Asalaam Aleiykum
Kutokana na hali hiyo ya usahaulivu Mwanaadamu anapita katika hali ya makosa kila wakati wa saa na dakika zake, hakuna anayevuka katika hilo isipokua yule ambaye amekwenda (Beyond) ya Woga na Ushujaa, ambaye sasa kwa mara ya mwanzo anaishi katika Utiifu, na ukiishi katika Utiifu Woga na Ushujaa vyote vinapotea, unakua Mja wa Mwenye enzi Mungu kama ilivyotajwa kwenye sura ya (Yunus aya ya 62-64)
أَلَآ إِنَّ أَوۡلِيَآءَ ٱللَّهِ لَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
"Wale vipenzi(Waja)wa Mwenye enzi Mungu hawatakua na Khofu wala hawatahuzunika"
Kwa sababu hawana woga wala ushujaa wao wanaishi kwenye Utiifu, na woga na ushujaa ni kwa wale ambao hawajafikia daraja ya kuwa vipenzi vya Mollah wao ili wapate kuondoshewa viwili hivi, sasa hawa ni watu gani?
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَڪَانُواْ يَتَّقُونَ
"Nao ni wale Waloamini na wakawa wanamtii(Kumcha)Mwenye enzi Mungu(Wakawa wanajiepusha na maovu)"
Ukiwa unatii huna wasiwasi maisha yako yanakua (Simple)huna haja ya kutetemeka, unaridhika na kila kitu.
لَهُمُ ٱلۡبُشۡرَىٰ فِى ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِى ٱلۡأَخِرَةِۚ لَا تَبۡدِيلَ لِڪَلِمَـٰتِ ٱللَّهِۚ ذَٲلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
"Wao wana mema katika maisha ya dunia na katika maisha ya Akhera, hakuna mabadiliko katika maneno ya Mwenye enzi Mungu, huku ndiko kufuzu kukubwa"
Na ukisharidhika unakua ushafanikiwa kupata Mema kutoka kwa Mollah wako, maisha yako yanakua ya aina nyengine kabisa hata kuyaeleza hakuna mfano wake mpaka uishi ndio utajua yakoje maisha haya ya (Bliss)unayapata hapa Ulimwenguni na huko Akhera, Na Mwenye enzi Mungu anasema huko ni kufuzu kukubwa, lakini kufuzu huku kunatakiwa ujitolee huo (Muhanga) wa Utiifu, sasa kama huko tayari ndio unapewa nafasi ufanye japo kidogo kidogo kwa njia ya Toba.
Endelea part 3
No comments:
Post a Comment