Asalaam Aleiykum
Umeshawahi kujiuliza urafiki wako na huyo mwenzio ulianza vipi? Jee mahusiano yenu yana mapenzi au makubaliano?Na kwanini Jambo dogo tu linavunja urafiki huo, ukiangalia kwa makini mahusiano hayo ya Urafiki wenu yamekamatana na makubaliano ya hiyari, ndani ya hiyo hiyari imejificha chembe ya mapenzi, kwenye hiyari kuna mbegu na kama mbegu hiyo itachanua Urafiki wenu unakua wa kufa na kuzikana, Mnakua kama ndugu wa tumbo moja, huo ni urafiki wa Binaadamu kwa Binaadamu, Mimi leo nataka kukujulisha vipi unapatikana Urafiki baina ya Mwanaadamu na Sala na nini kinatokezea Urafiki huo unapokuwa wa kweli, Wapi Rafiki yako Sala anakupeleka.
Sala ni sehemu maalum unayoingia na kutoka kwa njia ya Siri na Dhahiri, Dhahiri ni Msikitini au Nyumbani watu wote wanakushuhudia, halafu unaingia kwenye siri ambapo moyoni mwako wewe pekee na Mollah wako mnakutana katika njia zako maombi, Na katika hiyo siri wewe hukai moja kwa moja, mara umehamia kwenye akili na akili inakupeleka inapojua yenyewe, ndio maana unaingia msikitini lakini unajikuta upo senema, au upo dukani au unafunga hesabu na kuamua mambo haya na yale, Unatoka kabisa katika sehemu takatifu uliyosimama, sehemu ya unyenyekevu uloingia ukawa huna kusudio lolote ila ni kusali kwa kumuomba na kumsabahi Mollah wako.
Sasa nini kitakujulisha kuwa ushaanza kuipata Sala? Vipi utajua ushaanza kuwa wewe na Sala ni marafiki? Jambo la Mwanzo kabisa Rafiki wako huyu anakukinga na (Machafu na Maovu)
(إِنَّ ٱلصَّلَوٰةَ تَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِۗ)
Na moja kwa moja ukiepushwa na mambo hayo Sala inakupeleka kwenye Jambo la pili ambalo kubadilishwa au kugeuzwa khofu yako kuwa mapenzi, maisha yako yote yanabadilika kwa Jambo la kuipata Sala, Na jambo la tatu unakua huondoki tena kwenye hiyo sala na kwenda kutalii. Hapo tena Sala inakuondoshea khofu ya kufa, khofu ya Akhera unakua tayari kukutana na Mollah wako Mpenzi, wakati wote wa Sala na hata kurejea huko Akhera.
Lakini huwezi kuyapata hayo mpaka ufanye mazoea ya hiyo Sala, mpaka umuombe urafiki hicho kitendo kiitwacho Sala, mpaka mzoeane ndio utakua mwenye kusimamisha Sala, vipi unafanya mazoea haya, ni lazima kwanza uishinde Akili, halafu? .endelea part 2
No comments:
Post a Comment