Asalaam Aleiykum
Siku zote nimekua nashangazwa na jinsi gani Mawalii (Mystic)Wacha Mungu wanavo yakabili Mauti wakiwa hawana hofu, hujiuliza kuna kitu gani kinacho wapa matumaini mpaka kufikia kuaga, "anasema Mcha Mungu sasa basi msinipe dawa nimebakisha siku moja, Nyinyi msinitese tena kwa chakula kwani sina muda tena wa kuwa na nyinyi, na mwili wangu ushafungika haupokei tena hata maji, Na hadith nyingi ambazo kwa sasa ni mara chache sana kuzisikia.
Leo wako wapi wale walokua wakiaga nakwenda zangu kwenye dongo langu (Kufia)Mombasa, Wako wapi leo walofunga mizigo yao na kusema nakwenda kuzikiwa (Comoro), Wako wapi leo wale kwa makusudi anasema nikatieni (Ticket) mimi ntazikwa (Yemen).
Hakuna tunacho kiona katika (Generation) hii ila khofu kubwa ya Mauti, Nini kimetokezea?, Ni kweli isiyo shaka kwamba Mauti ni jambo zito sana, kishindo chake si kidogo, Roho haijawahi kushuhudia tukio kama hilo, Kiza kinene katika (Operation) hiyo kubwa ambayo kila mmoja wetu hana budi kupita katika (Theatre) ya Mauti.
Wengine inawachukua (Week), wengine mwezi mzima Roho kutenganishwa na kiwiliwili(Body) wale walokua hawajui kadhia hii wataona kama hadith lakini madada zetu waliopo (Hospital) manesi wanavijua vishindo hivi wanavokabiliana navyo kila siku, na yoyote mwenye kupinga na aende akashuhudie kadhia hii, atarudi na kusema kumbe kweli wanayosema si mchezo jamani Mja kutolewa Roho.
Hali hii ya kutolewa Roho imetajwa ina wakabili watu wa aina tatu katika sura ya (Waqia aya ya 88 mpaka 95)(فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ)
Kundi la (1)
Ikiwa katika Maisha yako ulikua karibu na sisi kwa matendo mema na yaliyo mazuri, Na ukawa na mapenzi na sisi, ukajua ya kwamba yupo alokuumba na anastahili kukumbukwa na kuabudiwa na kushukuriwa kwa kila saa na dakika, Basi wewe kabla ya kufa kwako utapata Fahamu ya kujua alaa kumbe Mauti na Uhai ni kitu kimoja hakuna mushkeli, na siwajibiki mimi kuogopa, tena na siku ya kufa kwako unafurahishwa kwa manukato mazuri mazuri na pepo unaoneshwa mbele yako, unawekewa wazi kule ndipo unapokwenda, hapo unakua tayari kuondoka bila ya mashaka katika (Body) yako wala hunganganii tena kubakia katika Ulimwengu huu, unakwenda bila ya ushindani ukiwa umeridhia huku umekubali kurudi kwa Mollah wako kwenda kupumzika katika (Jannat Firdous)uko radhi sasa kwenda kukutana na wale waja wema walo kutangulia kabla yako.
Endelea part 2.
No comments:
Post a Comment