Asalaam Aleiykum
Wanaadamu kuna hazina imetupotea siku nyingi, kuna wengine wanaijua na kuitafuta, kuna wengine wako mbioni kujitaarisha kuitafuta hazina hii, Na kuna wengine hawajui kabisa kama ipo hazina hii na ni haki yao kuitafuta, Na wako walo bahatika wachache sana wameipata hazina hii na hivi sasa wanaishi nayo wakiwa furahani katika pepo ya Dunia.
Ama kwa wale wote ambao hawajaigundua hazina hii itabidi niwachukue ili nipate kuwakumbusha njia ya kwenda ukafikia kwenye Hazina hiyo ya Ufalme wako, Wewe ni Mfalme lakini kwa sasa bado hujielewi, bado hujakumbuka japo Mollah wako anakukumbusha sana, anakwambia "Ewe Mwanaadamu" Wewe kwenye Ulimwengu huu Wewe (Khalifa) lakini unaendelea kuishi katika Umasikini, unaendelea kuishi kwenye mateso, unaendelea kuishi umo kupita kuomba hichi na kile, lini yatakwisha madhila na mateso haya.
Yatakwisha pale utakapo kumbuka kumbe hazina ipo chini ya miguu yangu, hazina imefukiwa chini ya (Ukuta) na ukifukua tu wewe ushakua (Mfalme)Tafauti yake ni kukumbuka kwa kitendo kumbe mimi (Mtawala). Sasa vipi inatokea hali hii ya kukumbuka? hali hii inatokea kwa wewe Mwenyewe kufanya kazi au kuwa karibu na watu wanofahamu, watu walokua tayari washakumbuka Ufalme huo, hao watasaidia kukumbusha kama nifanyavo mimi sasa hivi, venginevyo utaendelea kuishi kama Mtumwa hali yakua wewe ni Mfalme.
Nikitaja Ufalme tafsiri zako moja kwa moja zinakupeleka kwenye Utajiri, zinakupeleka kwenye kulimbikiza mali, hicho ndio kigezo chako ulichonacho, kwanini ikawa hivyo sababu maisha yako yote unaishi kwa vigezo vya nje, Fulani ana hichi na kile, Fulani ana Majumba makubwa ya ghorofa, Fulani ana watoto wengi, lakini hata siku moja hujapata kujiuliza hivyo Fulani ana Ufalme katika nafsi yake, anaishi Furahani na vyote alonavyo, keshajigundua yeye ni Mfalme, anaipata (Bliss)kutoka kwa Mollah wake, keshawahi ku(Test) kitu kilicho (Beyond) Furaha, vigezo hivyo huna, vigezo ulivyo navyo ni Fulani (Handsome) na Yule ana (Figure)nzuri, akitembea anapendeza umeshughulika na uonavyo nje nini habari ya Ndani kwako?.
Endelea part 2
No comments:
Post a Comment