Tuesday, February 24, 2026

NJIA YA KUIPATA SALA

 Aslm alekum.  Aina ya kwanza ni kupata uongofu wa taa ya Mollah wako ukaacha hapo hapo na aina ya pili ndio hii aya mloileta kwenye swali lenu kutoka kwenye aya ya 45 sura ya Ankabbot? Linasema hivi: 


ٱتۡلُ مَآ أُوحِيَ إِلَيۡكَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَۖ إِنَّ ٱلصَّلَوٰةَ تَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِۗ وَلَذِكۡرُ ٱللَّهِ أَكۡبَرُۗ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تَصۡنَعُونَ"Soma uliyoletewa Wahyi Katika kitabu na usimamishe Sala, Bila shaka (Sala ikisaliwa vizuri)Humzuiliya anaye sali na mambo machafu na maovu, na kwa yakini kumkumbuka Mwenye enzi Mungu ni jambo kubwa kabisa, na Mwenye enzi Mungu anajua mnayoyatenda"   Naam ukweli wenyewe hii aya imeshajibu swali lenu lakini tunapishana katika ufahamu,  Tatizo liko kwenye hiyo sala  unaisali vipi?. Imepambanua hii aya halafu jibu rasmi tutalipata kwenye aya nyengine lenye kuitilia nguvu aya hii twende taratibu usikurupuke utakua hujafahamu kitu, najua litawagusa hili lakini itanibidi mnipe nafasi nifafanue kidogo ili mpate kuamka usingizini, pengine mja bado kalala japo  anajiona yuko macho.Sala ziko za aina mbili aina ya  mwanzo ni ile inotegemea Akili na aina nyengine ni ile  inayo saliwa na Roho, hii ya Akili ndio wengi wetu Muadhini akinadi sote tunakimbilia msikitini na hapo vinaendelea vitendo vitupu ndio maana utajikuta mara upo bank mara upo ofisini, mara unamfikiri mkeo mara unakumbuka madeni,  mara chache sana kuipata Sala yenyewe ndio maana ukitoka hapo unakwenda kuendelea na vitendo vyako viovu na machafu ya kuzini, kula rushwa kudhulumu kuiba, kusema uongo na kudhulumu masikini haki zao na hali ya kuwa umetokea msikitini kwa sababu kwenye hiyo sala yenywe wewe hupo kabisa madeni yanakuja hapo, Mara unamdai mtu hii ndani ya sala Mollah wako ulomuendea humkumbuki kabisa, Lakini yeye Ana kusubiri kwenye enzi ya       kusubiri , anakungoja labda utatubia,bado umo kwenye Level ya kwanza ya Uislam,unajua kwanini? K  kwa   sababu Huzijui (Level)ya  sala yenywe. Salah ina (Level 3) Sala ya mwanzo ndio niliitaja hapo juu ni (Level 1), na (Level 2) ya pili Hii ni ya Muumin  (Fii Salat Ghashiun)Sala hii sasa niya  unyenyekevu (Empty) hakiji kitu ndani ya Sala isipokua kumsabahi Mollah na kumtukuza hayaji mambo ya kidunia kabisa, Hii ndio ile Sala ya (Ghaib)ilothibiti Imani na matumaini  halafu kuna hii (Level 3) Sala ya (Shahadat)ambayo hiyo imejaa (Taqwa)Mwanzo mpaka mwisho wa hiyo Sala  inasaliwa Kiroho ndio za Mawalii na wacha Mungu wakweli  mara utamuona mtu machozi yana miminika kwa sababu Sala imegusa kitu kisicho onekana. Kwenye (Level) hii wewe unageuka kuwa Shahid na hiyo ndio iwe (Target) yako ungali ukiishi kwenye Ulimwengu huu, Na Wakati wa kufa kwako, Naam sala hii inapatikanaje hapa nitakupeni(Dalili) halafu utaangalia mwenyewe unasali vipi kiroho au kutumia Akili. Aya inasema "Soma katika uliyoletewa wahyi katika kitabu na usimamishe Sala"Ulipoambiwa Soma umefundishwa uzingatie yaliyomo kwenye hichi kitabu ndio iwe muongozo wako ndio iwe taa yako, hayo utakayo yasoma ndio yatakufundisha usiibe, usizini, usidhulumu, usiseme uongo, usidhuru wenzio, usile rushwa, yaani kila ukisoma basi utakuta kuna mafundisho ambayo itakua muongozo na ndio taa yako itakayo kuepusha kwenye msitu wa  mchana wa hayo machafu na maovu quraan itakua inakushitua, usome wahyi huu, halafu ukishasoma ufanye nini? Udumishe kumkumbuka Mollah wako aliye Mkubwa, kwanini ikawa umkumbuke kwa sababu ni jambo kubwa kabisa kivipi?Ukimkumbuka Mollah wako kila mara utaona kuna vitu viwili  tafauti moja ni Sala na na la pili kukumbuka.nini kukumbuka? Ni (Awareness )(Hadhir)na  unapofanya hivyo huipi Akili kupenyeza jambo lengine na Akili ikiwa haipewi nafasi inafanya nini? Ina kufa(au kutulia) Akili ikifa ndio mwanzo wakufunguliwa juu yako mambo mengine, (Elimu zengine)(Na Hekima nyingi)Sala yako sasa itakua tafauti,  ucha Mungu wako unakua wa hali ya juu ila kufikia hali hiyo inabidi usubiri mlangoni kwenye kukumbukuka, kuna mambo mawili Mwanaadamu Huna uwezo nayo huwezi kuyatafuta ila yanakutafuta wewe,  Kifo na Mapenzi viwili hivyo Huna uwezo navyo kabisa lakini kaa mlangoni gonga mlango asaa utafunguliwa itumie quraan au yatumie Majina 99 ya Mwenye enzi Mungu mlango ukifunguliwa utaacha machafu yote na maovu yote na utakua unapata Sala yako kikamilifu na aya inamalizia kuwa Mwenye enzi Mungu anayajua yote mnayoyatenda. Huo ndio Muongozo wa mwanzo kwenye hiyo aya mloleta, ama aya ya pili inayokupa    nguvu zaidi ni hii aya ya 3.3b

No comments:

Post a Comment