Sunday, April 6, 2014

NGAZI SABA ZA ROHO PART 1(NGAZI 7)

Asalaam Aleiykum

Leo tumefikia kilele cha hitimisho la Darsa zetu za Ngazi saba za Roho, Hii leo tupo kileleni mwa hiyo Ngazi, sote tukiwa hatujui nini kitatokea? Mimi msimulizi na wewe msimuliwa darsa hii hatujui kwenye ngazi hii kuna nini, Tunachokifahamu Watu wengi wanaipanda ngazi hii wakati wa Mauti yao, Wachache sana wanofika wakapanda wakiwa hai. Na yule afikae akirudi anakua hana lugha ya kuhadithia mambo yaliyopo kwenye ngazi hii ya Saba.
Wanofanikiwa kuhadithia ni wachache  mno,Na sisi ndio tunapata kutoka kwa hao wachache habari za ngazi ya saba jinsi ilivyo, Unaweza Mwanaadamu ukajikaza ukazipanda mpaka ngazi ya sita lakini ngazi ya saba huna cha kufanya huwezi kupanda kwa uwezo wako, mpaka upewe mualiko, au labda utaraji maneno yaliyomo kwenye aya hii Sura ya Fussilat (35)
وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَمَا يُلَقَّٮٰهَآ إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ۬
"Lakini hawatapewa (Jambo hili) ila wale wanosubiri, wala hawatopewa ila wale wenye hadhi kubwa.(Mbele ya Mwenye enzi Mungu).
Wale wanosubiri kwa kufanya Ibada bila ya kuyumba, Na wale Wacha Mungu walojitupa kwa Mollah wao hao ndio watoifikia Ngazi hii(Soma Uzuri kuanzia aya ya 30 mpaka 35)ndio utajua kusudio la ngazi ya saba. Katika ngazi hii kinachotokea  ni kitu cha ajabu kabisa ikiwa utalifahamu tafsiri ya neno hili (Dis-Appear)maana yake unatoweka halafu unarejea, lakini marejeo yako ya pili sio ya kawaida, hurejei yule yule wa mwanzo, (Wenzetu Wakiristo wameita marejeo haya (Born Again) sio hivyo, uhakika ni kuwa umetoweka ikisha ukarejea, lakini marejeo haya unapata ladha ile ile kama utakumbuka ya utotoni (Innocent) kila kitu kwako ni (Bliss)kwa hiyo huwezi kuita kuzaliwa tena kwa sababu kuzaliwa (Complete) hujui lakini sasa hivi unajua lakini si kwa kutumia (Brain) ila kwa kutumia Roho yako.
Endelea part 2

No comments:

Post a Comment