Sunday, October 12, 2014

NINI MAPENZI ?TAQWA PART 2

Asalaam Aleiykum

Al Imran 14
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٲتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَـٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَـٰمِ وَٱلۡحَرۡثِ‌ۗ ذَٲلِكَ مَتَـٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا‌ۖ وَٱللَّهُ عِندَهُ ۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ 
"Watu wametiwa Huba(Mapenzi)ya kupenda wanawake na watoto na mirundi(wingi)wa dhahabu na Fedha, na Farasi wanaotunzwa vizuri, na wanyama na mashamba, na hayo ni matumizi ya maisha katika dunia, na kwa Mwenye enzi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri".
Niliposema tumezungukwa na mapenzi nilikua namaanisha zilivyofanywa Nafsi zetu ni kuishi katika hayo mapenzi, hakuna kosa kabisa, ukiwa hupendi wewe utakua na matatizo, ukiwa hutaki wenzio wapende wewe ndio kabisa unaumwa, hayo mambo yamewekwa na Mwenye enzi Mungu mwenyewe ili mpate kufurahi katika Dunia hii, na ikisha mnapewa taarifa kuwa yapo mazuri zaidi huko Akhera mnaporejea.
Sasa ukiyatizama mapenzi hayo ni (Vipande vipande)umependa hiki au kile, umpenda gari, umependa nyumba, umependa chakula, huko ni kugawika kwa mapenzi, na mapenzi ukiyagawa ndipo yanapatikana matatizo makubwa, mara unampenda huyu mara akipita yule ushampenda huyu umemsahau, kwa hiyo unakwenda na tabia hiyo mpaka mapenzi ulopewa na Mwenye enzi Mungu yanageuka kuwa (Desire) unakua mwenye kutaka kitu kufa kupona, na jambo hilo linakusahaulisha kila kitu, na hapo unakua mwenye kuharibikiwa kabisa, kwa hiyo hilo (Penzi)la (Second Class)huwezi kuliita (Taqwa) kwa sababu lishakuondoa katika kumpenda Mollah wako, unamshirikisha na vitu vyengine, unapenda kila unachokiona, na (Quality)yako inakua (Fragment).
(Taqwa) ni (Unity of Love)ukimpenda Mollah wako vyote vinafatia bila kipingamizi, unakua unapenda kila kitu kwa pamoja, lakini kwa sasa hivi wewe ulivyo unachagua, na kuchagua ndio matatizo yanokufanya usiipate (Taqwa)sasa kama huipati Taqwa, hupati kuyakamilisha mapenzi yako unaamua kufanya nini mpaka kufa kwako? Endelea part 3.


No comments:

Post a Comment