Friday, March 3, 2017

KIDOLE KINAONESHA MBINGUNI PART 3

Asalaam Aleiykum

Wale wenye kuhudhuria Umauti wa mtu wanajua au wanofanya kazi (Hospital)Wanajua Mtu akiwa anakufa Macho yanabiruka na kutizama Mbinguni au ita Juu, Kidole kinatwambia nini kuhusu swali hili,( Quraan aya ya 22 sura ya Adh-Dhaariyat)
وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزۡقُكُمۡ وَمَا تُوعَدُونَ 
"Na Katika Mbingu ziko Riziki zenu na Mliyoahidiwa".
Kuanzia leo Ukitizama Mbinguni ujue kule ndio inakopangwa Riziki yako upate ngapi, uwe na nini? na kiasi gani, kule Mbinguni ndiko tunanyanyua Mikono yetu kuonesha uwazi wa viganja vyetu kwa kuomba tukitaraji kupewa na Mollah wetu, Huko Mbinguni ndiko tunakotoa sauti zetu zisikike ili tupate kujibiwa dua zetu(Vipi leo mnatwambia tunyamaze kimya)huko huko Mbinguni ndiko siku ya kufa kwako unapelekwa na Malaika kama (Destination)ya mapumziko katika Makaazi yaitwayo(Barzaak).
Kwa hiyo ukiwa unatizama Mbinguni napenda uelewe yale Mloahidiwa mabaya ya (Moto)Na Mazuri ya (Pepo)yote yako huko, kwa hiyo kaa ukijua Safari unayo ya Kwenda Mbinguni, nasisitiza usije kuangalia Kidole, kwani kidole kinabaki hapa hapa ila tizama kinaonesha wapi. Kaa tayari kusikia Miujiza zaidi itokayo huko, Pata faida usikize kisa cha Miraji ili upate uyakinifu wa hayo yaloonekana huko Mbinguni ambayo na wewe hakuna shaka utakwenda kuyaona.

No comments:

Post a Comment