Sunday, April 6, 2014

NGAZI SABA ZA ROHO PART 2 (NGAZI 7)

Asalaam Aleiykum,

Kwa hiyo huwezi kuita umezaliwa tena, alozaliwa tena anakua yule yule, ndio maana Shetani (devil) rahisi kumuingia tena, ana uwezo wa kumtawala, lakini ukitoweka na kurejea unakuja na mambo mapya huku ukiwa unazijua mbinu za kale za shetani. Na hivyo ndivyo inavotokea kwa Wacha Mungu wengi walofanikiwa kupanda na kuchungulia katika ngazi hii, waliporejea  ndio baadhi yao wakahadithia  waloyaona huko mfano kama Bibi Rabbiya bin Adwiyya, Jalaludin Rumi, Mansour Bin Khalaj, kina Ibn Arabi na wengi wengineo, Na kila mmoja kahadithia kwa njia yake ili na wewe uweze kupata hamu na shauku ya kupanda ngazi hii ya saba.
Nini Walichokutana nacho?
Jambo la Mwanzo wanakutana na Nuru ya Mwenye Enzi Mungu, hivi ndivo Wacha Mungu wote wasemavyo kiwatokeacho katika ngazi hii, sio kuwa wamekutana na Mwenye enzi Mungu kwani jambo hilo haliwezekani, na wala halitotokea, unaweza kuhisi lakini sio kumjua au kumuona(Never)kwani Mollah wako (Si kitu kinachoweza kujulikana. Kwa hiyo Roho inachopata kuona ni hiyo Nuru.
ٱللَّهُ نُورُ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ‌ۚ مَثَلُ نُورِهِۦ كَمِشۡكَوٰةٍ۬ فِيہَا مِصۡبَاحٌ‌ۖ ٱلۡمِصۡبَاحُ فِى زُجَاجَةٍ‌ۖ ٱلزُّجَاجَةُ كَأَنَّہَا كَوۡكَبٌ۬ دُرِّىٌّ۬ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ۬ مُّبَـٰرَڪَةٍ۬ زَيۡتُونَةٍ۬ لَّا شَرۡقِيَّةٍ۬ وَلَا غَرۡبِيَّةٍ۬ يَكَادُ زَيۡتُہَا يُضِىٓءُ وَلَوۡ لَمۡ تَمۡسَسۡهُ نَارٌ۬‌ۚ نُّورٌ عَلَىٰ نُورٍ۬‌ۗ يَہۡدِى ٱللَّهُ لِنُورِهِۦ مَن يَشَآءُ‌ۚ وَيَضۡرِبُ ٱللَّهُ ٱلۡأَمۡثَـٰلَ لِلنَّاسِ‌ۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَىۡءٍ عَلِيم 
Mwenye Enzi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi, Mfano wa Nuru yake, ni kama Shubaka ndani yake Taa, (Imo)katika Tungi(Kama Chemni)tungi (hilo ni)kama nyota ingarayo, inayowashwa(Taa hiyo kwa mafuta yatokeayo)katika mti ulobarikiwa wa mzeituni, usio wa (Upande)wa Mashariki wala wa Magharibi, Yanakaribia mafuta yake kungaa (wenyewe)ingawa moto haujayagusa, Nuru juu ya Nuru Mwenye Enzi Mungu humuongoza katika Nuru yake amtakaye, Na Mwenye enzi Mungu hupiga mifano kwa watu, Na Mwenye enzi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.
Mambo mengi yanataka kuzungumzwa katika aya hii lakini leo si siku yake, Inshaa Allah siku za usoni penye uhai tutaizungumza aya hii kwa undani zaidi ila leo ni kuonesha nini hicho wanachokutana nacho wale wanofikia ngazi hii ya saba, hicho ndio wanachokikuta cha mwanzo kabla ya kitu chochote kile.
Na mwanzo kabisa Nuru hii inavokumurika unaingiwa na khofu kubwa kabisa mpaka unapoteza fahamu, unaweza kushikwa na homa hata kuishinda ya (Malaria), Na inaweza kuchukua tukio hili ukawamo katika hali hiyo kwa masiku au siku kutokana na kupanda kwako katika ngazi hii. Hofu ikimalizika ukakaa sawa ndio kidogo kidogo unarejea katika hali ya kawaida lakini sasa ukiwa Mtu mwengine kabisa, Na hivyo ndivyo inavotokezea kadhia hii katika ngazi hii ya Saba kwa kila apandae, Na kizuri zaidi kinachotokezea ukiteremka lazima upewe zawadi kama vile (Mfano) wa Imam Ghazzali aliposhuka kutoka ngazi ya Saba akatuletea zawadi ya kitabu chake maarufu (Uhiyya Ullumu Diin) basi na wewe fanya jitihada upande ili upate kutuletea zawadi yako.
Endelea part 3 

No comments:

Post a Comment