Aslm Alekum, Kama nilivosema huo ni muongozo wa mwanzo sasa wacha tuingie kwenye muongozo wa pili pia tunabebwa na (aya ya 78 Sura ya israa)" simamisha Sala linapopinduka jua mpaka unapoingia usiku na Quraan wakati wa alfajir imekua yenye kushudiwa" Naam wamefasir kwa ukamilifu kuhusu kusimamisha sala na wakasema inashuhudiwa na Malaika, sasa sisi tuendelee zaidi tuchambue nini neno (Shahada)?Kwanini ikatajwa Shahada, na Kwanini ikazingatiwa Alfajir? Kwanza kabisa wacha tujue Shahada yenyewe ikoje,? Shahada iliyo kusudiwa hapo ni ile Shahada ya mwanzo ,napenda uelewe Shahada ina nguzo saba kikamilifu(Katika hizo 4 ndio kubwa) Lakini zote zinategemeana na katika hilo La shahada umelibeba wewe Mwanaadamu kutokana na kuwezeshwa na Mollah wako, Amma nguzo ya Mwanzo ya Shahada ni kusikia (Ndio maana utaona mwanzo inatajwa Samia 1) ikisha inafatia (Basira 2)Kuona, halafu tena inakuja Uwepo(Present au moment of Now 3)Na baadae inafatiwa na Kumbukumbu(history 4)nguzo ya tano (Experience 5)Nguzo ya sita ni elimu(Knowledge)au ita kujua na ya saba ni hiyo (Silent)Ukizipitia hizo zote hapo ndio utajikuta wewe mwenyewe jiite utakavo (Roho) Au (Human being) hizo ndio (Level) za Shahadat ambazo mja unatakiwa kuzitambua unaposema neno Shahidi, ujue umekusudia nini ama una shuhudia nini?, Sasa kwanini ikatajwa nyakati za Alfajir?. Tukitaka kulijua hilo tukihudhurie kwanza kisa kilichomo kwenye (Quraan) Kuhusiana na wale (As-Habul-Kahf)Kuhusiana na Kadhia ya kusikia ili tupate kujua kwani kusikia kuna faida gani, Mollah wako ?Alifanya nini, (Quraan aya ya 11 sura ya Al-Kahfi) "Tukaziba masikio yao (Wakalala hawasikii chochote) Katika pango hilo kwa idadi ya miaka mingi. Wameondoshewa uwezo wa kusikia ili wapate kulala, hata wewe unafanyiwa kitendo hicho kila usiku ukenda kulala, bila kuondoshewa uwezo huo utakua hulali kabisa, kumbuka huna uwezo wewe wa kuzuia usisikie, ( Natural)Huwezi kufanya usisikie, ukiziba masikio (Still) Utasikia sauti Nyengine ambayo pia ita ku (Disturb)Utaipa jina (Tinnitus), sasa baada ya kujua hayo Sayansi inasemaje katika hili, Wanasema wanasayansi Kusikia ni kitu cha Mwisho Mwanaadamu anapolala kuondoka, Kwa Sababu kusikia ndio chanzo kinachoiweka Akili (Active)Ukiondoshewa Uwezo wa kusikia Akili inajizima (Data)Na kuanza (Kudelete)Mambo ya mchana kutwa. Na ikiwa haijazimika inabakia (Alert) utaona kelele kidogo umeshituka, Wagonjwa walio kwenye (Coma) Wanapata kusikia ndio maana (Akili)zao zikitizamwa zinafanya kazi, kwa sababu ya sauti, wakaendelea kusema Wachunguzi wa Sayansi ya usingizi sauti zinakuzuia kupata (Deep sleep)Mwanaadamu katengenezewa (System)Maalum itwayo (The Reticular Activating System) Hii (RAS) ndio inayokuweka (Awake,conscious, Aware) Na sikio ndio Sehemu yenye nguvu ya kupitisha sauti za kila aina, hiyo (RAS System) inapofungwa au kufunikwa ndio Mwanaadamu anapata (Deep unconscious sleep) Akili haipat (Sensory disturbance) ndio inapoingia kwenye (Minimal activity ) hapo ndio unapata nafasi ya kufuta yale yote yasokua muhimu na mengine kuyaweka kwenye (Memory) Ukiamka usha (Deleted) Unakuwa mweupe hukumbuki mengi yalopita jana. Sasa nini kinatokea unaporudishiwa uwezo wa kusikia, Jambo la mwanzo linalo rudi ni kusikia, ila wewe kwakua huko (Aware) unadhani ni kufungua macho, Lakini ukichunguza utakuta jambo la mwanzo ni kusikia kama ulivokuja duniani wakati wakuzaliwa, (Umo kwenye darsa ya simulizi ya kusikia katika fani ya Shahada zingatia sana Miujiza ya Mollah wako ikisha useme Ametukuka mbora wa Uumbaji) Naam Sasa kumbuka ikiwa ulipokuja kwenye Ulimwengu kwa mara ya Mwanzo ni kusikia basi elewa na jambo la mwisho pia itakua kusikia itakua sauti (Kwa hiyo kuweni na tahadhari mkiwa kwa wagonjwa mahtuti wanokaribia kufa kumbukeni wanasikia mnayoyasema yote), Sasa kwanini ikatajwa (Quraan) Wakati wa Alfajir ni kwa sababu kinachoingia na kusikiwa Mwanzo ndio kina kua (Pure) kina kaa kwa muda mrefu kina kuwa Na (Direct communication) Na Roho yako, hapo kinakupa (Deep Meaning) Ufasaha wa wazi , sasa ikiwa tabia yako kusoma, kusikiliza, Quraan nyakati za Alfajir wakati una Sali au baada ya sala ndio nyakati hizo za Alfajir unapata hiyo (Hudan lin-nasi)Muongozo kutoka kwa Mollah wako(Al-Baqarah 120) Ukiufata sawa sawa muongozo huo ndio itakua taa yako (Torch) ya kukumurikia njia kwenye huu msitu wa dunia ulojaa maasi, hapo ndio unapata (clear Picture) Wewe usitende Dhanbi, usile rushwa, usidhulumu, Usizini, unapata ufafanuzi wa mambo hayo kama ulivopata ufafanuzi wa hii kadhia ya kusikia na mahusiano ya Quraan Alfajir, kila kitu kinafunguliwa kwako kunakua kweupe, na pia utapata maelekezo ya mambo mema mchana kutwa ikiwa umeyashika sawasawa mafunzo ulopitia Alfajir yenye Uongofu kutoka kwa Mollah wako, Maisha yako yatabadilika ikiwa Quraan itajaa kwenye moyo wako ikiambatana na tafsiri yake , itakupa uwezo wa kuacha Maasi na kuipata Sala yako sawa sawa bila ya upungufu, utaacha maasi na Sala zako zitakamilika bila ya wewe kuyarejea maasi, hii ndio ngao ya pili, kumbuka ya Mwanzo kutumia jina La Mollah wako kwa ukumbusho na hii ya pili kukisoma kitabu chake kama Muongozo. Mollah wangu anajua zaidi. 4
No comments:
Post a Comment