Wednesday, November 1, 2017

NJIA YA KUMKUMBUKA ALLAH PART 3

Asalaam Aleiykum

Amesema Mwenye Enzi Mungu katika sura ya (Adh-Dhariyat-56)"وَمَا خَلَقۡتُ ٱلۡجِنَّ وَٱلۡإِنسَ إِلَّا لِيَعۡبُدُونِ"
"Sikuwaumba Majini na Watu ila wapate kuniabudu"
Sikuwaumba kwa ajili yoyote, ila nimewapa (Choice)wakitaka waniabudu watakua wamechagua Pepo wenyewe, Na wasipotaka na kukataa watakua wamechagua njia yao itakayo wapeleka kwenye mateso, kwani kwenda kinyume cha Maumbile(Nature)ya Ulimwengu huu utakua umechagua kinyume na atakavyo alokuumba.
Sasa kuipata hiyo Ibada yenyewe lazima uviunganishe vitu viwili nilivyovitaja vya Fikra na Kukumbuka yaani (Roho Na Akili) Vikiungana hivyo ndio unapata huo Unyenyekevu, Akili haiyumbi tena, Vipi Akili itayumba wakati daima uko mbele ya Mollah wako, Na Mbele ya Mollah lazima upate na Unyenyekevu, Na huku Duniani wakikuona wanahisi kuna kitu (kimetokezea)ndio wakikuuliza kitu mbona imekua hivi, au wakibishana na wewe huna la kusema ila unawaambia Salaam(Peace).
Kwa habari hii nilokupeni na ikiwa umeipokea sawa sawa na sasa na wewe unataka kuanza kuipata hali kama hiyo, Basi chukua moja katika majina 99 ya Mwenye Enzi Mungu halafu litaje (Non Stop) kwa miezi mitatu ikisha (Stop) baada ya hapo ndio utafunguliwa hiyo (Nameless) ya kukumbuka daima, Nje utakua Binaadamu wa kawaida lakini ndani kiumbe mwengine kabisa, kila kitu kinafunguliwa kwako, na ukiipata hali kama hiyo utakua ushaipata hiyo njia, Na njia hiyo ndio hiyo inotajwa (Mustaqim)ambayo inakupeleka kwa Mollah wako ukiwa safi umesafishika na dhanmbi zote ulizozifanya huko nyuma. Na Mollah ndie ajuae zaidi.






No comments:

Post a Comment