Aslm alekum. Limekuja . Swali wameniomba muongozo japo kidogo ili na sisi wasomaji wako tupate faida. Na swali la lenyewe tunakuomba tupe uchambuzi wa aya ya 45 iliyomo kwenye sura ya (An-Kabut)Tunaomba ufafanuzi kwa sababu aya hiyo inasema Sala inatuepusha na machafu na maovu, Na sisi tunasali kama wengine wanavosali, ila sisi bado tunaendelea na maasi na machafu, Na hali hii inaendelea miaka nenda miaka rudi na tumeshindwa kabisa kujivua katika katika kadhia hii ya uchafu na maovu. Naam Kwanza kabisa wacha niweke wazi mimi ni msafiri mwenzenu tumo kwenye meli hii ya Dunia tuna kwenda kwenye safari hii ya Ulimengu tunazungumza na nyie kwa kile kidogo alichotupa Mwenye enzi Mungu katika elimu zake, na ikifika wakati kila mmoja wetu anateremka na kuachia wengine waendelee na safari hii ya Maisha, Kwa hiyo kazi yangu mimi sio kusomesha (hiyo ni kazi ya Masheikh)kazi yangu mimi ni kukumbusha kile ulicho sahau, Naam sasa twendeni kwenye swali lenu lenye kuhusu hiyo aya mloitaja, Ama kuhusu kuendelea kwenu na maasi na machafu wakati mnasali inakushangazeni wakati (Quraan) imetoa Ahadi hilo nishalizungumza kwenye makala ya (Dawa ya Dhanbi)Lakini leo ntatoa tena ufafanuzi ili niongeze (Dozi)ya hilo swali ili mtibu maradhi mlonayo.Katika darsa hii wacha nikukumbushe kitu, katika harakati zote hizo lazima upate taa ya Mwenye enzi Mungu kwa njia ya Neno au ufahamu ndio utaweza kutekeleza kwa ukamilifu agizo la utiifu kwa Mwenye enzi Mungu, kwanini nikasema hivyo? Kwa sababu bila ya kupata taa uongofu huo itakua Taa inawaka lakini wewe (Still) Huoni bado upo kwenye kiza. Nikisema (TAA)(Light)Nina maana gani?, Maana yangu kuwa Uislam ndio dini pekee iloanza na Neno Soma, kwa hiyo Dini inakutaka usome kwanza ili upate kufahamu, ukisha kufahamu ndio matendo yako yote yatakua na mafanikio, sio ufate tu ukiambiwa, kwa hiyo ukisoma utapata kujua vipi Neno lina nguvu ya kubadilisha mwenendo wa mtu, Hapa wacha niwape kisa ili kukuonesheni nguvu ya neno linavopasua moyo na ujumbe kufika kwenye roho na ukaacha maasi na machafu mara moja, Lakini kwanza ifahamike Mwenye enzi Mungu hakubadilishi mpaka utake Mwenyewe kubadilika, kama anavosema kwenye sura ya (RAD aya ya 11), kwanza napenda ieleweke kuacha kuna aina mbili aina ya mwanzo unaacha hapo hapo, ukipata (Single spike)Ya neno likapenya kwenye Roho yako sio kwenye Akili basi unabadilika daima, na aina ya pili unaacha kidogo kidogo mpaka unatambua haya mambo hayana faida kwangu wala hayanipi furaha ila kunipa matatizo sasa na baadae. Sasa nifanye nini,? wacha tukisikilize kisa cha Tajiri Mmoja aliyeishi Iraq akawa na yeye mtenda maasi kama wewe na huku Ana sali Anafanya ibada lakini anaendelea na Maasi.kisome au kisikilize kisa hiki kwa mazingatio makubwa inaweza kuwa na wewe ni sababu yako ya kuacha maasi na ukaendelea na Ibada. Alikua tajiri huyu Akiishi kwenye nchi ya (Iraq) Na ikawa kawaida yake akialika watu kwenye (Party)zake wao wakiziita (Samra, au Raksa) au (Sumsumia)ila kwa lugha yenu ya sasa wacha tuite (Kizaizai). 1
No comments:
Post a Comment