Asalaam Aleiykum
Al-Fajr aya ya 20
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
Na Mnapenda Mali Pendo la kupita kiasi.
Kitizame kinyanganyiro kinacho kukumba, Mollah anakwita kwenye mapenzi yake, jitizame vipi unavo mjibu, bila kutoa sauti unamuonesha kwa ishara, mimi bado niko kwenye siasa, mimi bado nashughulika kutafuta mali,mimi niko nafanya maarifa vipi nitayamaliza mambo ya watu, mimi najenga majumba, mimi natafutia wake zangu na wanangu Mali, niko mbioni kusimamia mashamba, nakwenda kazini asubuhi mpaka jioni vipi nitakukumbka Mollah wangu, Fulani anaumwa mimi namshughulikia sipati wakati wa kuabudu, nasimamia jengo sina nafasi.
Mapenzi yakuchuma Mali yamekushughulisha huwezi kuyawacha ndio maana ukaambiwa bora "Ngamia ataweza kupita kwenye tundu ya shindano"kuliko wewe afadhali ngamia atakua anafafanya jitihada za kujikunja ili apite, lakini wewe kwanza utatafuta uzi uko wapi uuze kwanza ikisha ndio upite kwenye tundu ya shindano, Mali imekushughulisha sana, hujui tena hata maana ya kupenda, hata penzi likiwa mbele yako unauliza hichi nini?. Kila mmoja wetu kashughulika na utafutitaji wa Mali ikisha ikisha nini? unaziacha Ulimwenguni huendi hata na karatasi ya kusema mimi nilikua na Mali, Mimi nilikua na Majumba na magari, mimi nilikua na viwanja na mashamba, yale yote uliyokua unayashughulikia unayawacha unakwenda mikono mitupu, huja starehe kabisa sababu siku zote ulikua unatafuta na kuilinda mali yako, huku mapenzi yapo pembezoni mwako yanakwambia geuka unipende wewe upate furaha, acha na mambo ya kidunia hayana maana, ukiandikiwa uyapate utayapata, na kama hujaandikiwa basi utahangaika bure, na hayo ndio mapenzi ya hali ya chini kabisa, mapenzi ya mateso, na mifano ipo tazameni matajiri wenu hawana furaha kabisa, sikatai wana (Security)lakini furaha haipo, hawajui kupenda wala kupendwa, na wakipendwa wanadhani huyoo anataka mali yangu, hayo ndio mateso kila mmoja wetu anashindwa kuyaepuka.
Sasa jiulize wewe Mwenyewe ukoje katika kadhia hii ya mapenzi unapenda nini? Unampenda Mollah, au Mpira, Unawapenda watu au kikundi, unapenda Nyumba zako au Mashamba yanakusumbua na faida zake, au una maradhi ya pesa uzione tu ukishajigundua wewe mapenzi yako yamehimili wapi basi anza taratibu kuya(Mix)na kumpenda Mollah wako ili upate hiyo (Unity)ya mapenzi nayo ndio hiyo (Taqwa) na ukipata hiyo ndio umefanikiwa kukubwa na Raha na Furaha zilizopo hapo unatakiwa lazima wewe Mwenyewe upate (Exeperience)hiyo, hutoelewa mtu akikuhadithia, hayo ndio mapenzi katika kipimo chake cha juu kabisa.
No comments:
Post a Comment