Tuesday, October 28, 2014

KUMKUMBUKA ALLAH(DHIKR)PART 2

Asalaam Aleiykum

Sasa kama umeamua kwa Bidii kutaka kumkumbuka Mollah wako na uzidishe hizo dakika, basi soma maudhui hii kwa kituo ili ipate kukuonesha njia za kumkurubia Mollah wako na kumsabahi na kumkumbuka wakati bado una nguvu zako, usisubiri mpaka kuumwa au umefanya dhanmbi ndio ukakurupuka kukumbuka kuomba msamaha, au huna nguvu tena una wasiwasi karibu utakufa ndio ukaanza kazi hii, unatakiwa uianze mapema ikujae Moyoni na utapata manufaa yake makubwa baadae.
Nataka kukufahamisha kuwa ukitegemea kukumbuka ina maana wewe unaitegemea Akili, sawa, nzuri lakini inatakiwa uende (Beyond)Akili, kwa sababu Akili ina tabia ya kusahau ndio maana ukaambiwa ufikiri, lakini kuna kitu ambacho hakisahau ambacho ni huo moyo, na mifano nitakutolea hiyo sura ya (Fatiha)unaona unavyoisoma hutaki hata kuikumbuka sababu iko moyoni unaitoa (Direct)lakini zengine mpaka uzifikiri na mara unakwama, sasa nini kinachokusadia kukumbuka, kile ambacho hakikumbuki ila kinataja, moyo hausahau lakini unataka mazoea, lazima ujizoeshe ndio moyo unaweza kushika jambo, Na Mollah wako katumia mifano mingi kukupa mazoea hayo kwa kukujulisha kuwepo kwake, na kila mara anakukumbusha lakini wewe umo kuyasahau, sasa mambo hayo yepi ambayo unaishi nayo lakini hukumbuki chochote, kabla ya kuyataja mambo hayo wacha nikujulishe kitu kimoja kuhusiana na kile unachoambiwa kuona kwa moyo na kutaja kwake, moyo una uwezo wa kuona mara mbili ya mwanzo ni kuhisi(Feeling) na ya pili ni kuona kwa (Pureness)kuondokewa na pazia na unakua (Knower)unajua bila ya kuona huku kwa macho wala kufundishwa, kwa hiyo ukitia sauti ndani ya kujua huko ndio inakua sasa umetaja, na ukinyamaza kimya vilevile bado unaendelea kujua katika njia za ukimya, na yote hayo yamo katika kukumbuka, na kukumbuka huku kuna kua kila wakati na sio mara moja kama ilivyo sasa.
Sasa Ujumbe gani Mollah anatuletea ili tumkumbuke, endelea part 3.

No comments:

Post a Comment