Sunday, April 27, 2014

FAIDA YA SALA ZA USIKU PART 4

Asalaam Aleiykum

Najua utasema huyu anasema nini hali yakua mimi niko macho, Nakwambia wewe huko macho, ila hayo macho yako wazi wewe mwenyewe unaendelea na ndoto unazipanga hizi za mchana na hizi za usiku na zote ukitaka unaweza kuziona, lakini za usiku unaziona uzuri sababu umetulia. Na mchana unaendelea kuona ndoto zako, mara umejenga nyumba, pengine unaota mpaka ushatajirika au uko (Beach una Enjoy)au unamuota mwanamke au mwanamme huku umetulia na ukishtuka duh kumbe hizi ndoto unakurupuka usingizini na kuona huu ni ujinga, unajibabaisha kidogo ikisha huyoo unaendelea na ndoto nyengine na hiyo ndio hali ya kila saa na dakika zetu tulizojaaliwa.
Na usiku ni hivyo hivyo ila umekua hodari wa lugha usiku unaziita ndoto na mchana unaita fikira ni kitu kimoja kama utakichunguza kwa makini, Lakini kutokana na uweza wako wa kushuhudia hayo yote ya usiku na mchana lazima ipatikane hali nyengine ambayo inaitwa (Awakening State) Hali hiyo ndio inayopatikana kutokana na hizo Ibada za usiku.
Nini(Awakening)? Ni hali ya kuwa macho wakati wote na watu hao wametajwa katika sura ya (Al-Imran aya ya 191)"(Ambao humkumbuka Mollah wao wakiwa wima wamesimama, na wakikaa na hata wakilala)"Hali hiyo inatokea kwenye (Mind)ndio ukaambiwa hali hiyo inawafikiana sana na Moyo, kwa hiyo kwenye (Mind)Akili inatokezea (Awakening)Muamko na kwenye Moyo ndio inatokezea hiyo (Laylatul Qadir) kwa hiyo maana ya kuwafikiana sasa unakua tayari ushafanya mataarisho ya kujiandaa na hiyo (Laylatul Qadir) Akili ushaiweza sasa huna nafasi tena ya kutenda dhanmbi, kwani sasa uko macho, na Shetani hapati nafasi ya kukushawishi na kukulaza.
Sababu kubwa Shetani anayoweza kukufitini na Mollah wako shuruti lake lazima uwe umesahau au umelala, ndio anakuletea firimbi na wewe unatoka kama nyoka wa kihindi kwenye kikapu, hapo unavamia chochote, unaletewa nyimbo, au ngoma au senema au watu wanatembea uchi, anakupa mambo chungu nzima ili upate kukoroma, na ukikoroma umekwisha, unatenda kila maasi, lakini ukiwa macho mwizi hawezi kuja kukuibia mema yako, na afanyacho Shetani hataki jambo moja tu la wewe kuwa karibu na Mollah wako, ndio maana utaona ukisali siku mbili ushachoka au unasubiri mpaka Ramadhani ije.
Unaendelea kuambiwa Nyakati hizi za usiku "Maneno yake yanatulia kwenye moyo"yanateremka vizuri, unajua kwa sababu gani (Ndio maana unaambiwa ulale kidogo)sababu ukiamka unakua (Empty Mind) kwa muda ule hakuna mawazo, umeamka ghafla ndoto zimesita, na mfano mzuri hivi sasa pengine umekuja na tafsiri za (Sheikh)wako huwezi kukubaliana na mimi mpaka uje bila ya Tafsiri, au utakua unasoma maneno yangu lakini anatafsiri (Sheikh) wako kichwani(Amka)hata niseme nini huwezi kukubaliana na mimi moyo wako hauafikiani na maneno yangu mpaka uipate hiyo (Awakening) kwa hiyo ukija na (Mind iko full) unakua umo hasarani.Aya inayofatia inasemaje kuhusiana na kuja kwako na mizigo kichwani. "إِنَّ لَكَ فِى ٱلنَّہَارِ سَبۡحً۬ا طَوِيلاً۬ "Hakika mchana una shughuli nyingi"
Vipi utapata Muamko(Awakening)kwenye jiji kama la Daressalaam haiwezekani kabisa au uwe umedumu kwenye Ibada hizi za usiku kwa muda mrefu, kwa sababu shughuli zake nyingi, kelele ndio usiseme, nyimbo ndani ya vilabu vya pombe mpaka asubuhi, biashara honi za magari, kelele za binaadamu zinakuzuilia kupata (Awakening)Muamko kabisa, akili haiwezi kutulia.
Namalizia darsa ya leo kwa hii aya ya 8 sura ya Muzammil
"وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلۡ إِلَيۡهِ تَبۡتِيلاً۬ "
Na litaje jina la Mollah wako na ujitupe kwake kwa kweli(Mapenzi)
kwanini ikawa ulitaje jina la Mollah wako, kwa sababu unaweza kushikwa na usingizi ukalala tena kwa kuwa umekaa macho na huna la kufanya, (Kwani hujawahi kumuona mtu kalala chini ya Speaker na Muziki unaendelea na yeye anakoroma)sasa na wewe unaogopewa ndio unaambiwa litaje jina la Mollah na ujitupe kwake kwa mapenzi ya kutaka kumjua, mapenzi ya kutaka uwe karibu naye, na katika hayo majina kuna siri kubwa.
Na ukimtaja kwa ukweli mara nyingi unakua muda wote unamkumbuka na ukimkumbuka sana unakua katika waja waliyo karibu yake, Na waja wote walo karibu na Mwenye enzi Mungu wanaipata Nuru yake, Na nuru ya Mwenye Enzi Mungu ikikuwakia ukaanza kungara watu wataanza kukupenda na kukuogopa, sio kukuogopa na kukuchukia, huo uadui, hayo maradhi, lakini kuogopewa na kupendwa mfano vile wa watoto wako wanakuogopa na kukupenda, na kama sisi tunavyo muogopa Mollah wetu na kumpenda, hiyo ndio kheri, hiyo ndio neema itokayo kwa Mollah wako, na huko ni kufanikiwa kukubwa katika upeo wa kibinaadamu, ama kwa upeo wa upande wa Mollah wako utaujua mwenyewe utakapoipata hiyo (Awakening)vipi anavokufungulia zawadi zake zisizokua na Mwisho kwa ajili ya kisimamo chako cha usiku.
Nakuomba Mollah wetu tuwezeshe kuifanya na kudumu katika Ibada hii ya Usiku ili utupe fadhila zake na Rehma zako. Amin

No comments:

Post a Comment