Tuesday, October 28, 2014

KUMKUMBUKA ALLAH(DHIKR)PART 1

Asalaam Aleiykum

Wanasema Wanasayansi Mwanaadamu Bingwa wa Maarifa(Genious)hodari wa kupita mfano anaitumia Akili kwa uchache wa Asilimia 15 tu, Na hiyo katika jambo pengine hususia la uvumbuzi wa kitu fulani na huku akiacha mambo mengine chungu nzima yakimpita. Sasa ikiwa hali kama hiyo inatokezea kwa Bingwa kama huyo, nini habari yetu ya mimi na wewe tunatumia kiwango gani cha Akili zetu katika kujishughulisha na mambo yote yalotuzunguka?.
Inapaswa Mwanaadamu ajiulize asilimia ngapi anatumia, na katika kuzipata asilimia hizo ujitizame pia kiasi gani unatumia katika kumkumbuka Mollah wako, kama hutaki mahangaiko hayo basi nipe nafasi nikuonee mimi huruma ili nikupe kiwango chako unachotumia kwa ukamilifu kumkumbuka Mollah wako kwa masaa 24, Wallahi huzidi ila dakika 10 na nitakuonesha vipi kama angalau unazipata hizo dakika 10, Anzia wewe mwanzo unapomkumbuka Mollah wako labda tuseme kwenye Adhana unapoisikia au kipindi cha Sala kinapoingia basi muda wote huo mpaka kusali kwako labda ni dakika mbili tu ambazo pengine ndizo unazo bakia na Mollah wako, lakini mawazo yako safarini kuanzia kwenye Udhu mpaka Sala nzima, hukai hata sekunde saba katika kumkumbuka huko Mollah wako, kutwa unaendelea ku (Process)mawazo haya na yale, na ukiingia katika hiyo Sala basi unaweza hata kutukana au bure linakutoka (Fonyo)kwa ajili ya fulani alivyo kukera, hutulii kwenye Sala Abadan, unakaribia kukufuru mambo chungu nzima yanakuja katika hiyo Sala, na hapo ndio sehemu moja pekee ambayo labda unatakiwa umkumbuke Mollah wako kwa ukamilifu, lakini wapi viuno vinakuja hapo, michezo ya Tv unamalizia hapo, madeni unayalipa hapo, imekua Sala yote ni kitendo cha kupanga mambo yako na vipi utayatekeleza, ndio maana nikakupa angalau dakika mbili labda unamkumbuka uso umeumbwa na haya katika masaa 24 basi usipate hata hizo dakika 10, usishangae kuna wengine hawapati kabisa, hawajaanza safari hii ya kukumbuka hata hatua moja. Sasa wewe ulopata nafasi ukayajua haya nakuomba Jiulize hivo yule alokuumba akakupa Uhai anastahiki dakika 10 au zaidi ya dakika hizo, katika darsa hii nakufungua macho ili upate kujua vipi utamkumbuka Mollah wako, nini ufanye mpaka upate ladha ya kuwa karibu na Mollah wako.
Endelea part 2

No comments:

Post a Comment