Sunday, April 27, 2014

FAIDA YA SALA ZA USIKU PART 1

Asalaam Aleiykum

Tuna anza tena darsa zetu kama kawaida baada ya kusita kama jumapili mbili hivi ili tupate kusoma yalotangulia, tutaendelea na kawaida yetu ya darsa mpya Inshaa Allah kila Jumapili ikiwa Mwenyewe mwenye kutupa hekima na afya kwa uweza wake ataturidhia kwa mapenzi yake ambayo yanaendelea kumiminika juu yetu kila siku. Katika Darsa hii ya faida ya Sala za usiku dhumuni langu ni kujulisha kitu fulani ikiwa unaweza kukipata utakua umeshafuzu katika Ulimwengu huu, Nataka kujulisha kwanini hassa ikawa Sala ya usiku, lakini ntafanya hivyo kwa njia nyengine kabisa, ntakupa faida ya ndani yenye umuhimu na uhai wako katika Ulimwengu huu.
Kuna msemo wa kiswahili unasema (Jipendekeze Upendwe), 
Nini Maana ya Kujipendekeza?
Watu wengi wakiulizwa huwa wanajibu kujipendekeza ni mwenendo wa ima kujionesha unapenda au kufanya matendo ya kukupelekea uonekane mtu mzuri ili upate kupendwa, hizo ndio Fahamu za kawaida yetu ya kila siku. Lakini kuna Fahamu nyengine ya Wacha Mungu ambayo inajulikana kama kujipendekeza ni mwenendo wa kukumbusha au kujikumbusha usisahau au usisahaulike kwa mpenzi wako.
Na kwa hili la mapenzi hakuna mpenzi mkubwa aliye karibu na wewe kama Mollah wako, Yeye ndiye ambaye anakukumbuka kila sekunde na dakika katika Uhai wako wote, Hakusahau Mollah wako ukiwa kwenye Maasi au kwenye kutenda Mema daima yupo na wewe ana kukumbuka kiumbe chake. Tunaona mapenzi yetu ya kawaida vipi tunavo sahau, mpende mtu upendavo lakini , ukenda senema umemsahau, ukicheza karata umemsahau, ukenda harusini umemsahau, ukenda mpirani umemsahau na mwisho utashikwa usingizi utalala kwa masaa burdani hukumbuki chochote na ukiamka huombi hata msamaha na mapenzi yanaendelea kama kawaida, sasa baada ya kujulika udhaifu wako huo na kuonekana kama utaachiwa hivi hivi Mwanaadamu utaingia kwenye hasara kubwa, sasa ufanye nini? Endelea part 2

No comments:

Post a Comment