Sunday, April 6, 2014

NGAZI SABA ZA ROHO PART 3 (NGAZI 7)

Asalaam Aleiykum,

Sasa na wewe pia unaweza kuipata hiyo Nuru hapa hapa chini lakini iliyo (Hafifu) ikiwa utafanya Ibadah kwa muda wa miezi mitatu mfululizo na bila ya kufanya makosa makubwa, utaanza kutoa Nuru fulani ambayo watakua wanahisi lakini hawajui kitu gani, mtu akikaa na wewe tu atakua anasikia furaha kwa ajili ya hiyo (Energy)inayotoka katika mwili wako.
Naam katika ngazi hii baada ya hiyo Nuru ndipo unakuja kuona vipi Dunia mbili zinavokutana ile Dunia ya (Spirit)na Dunia ya (Matter), Nuru hiyo inakusaidia kuona mambo yalivyo kwa uwazi kabisa, kwa mara ya mwanzo unajua alaa kumbe haya ndio yalosemwa kwenye aya ya mwanzo sura ya (Nisaa)mpaka mwisho wa aya.
يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِى خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٍ۬ وَٲحِدَةٍ۬ وَخَلَقَ مِنۡہَا زَوۡجَهَا وَبَثَّ مِنۡہُمَا رِجَالاً۬ كَثِيرً۬ا وَنِسَآءً۬‌ۚ 
Enyi Watu Mcheni Mwenye Enzi Mungu  wenu ambaye amekuumbeni katika Nafsi moja, akamuumba mkewe katika nafsi ile ile na akaeneza wanaume wengi na wanawake(Mpaka mwisho wa aya).
Unapata kuona kumbe kilichomo kwenye Nafsi yangu ndio hicho hicho kilichomo kwa Mke wangu, au wanangu au majirani au hata mpita njia, hapa ndio unagundua lile Daraja la mmoja kwa wengi na wengi kurejea kuwa mmoja (Nafsi Wahida), na ukiyajua hayo kama wewe Shujaa wa kweli unachupa, na huko uchupapo hakuna (Gurantee)unaweza kurudi Akili imeharibika, unaweza kurudi ukakaa kimya mpaka kufa kwako.
Kumbuka Nasema ukirejea kutoka Ngazi ya saba unakua mtu mwengine kabisa kutokana na mabadiliko ya matendo yako, kama tuonavo mfano huu ulomtokea "Ibn Arabi" siku moja alikuja maskini kuomba ikawa Ibn Arabi hana cha kumpa basi akatoa Nyumba yake,(Unajua kwanini?)(kwa sababu ukipanda huko unatambua kuwa haya mambo yote ya Ulimwengu ni Temproray, hayadumu kwa hiyo unakua huna shughuli nayo) Sasa wewe huko tayari hata kutoa chakula hivyo kweli utafika ngazi ya Saba. Alisimama siku moja Ibn Arabi msikitini  akanadi kwa kupiga makelele na  kuwaambia waliyomo msikitini enyi mliyomo ndani "Mollah mnaye muabudu yupo chini ya miguu yangu"wakatoka watu ndani wakampiga vibaya sana kwa hasira, lakini kwa kuwa wanajua Ibn Arabi katokea ngazi ya Saba wakaona bora wachunguze kwanini kasema vile na yeye ni mtu wa Mungu, na hivi ndivyo walivyo wanasiasa misikitini na wafanya biashara wanasubiri tu wapate (Chance) ya kufanya (Bussiness) au kudhulumu watu haki zao, "kweli walipochimba ile sehemu wakakuta Dhahabu nyingi"wakagundua nini alikua anakusudia Ibn Arabi.
Na hivyo ndivyo tufanyavyo Misikitini mtu anaomba mpaka mechi ya mpira timu ishinde, au uchaguzi wa diwani eti ashinde yeye, tumegeuza misikiti sehemu ya biashara na siasa hakuna ibadah tena, na naogopa kama kuna mtu atakua anarekodi mawazo yetu wengi tutakua hatuna (Stara)wakati wa Sijjida zetu, itakua aibu tupu.
Naam: (Ahmad Ibn Hanbal) Anahadithia hadith ya Bwana Mtume s.a.w "Kasema"Hakika Mwenye enzi Mungu Kaumba Ulimwengu kwa kutumia Kiza,(Na sasa Inajulika kama Dark Matter)Ikisha akaumurika kwa Nuru yake, Na yoyote yule Mwenye kumurikwa na Nuru hiyo basi atapata baraka za kuongozwa kwenye njia iliyonyooka, Na yoyote yule ambaye Nuru hii haitompata basi huyo ndio alopotea".
Basi namie nakuomba panda ngazi hizi saba ili upate kufanikiwa na uzipate hizo Baraka za Mollah wako.
Mimi sitoendelea sana kuhadithia mambo ya ngazi ya saba,kuna mengi mno mpaka ya kuonana na Majini na Malaika lakini nafata wasia wa Bwana Mtume s.a.w katika hadith ilo hadithiwa na (Bukhari)"Kasema Bwana Mtume s.a.w" "Usizungumze sana mwishoe utasema uongo"Yafanye mawaidha yako mafupi"ili uwafanyie watu wepesi na sio uwatie dhiki""Na wape habari njema""Na wala usiwape vitisho vya Adhabu".
Na mimi nakutakieni kheri na kufahamu niliyoyaandika.Mollah atupe Fahamu ya kuyajua mambo mengi yaliyomo kwenye Ufalme wake. Ikisha aturuzuku msamaha kwa Radhi zake. Amin

No comments:

Post a Comment