Sunday, April 27, 2014

FAIDA YA SALA ZA USIKU PART 2

Asalaam Aleiykum

Na kama ukiachiwa ulale mpaka asubuhi utakua unaendelea  kulala hata ukiwa macho, najua unajiuliza vipi utalala ukiwa macho, Naam hivyo ndio sote tutendavyo, unajiuliza vipi nimeamka halafu bado niwe nimelala, yapo mambo mengi yakuuzungumzia usingizi wako lakini leo mie nataka kulitaja moja kabla ya kuendelea na darsa yetu halafu ndio utajua jee umelala au uko macho.
Wacha nigusie hili moja ili tupate kulijua, kwanza kabisa napenda uelewe kabla ya kutenda maasi yoyote pale unakua Macho, katika kipindi hicho unaweza kutenda jambo la kheri, lakini hudumu sana katika hali hiyo ya kua macho hazifiki hata dakika mbili huyo ushalala, ni muda mchache sana unakua macho wewe fikiri utalijua hilo, au lichunguze utakutana nalo hilo tendo la kuwa macho, Basi unapotaka kutenda maasi lazima uwe umelala huku umesimama vipi inatokea hali hiyo? na kwanini isitokee wakati ukilala si zinakuja ndoto? Na ukiwa macho vilevile ndoto zinakuja tafauti yake huu mchana na ule usiku, vipi inakua.
Unakua umacho saa sita ya mchana pengine umemaliza sala ya (Adhuhuri)upo kwenye baraza ya Msikiti anapita Mtoto wa Kike, Mtoto ndio Mtoto kama mnavovijua vivazi vyao unapiga Jicho hujui kama kavaa (Skati)au hakuvaa, ila ninachokijua mimi mtoto huyo anakuletea usingizi Wallahi umacho unalala huku unakoroma tena unageuka Fundi cherehani na ndoto zinafatia, utaitia zipu hiyo (Sketi)utamtilia vifungo, itakuingia mpaka khofu duh kama itamvuka itakuaje, unawapangia mpaka watu wataona nini, basi hapo unashughulika na ndoto zako mpaka unakuja kuamshwa na Muazzin wa Alasiri (Salaa Salaa)unaingia tena Msikitini na bado unaendelea na ndoto eti lakini ile (Sketi)chini haijapindwa huku unatia Udhu. 
Huo ndio usingizi niloukusudia, na ziko ndoto nyingi tena kila sehemu mwengine kutwa anafunga hesabu, unawadhuru walokukera, Nini kilitokea jana usiku, Fulani ana mpya gani leo, mambo millioni, likimalizika hili linakuja lile almuradi ndoto hazishi kichwani mwako, Na ikiwa wewe huna ndoto yoyote kichwani mwako basi wewe ushafuzu na upo katika kundi jengine kabisa, lakini ikiwa bado usiku unapata ndoto na mchana vile vile unaendelea kuota inabidi nikupe zawadi pengine ukiweza kuidumisha inaweza ndoto zikatoweka au kupungua na ukapata nafasi ya kuamka na kumpwekesha Mollah wako.
Mimi sikupi kitu kipya au ukaona nimevumbua jambo, nifanyacho mimi ni kukupa ufafanuzi wa tafsiri halisi  na wewe una hiyari kufata au kutokufata, kukubali au kukataa ni haki yako.
Ili kuifungua zawadi hii Endelea part 3

No comments:

Post a Comment