Sunday, October 19, 2014

UFALME WA SHETANI (IBILIS)PART 3

Asalaam Aleiykum

قَالَ ٱخۡرُجۡ مِنۡہَا مَذۡءُومً۬ا مَّدۡحُورً۬ا‌ۖ لَّمَن تَبِعَكَ مِنۡہُمۡ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكُمۡ أَجۡمَعِينَ 
"Akasema (Mwenye enzi Mungu)Toka humo(Peponi-Mbinguni)hali ya kuwa ni mwenye kudharauliwa na mwenye kufukuzwa, atakayekufata miongoni mwao(Nitamtia motoni) niijaze jahannamu kwa nyinyi nyote"
Limetumika Neno kuijaza Jahannam kwa sababu kama nilvyo sema vigumu kumshinda shetani Ibilis isipokua kama utaweza kuyafanya mambo haya, ili kuweza kumshinda Ibilis na mbinu zake za kukupoteza kwanza inabidi utumie busara yako ya muamko ambao kama utauzingatia utatambua tafauti yako ya siku za utotoni na ujanani, na huu wakati ulo nao pengine wa uzeeni ambao busara zake zinakuonesha mambo wazi wazi pasipo na kizuizi, mfano hakika upo ukijitizama pale ulivopita utotoni bila ya fahamu zozote, umepita ukiwa huna maarifa na Akili imelala kabisa, na sasa umeamka ukawa unaelewa mambo kwa upeo wa mazingatio yakua hili baya na hili zuri,umegundua kumbe mali na vyote nilivyochuma havina maana kwangu, ukagundua siku zangu zinakaribia na huko niendako sichukui chochote, ukagundua mbona moyo wangu una mazito,Na vipi nitaufanya mwepesi tena, mwanzoni ulikua huwezi kupambanua lakini sasa hivi unaweza kutenganisha baya na zuri, haramu na halali na ukitaka kuyafanya unayafanya kwa hiyari yako ilojaa kusudi, kwa hiyo ukiamua kumsahau na kutomuabudu Mollah wako sasa hivi ni kusudi si usingizi tena, ukiamua kushughulikia mali hilo ni tendo la kusudi, ukijifunga na kushughulika na maumbile ya wanawake hilo pia ni kusudio ambalo huambiwi pole na utayapata mateso ya Mwenye enzi Mungu kama alivyosema mwenyewe kuwa ataijaza Jahannam kwa yoyote yule atakayemfata Ibilis, pia na wewe unafukuzwa na kudharauliwa kama nilivosema wa mwanzo kabisa kufanya hivyo Familia yako.
Sasa cha kufanya nini?Al-shuaraa-89 إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٍ۬ سَلِيمٍ۬ 
"Isipokua mwenye kuja kwa Mwenye enzi Mungu na moyo safi"
 kupata ukumbusho wa Mwenye enzi Mungu Fanya Biashara, wapende wanawake, lakini fanya bila ya matamanio ya kudumu katika nafsi yako, Fanya Biashara ukiwa huna tamaa ya kupata utajiri, mpende mwanamke lakini usianze kumuabudu ikawa huli hulali,Elewa vitu hivi ni vya muda, halafu ielekeze daima nafasi ilobakia umkumbuke Mollah wako, hapo utakua katika njia ya kati yenye furaha na jaza njema kutoka kwa Mollah wako, hapo utakua Duniani upo na Akhera pia upo, hugandi katika kitu kimoja, ushagundua hakuna kitu cha kudumu, kama Uraisi, ubunge,uwaziri,ubalozi vyote vinapita na kuna siku vyote vitakukimbia na kimoja tu ndicho kitabaki na wewe nacho ni huyo Mollah wako, siku hiyo ikifika utakua na furaha ya kusema Mollah wangu japo nilikua kwenye Biashara, japo nilikua na Mke au Mume wangu lakini wewe ulikua hunitoki moyoni mwangu nikiamini siku hii itafika ya mimi kukutana na wewe kama vile ulivyoniumba mwanzoni, kwa hilo Mollah wangu nakuomba Nisamehe unikaribishe kwenye Ufalme wako wa Kudumu. Mollah wangu leo niko katika Ufalme wako nikiwa kimya mimi na Malaika wako, wakati Mpaka walo wangu wanaogopa hata kulala na mimi chumba kimoja kwa kuwa nimeshakufa, basi mimi sina mwenginewe isipokua wewe Mfalme wa Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo, na kwa hilo Mollah wangu nipokee kwenye utukufu wako hali ya kuwa nimesamehewa na nimeridhiwa kwa kuweza kumshinda Shetani Ibilis mwenye kuwapoteza waja wako.
Mollah wetu tujaalie mazingatio haya yadumu nyoyoni mwetu na tuwe wenye kufanikiwa na kupendwa na wewe Mlezi wetu. Amin

No comments:

Post a Comment