Sunday, September 28, 2014

SALA YA TOBA PART 3

Asalaam Aleiykum

Sasa kwa sie tusoyaweza Kutii moja kwa moja ndio tunapewa hii Sala ya Toba. Kutokana na hali ya makosa wakati wote viumbe tunakua tumejaza wingu hili la makosa katika nafsi zetu, kiza totoro kimetufunika Mja hapo na pale huoni, daima unakua (Guilty)huna furaha, hujui wapi unakwenda nini kitatokea dhiki tupu kwenye nafsi yako, ili kuondosha uzito huo na kuisafisha nafsi yako umepewa Sala hii ya Toba kwa kuambiwa hivi katika sura ya (Imran aya ya 135)
وَٱلَّذِينَ إِذَا فَعَلُواْ فَـٰحِشَةً أَوۡ ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَہُمۡ ذَكَرُواْ ٱللَّهَ فَٱسۡتَغۡفَرُواْ لِذُنُوبِهِمۡ وَمَن يَغۡفِرُ ٱلذُّنُوبَ إِلَّا ٱللَّهُ وَلَمۡ يُصِرُّواْ عَلَىٰ مَا فَعَلُواْ وَهُمۡ يَعۡلَمُون
Na ambao wanapofanya uchafu(Mambo ya Zinaa)au kudhulumu nafsi zao humkumbuka Mwenye enzi Mungu na kuomba msamaha kwa Dhanmbi zao, Na nani anayeghufiria Dhanmbi isipokua Mwenye enzi Mungu, Na hawaendelei na(Maovu)waliyoyafanya hali wanajua(Kwamba haya ni Maovu).
Hakuna kitu chenye nguvu kinacho mshinda mwanaadamu kama hii (Ngono)jambo la (Sex) ndio maana hapo ikatajwa mwanzo, kwa sababu ikishaingia Akilini vigumu kutoka mpaka uzeeni mate yanakudondoka, hujiwezi, vipi utajiweza na nguvu amabazo ukizitumia kihalali zina mtengeneza kiumbe, sasa nini habari yetu tunaitumia kwa njia ya haramu? lazima itutengenezee Moto au adhabu zozote tulizoandaliwa.
Au ukidhulumu nafsi yako, vipi unaidhulumu nafsi yako kwa kutenda madhanbi na kila ukitenda dhanmbi ina maana unajitengenezea njia ya adhabu, kwa maana hiyo unaidhulumu nafsi yako mwenyewe, unautaarisha huo mwili ulokubeba kwenda kuungua kwenye moto wa Jahannam.
Sasa ufanye nini kila ukikumbuka, na hakuna kukumbuka kama kusali, kwani Sala ina kitu gani, Sala kama utaikumbuka basi inakupa (Awareness) ya kukumbuka jambo lengine kabisa la Ufalme wa Mollah wako, Sala ni (Light) kila wakati ukikumbuka Sala ina maana unawasha taa kwa kuzima giza la Akili, Jitahidi sana katika hiyo Sala usianze safari za huku na kule ikawa Sala nzima wewe umelala unakuja kuamka kwenye Salaam, Sasa kila ukikumbuka Simamisha Sala hii ya Toba na uombe (Maghfira)usichoke japo unajikwaa na kuanguka tena, hapa umetajwa wewe kwa kufanya hayo machafu na kudhulumu nafsi yako, endelea kuomba toba jizoeshe kuisali sala hii mpaka utafikia pahala taa hii ya Sala ya Toba itawaka moja kwa moja na haitozimika tena, hapo ndio utaijua tafauti ya kosa kwa undani, lakini sasa hivi unaendelea kuwa shujaa, unatubu unasahau unarejea tena, lakini utakapo pata fahamu ndani ya moyo wako na sala hii ya toba ikaingia ndani ya huo moyo hapo tena utasita wewe mwenyewe kufanya hayo makosa, mimi sikwambii kuwa ukisali mara moja ushasamehewa au ndio utaacha kabisa au kusita, ninacho kuhimiza mimi isali Sala hii kila unapohisi umetenda kosa au bila ya kutenda kosa fanya iwe ndio mazoea yako ya kuomba Toba kwa njia hii ya Sala na mwisho nakupa hakika utajikuta umeshafika kwenye Mji wa Utiifu na mapenzi ya Mollah wako.
Inasaliwa vipi Sala hii?
Anahadithia Abubakar Sadik r.a"Nimemsikia Bwana Mtume s.a.w kasema"Mtu yoyote yule ambaye katenda Dhanmbi ikisha akasimama na kutia Udhu halafu akasali Rakaa mbili na kutubu kwa Mwenye enzi Mungu basi humkuta Mwenye enzi Mungu ni Mwenye kumsamehe".
Hivyo ndivyo inavosaliwa sala ya Toba, yatizame mambo mangapi yanatokezea mpaka ukasimamisha hiyo Sala, kwanza unakumbuka, ikisha unatia Udhu, halafu tena Unasali, ndani yake unaomba Maghfira(Toba)basi ikiwa utashindwa kuacha hapo tena itabidi tukupeleke (Sober house) kama vijana wanavoita au ukajiunge (Rehabilitation clinic).Jiunge  uidumishe Sala ya Toba ipate kukuokoa na madhila haya ya Ulimwengu.

No comments:

Post a Comment