Asalaam Aleiykum
Nakuletea zawadi nzuri ya maneno yalojaa hekima kama utayatafakari kwa makini na kuyapa uhuru maneno hayo kushuka moyoni mwako basi yatakua ndio mwanzo wa mageuzi yako ya kukufanya kuwa mtu wa Mungu, Ufahamu wako wa mambo ya maisha haya unayoishi utageuka kuwa mwengine kabisa, utakutana na ukweli uso na macho, hiyari itakua yako kuukubali ukweli au kuukataa,hapo utajijua katika falme hizi mbili wewe unaishi wapi, ukishagundua (Kukumbuka) wapi uliko itakua rahisi kwako kupata mafanikio ambayo yatafatia yenyewe baadae.
Kumbuka huwezi kugundua siri ilofichikana mpaka hayo maneno yaende (Deep)kwenye moyo wako neno baada ya neno, kwanza napenda ufahamu nilivyotaja falme mbili nilikua naelekeza Akili yako kwenye jambo fulani, Lakini haiwezekani kabisa katika Ulimwengu huu kuwepo Falme Mbili, Ufalme ni mmoja na ni wake pekee(Subbhanna Allah)Mollah wetu mlezi, ili upate kunifahamu nimekutajia huu Ufalme mwengine ambao ni (Fake) wa Uongo na ndio wengi wetu tumechagua kuishi katika kasiri hii ya (Mwinyi Ibilis).
Sasa tuingie kwenye chanzo cha Darsa yetu hii ya Ufalme wa Shetani kwa kuichukua aya iliyomo kwenye sura ya Al-Aaraf aya ya 16 mpaka 18.
قَالَ فَبِمَآ أَغۡوَيۡتَنِى لَأَقۡعُدَنَّ لَهُمۡ صِرَٲطَكَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
"Akasema Kwa kuwa umenihukumu upotofu(Kupotea kwa jeuri yangu)Basi nitawakalia(Waja Wako)Katika njia ilonyooka(Ili nipate kuwapoteza)"
Isije kutajwa njia ukaona labda kuna njia reefu ikisha pana ya kupita, Njia ilonyooka ni ile kanuni ya haki yenye kubainisha Uhalali wa kila jambo katika Dunia hii, Yeye kachukua Ahadi ya kukaa kwenye hiyo halali ambayo nyinyi mnaitaraji ikuvueni kwa usalama katika maisha haya yeye ndio anakwenda kukaa hapo, nini anafanya? kazi ni moja kukusahaulisha na kukufitini na Mollah wako ndani ya hiyo Halali, na rahisi sana kughilibiwa ndani ya huo Uhalali kuliko kwenye hiyo haramu kama tutavoona huko mbele.Kwa sababu ndani ya Halali ni vigumu kugundua kwamba unafanya makosa, ni vigumu kuona kwamba umetoka kwenye Uhalali na unaishi katika Haramu, unatenda yalo ya haramu, umezama kwenye haramu na ufisadi lakini kupitia ndani ya halali, Vipi Mfalme Ibilis Kakaa kwenye njia ilonyooka?
Endelea part 2
No comments:
Post a Comment