Sunday, September 14, 2014

URAFIKI WA SALA PART 2

Asalaam Aleiykum

Ndio nakutajia Sala ambazo zitakuwezesha kufikia lengo lako la kuwa Rafiki wa Sala na ukageuka kuwa Kipenzi cha Mollah wako,
Nakupa utangulizi wa maneno kuna vitabu vyengine vinasema hizi Sala hazijathibiti, Sasa wewe una hiyari yako kama alivyosema Mwanasayansi mmoja alipoulizwa kwanini unaamini Mungu? akajibu Majuto ya kutoamini makubwa pale ambapo ntakapokufa ikisha Mungu akawa yupo, nini hali yangu itakua wakati huo, basi bora Imani yangu itanitetea na kama hayupo basi vilevile sijapata hasara yoyote.
Basi na wewe hali kama hiyo kama utaamini hazijathibiti sawa, na kama itakua zimethibiti nini habari yako wewe katika hayo mapokezi kwa Mollah wako, Ama kwa hapa Ulimwenguni dalili ninazokupa mimi ni huo Urafiki, sasa una uamuzi wako kuzisali au kuziacha, sasa kwanini nikakukumbusha sababu kubwa watu wameacha hata Sala za sunna siku hizi wameziacha, hawajui kipi kinaruhusiwa na kipi kinakatazwa, misingi ya dini yote imevunjwa, na sisi wengine kazi yetu ni kutafuta (Vifusi) vilobakia ili tujaribu kujenga tena kama tutaweza, ziko wapi zile zama ambapo unakwenda Msikitini robo saa kabla ya Sala ya Fardhi ili upate kutanguliza Sunna zako, uko wapi Urafiki wa Sala siku hizi.
Sala ya Dhuhaa
Kwanini nikaanza na Sala hii kwa sababu nakutaka uwe mwenye kujizoesha kumsabahi Mollah wako baada ya kumalizika ile fardhi ya alfajiri, jipangie uwe mwenye kuipata sala hii ukiwa ofisini, ukiwa kwenye biashara, ukiwa darasani popote kuwa mwenye kukumbuka uipate sala hii kwani anasema Abuu Hurairah r.a "amenihusia Bwana Mtume s.a.w" kufunga siku tatu kila mwezi, kusali Rakaa za sala ya Dhuhaa, na kusali sala Witr kabla ya kulala.
Anahadithia Bibi Aisha r.a Alikua Mtume akisali Rakaa nne za Sala hii ya Dhuhaa na kuzidi.
Na fadhila zake Sala hii ya Dhuhaa kama vile uliyetoa sadaka, pia ni yenye kukuamrisha mema na kukuepusha na mabaya na mengine yalotajwa katika hadith, na Rakaa zimetajwa nyingi tu ikiwa utaweza kuziendeleza na umehimzwa kusoma sura ya (Fatiha na kufatiwa na Washamsi, na sura ya Dhuhaa.
Sala ya Istikhara(Maombi)unaweza kuisali wakati wowote uloruhusiwa sala za sunna, lakini ikiwa unataka upate ishara za maombi yako basi unaweza kusali usiku Rakaa zako mbili na kutaka kujulishwa maombi yako.
Sala ya Haja.
Utasali Rakaa mbili nakuomba haja yako.
Sala Ya usiku, soma mada ya (Faida ya Sala za usiku).
Na zengine zinofatia Sunna za Kabliya na Baadiya na pia usisahau rakaa mbili za Tahiyatul Masjid uingiapo msikitini. endelea part 3

No comments:

Post a Comment