vyuoni mtachukua (siri) hii ili ikusaidieni na kupata faida kubwa kabisa.
Mwanaadamu una nyenzo mbili za ufanyaji kazi kwa kutumia Sauti, nyenzo ya kwanza ni ile ya kusema kwa kutumia sauti, Na ya pili ni ile ya kusikiliza, moja unatoa sauti na ya pili unatia sauti, unaposema au kuzungumza huwezi kusikiliza wakati mmoja, lazima unyamaze ndio uweze kusikiliza, Sasa kwanini ukaambiwa utulie unaposomewa kitu, kwa sababu (Any Movement inside) inatingisha Akili, Na Akili ikitingishwa ina mambo mengi ya mawazo. Nini Mawazo ? Mawazo ni mzungumzaji wako wa ndani, ukikosa Mtu nje unamualika rafiki yako mawazo mnaanza kuongea, unaweza kuwa nje umenyamaza kumbe ndani ya Akili yako una hutubia mkutano wa hadhara, Mwalimu anasomesha na wewe huko mawazoni unasomesha inakua hapo wewe husomi ila unashindana na Mwalimu kusomesha, na huku unabakia kusindikiza Darasa.
Kwa kuwa (University) au taasisi nyengine umelipa pesa basi hawawezi kukufelisha kwa hiyo wanakupa (cheti) Shahada ambayo haina faida yoyote huwezi kuleta maendeleo kwa sababu hujasoma,
Na kichwani umebaki mweupe. Sasa Siri yenyewe ni lazima ujifundishe kunyamaza kimya ndani ya kichwa chako kwenye Akili.
Endelea part 3
SIRI YA KUSOMA PART 3
Asalaam Aleiykum
Sio ujifundishe kufunga mdomo tu bali kichwani uwe (Empty) hakuna mawazo mengine yanayopenya ila kwa lile unalofundishwa au kusomeshwa. Ukiweza Ku(Master Art) hii ya kusikiliza wewe utakua tayari Msomi, Na kila kitachofundishwa au kusomeshwa kitaingia ndani na kukaa kwa ufahamu wa hali ya juu na huko ndiko kurehemewa kulikotajwa katika (Quraan).
Kwa jinsi hiyo ndivyo kinavokaa kwa mtoto mdogo, sababu mtoto mdogo hana mawazo wala haongei kwenye Akili yake, ila yeye ana (Art) ya kusikiliza kwa makini ikiwa una uwezo wa kumuangalia mtoto mdogo mtizame anavo kusikiliza. Kwa kuwa wewe ni mtu mzima sasa ukiwa msikilizaji mzuri utaona unaanza kuzaa (Hekima) wala hujui inatokea wapi.
Ukiulizwa swali moja kwa moja unapewa na jawabu tayari ndani kwa ndani, Lakini inatakiwa kazi kubwa ifanyike kujifundisha tena kusikiliza, kazi pevu ifanyike kujifunza tena kunyamaza, lakini inawezekana ukiifanyia mazoezi ya kila siku, sasa hivi bado usikurupuke ukaanza kuona ushaweza, Jitizame mwenyewe huku unasoma, kichwani unazungumza, unapata matatizo matupu, ukimaliza (Class) unasema sijafahamu kitu, utafahamu vipi na wewe umemeza (cassete), Huku watu wanasema Maskini kajikalia kimya, kumbe wewe kichwani una mambo chungu nzima unayajadili.
Mpaka upate uwezo wa kukaa kimya nje na ndani ndipo Elimu itaingia, Hekima itakushukia, Sala yako itatimia, lakini kwanza lazima ujifunze tena kusikiliza, Iwe ndani ya akili hakiingii chochote isipokua yale unayo someshwa, lakini ikiwa Mwalimu anasomesha na wewe unamjibu na katika sauti ya ukimya basi haipatikani faida ya kusoma, kwenye sauti ya ukimya kazi yake kusikiliza na wala sio kuzungumza. Faida na siri ya kufahamu inapatikana ndani ya ukimya wako wa nje na ndani ya Akili, na hiyo ndio siri ya kusoma kwa mwenye kuitaka.
Kumbuka siku zote Elimu inakuja kutokea nje, Ila kufahamu pekee ndio kunatokea ndani.
Sio ujifundishe kufunga mdomo tu bali kichwani uwe (Empty) hakuna mawazo mengine yanayopenya ila kwa lile unalofundishwa au kusomeshwa. Ukiweza Ku(Master Art) hii ya kusikiliza wewe utakua tayari Msomi, Na kila kitachofundishwa au kusomeshwa kitaingia ndani na kukaa kwa ufahamu wa hali ya juu na huko ndiko kurehemewa kulikotajwa katika (Quraan).
Kwa jinsi hiyo ndivyo kinavokaa kwa mtoto mdogo, sababu mtoto mdogo hana mawazo wala haongei kwenye Akili yake, ila yeye ana (Art) ya kusikiliza kwa makini ikiwa una uwezo wa kumuangalia mtoto mdogo mtizame anavo kusikiliza. Kwa kuwa wewe ni mtu mzima sasa ukiwa msikilizaji mzuri utaona unaanza kuzaa (Hekima) wala hujui inatokea wapi.
Ukiulizwa swali moja kwa moja unapewa na jawabu tayari ndani kwa ndani, Lakini inatakiwa kazi kubwa ifanyike kujifundisha tena kusikiliza, kazi pevu ifanyike kujifunza tena kunyamaza, lakini inawezekana ukiifanyia mazoezi ya kila siku, sasa hivi bado usikurupuke ukaanza kuona ushaweza, Jitizame mwenyewe huku unasoma, kichwani unazungumza, unapata matatizo matupu, ukimaliza (Class) unasema sijafahamu kitu, utafahamu vipi na wewe umemeza (cassete), Huku watu wanasema Maskini kajikalia kimya, kumbe wewe kichwani una mambo chungu nzima unayajadili.
Mpaka upate uwezo wa kukaa kimya nje na ndani ndipo Elimu itaingia, Hekima itakushukia, Sala yako itatimia, lakini kwanza lazima ujifunze tena kusikiliza, Iwe ndani ya akili hakiingii chochote isipokua yale unayo someshwa, lakini ikiwa Mwalimu anasomesha na wewe unamjibu na katika sauti ya ukimya basi haipatikani faida ya kusoma, kwenye sauti ya ukimya kazi yake kusikiliza na wala sio kuzungumza. Faida na siri ya kufahamu inapatikana ndani ya ukimya wako wa nje na ndani ya Akili, na hiyo ndio siri ya kusoma kwa mwenye kuitaka.
Kumbuka siku zote Elimu inakuja kutokea nje, Ila kufahamu pekee ndio kunatokea ndani.
Subscribe to:
Posts (Atom)