Sunday, October 12, 2014

NINI MAPENZI ?TAQWA PART 1

Asalaam Aleiykum

Nimetakiwa nitoe ufafanuzi  kuhusu darsa zilizopita niliposema (Taqwa) ni Mapenzi nilikua nina maana gani? kuihusisha (Taqwa)na Mapenzi, Ingekua rahisi kwangu kumjibu muulizaji kwa ufupi swali lake hili, lakini kanifunga aliponambia nilete ufafanuzi, sasa pakitakiwa ufafanuzi inakua pengine muulizaji pamoja na wale wengine wasouliza labda hawajui nini Mapenzi?, ndio maana ukatakiwa ufafanuzi ili wajue yana mahusiano gani na (Taqwa).
Sasa nakuchukua katika safari hii ili upate muangaza japo kidogo ikitokea siku nyengine unamwambia mtu neno la kupenda angalau uwe karibu japokua kwa neno, sababu sasa hivi unalitamka hujui hata maana yake, hujui hata kusudio, Nini Mapenzi?.
Mapenzi hayana Tafsiri ila yana ufafanuzi, na ufafanuzi wake ni kama hivi, Mapenzi ni Muujiza unaotoka(Mbinguni)unakuja na (Quality of your Being) au niseme mwenendo wa nafsi yako, na kila kiumbe anayo haki hii ya mapenzi, anaishi katika mapenzi na kinachotizamwa hapo ni hiyo (Quality)ya Mapenzi yake kayaelekezea wapi, tukijua yalipoelemea ndipo tutapata kufahamu ni mahusiano yepi yaliyopo baina ya Mapenzi na (Taqwa).
Mapenzi yanatokana na Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, sisi hatuna uamuzi katika jambo hilo, tunachoweza sisi kufanya ni kulikataa hilo penzi kwa njia tunazochagua sisi wenyewe, Nini Mapenzi? Mapenzi ni (Sharing of your Being)ni nafsi ilojitolea kwa njia ya (jihad)ukiniuliza mimi nitakwambia soma sura ya (Baqarah aya 2 na 3)
 ذَٲلِكَ ٱلۡڪِتَـٰبُ لَا رَيۡبَ‌ۛ فِيهِ‌ۛ هُدً۬ى لِّلۡمُتَّقِينَ 
"Hicho ni Kitabu kisicho na shaka na Muongozo kwa wamchao Mungu"(Wenye Mapenzi)
Kitabu hichi wameletewa wale wenye mapenzi ili uwe muongozo wao wa kuepuka maovu(Mabaya)watu hawa kwani wana mapenzi ya aina gani?
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَـٰهُمۡ يُنفِقُونَ 
"Ambao huamini yasoonekana na husimamisha Sala na kutoa katika yale tuliyowapa"
Hiyo ndio (Quality of your Being) imejaa mapenzi ya kile kisichoonekana, Nafsi yako iko kwa ukamilifu wa kile unachoamini kipo na ndicho chenye kukuongoza katika maisha haya na hayo ya baadae,ndio maana Walimwengu wakasema(Love is Blind)kisichoonekana(Usilaumu macho kwa kuwa hakioni jambo hili ulaumu Moyo kwanini mpaka leo haujapenda hichi kisichoonekana, Juta sana kukosa kitu adhimu kama hicho, Ndio maana ukiangalia kwa yule aliyekuwemo kwenye mapenzi kikweli anakua haoni kitu, mnayeona nyinyi watazamaji, mbona anafanya hivi, mbona kaacha kila kitu, hivyo hajui kama anapoteza mali yake, hizo zinakua shida zenu nyinyi lakini yeye kwa wakati ule ana(Enjoy)mapenzi yake(Love is from Beyond)linachukua Mamlaka yote ya kiumbe akawa hana uwezo wowote wa maamuzi, Na ukipata mapenzi ya kumpenda Mollah wako ukapenda dini yako wewe ndio umepata (Taqwa), baada ya kulijua hilo basi wewe huna linalo kushughulisha isipokua kusimamisha Sala, kuwasiliana na Mollah wako asiyeonekana, Na Mollah wako kama utampa mapenzi yako kwa ukamilifu basi atakuonesha Ufalme wake bado ukiwa Hai, Na watu hao kwa kuwa wamejaa Mapenzi basi wao hawana haja tena ya kuvizuia vile wanavopewa na Mollah wao, wana (Share)na yoyote yule iwe mali au nafsi zao kwa kujitolea, hilo ndio penzi (First class)Namba moja, halafu kuna penzi namba mbili(Second Class) Endelea part 2

No comments:

Post a Comment