Sunday, March 22, 2015

NDANI MCHA MUNGU NJE MCHA MUNGU PART 1

Asalaam Aleiykum

Maombi na huruma zangu Mollah wangu ni kuwaombea wale Masheikh wangu na ndugu zangu Waumini wenzangu na mimi Mwenyewe pamoja na Waislam wenzangu walokua hawafahamu maana halisi ya Ucha Mungu, Mollah wangu wafikishie Rehma ya Kufahamu wote kwa jumla.
Watu wamekua wamo katika ubabaishaji wa kudhani kuwa ukiwa unavaa vazi fulani au unatenda mambo fulani kwa ajili ya Allah basi huo ndio Ucha Mungu, Ikazama dhana hii mpaka kuwaona wale wenye kuishi maisha ya kawaida na kufata Amri za Mwenye enzi Mungu hao hawana nafasi kwa Mollah wao, mpaka uwe una kitu cha ziada cha kukuonesha wewe tafauti na wengine ndio unakua Mcha Mungu. Vimekithiri Viburi hivi hassa kwa wale wenye kudhani wako karibu na Mollah wao zaidi kuliko wengine, hivyo ndio kiburi kifanyavyo kazi yake, ikampitikia Mtu katika Akili yake kuwa yumo kwenye nyumba za Ibada, au wanatenda mambo ya Khairat basi huo ndio ucha Mungu, Shetani katumia Fursa hii kuwafunika kwa Mwanvuli wa upotofu wa Kiburi mpaka kufikia kuwatoa katika Dini pasi wenyewe kujijua.
Imefikia hali kama hii pengine kutokana na uchache wa kujua, au ubishi wa kutotaka kufahamu, au ndani ya moyo kuna mizigo mingi ndio maana Ucha Mungu hauna nafasi ya kukaa. Nawaona watu wengi sana wanasumbuliwa na hali kama hii, lakini kwa kuwa ni siri ikaayo ndani hakuna mwenye kutaka kuisema.
Kwa hiyo Mimi kazi yangu daima ni kukuonesha njia, ikisha una hiyari yako mwenyewe kuifata au kubaki kama ulivyo sasa. Kujua vipi utaupata Ucha Mungu wa ndani, halafu uupate na wa nje  inabidi nikuchukue twende tukayahudhurie maneno matatu yalosemwa ndani ya Quraan, Yamesema Nini?.
Kwanza kabisa katujua kwamba sisi sote Ima wafanya Biashara au Wanasiasa, kwa hiyo akaanza maneno yake kwa kututega, sasa kama wewe unakula pesa za Msikiti, au unakula pesa za Umma, au unavamia kufilisi mali za Yatima, au unajifanya (Tabibu) unaponesha watu kwa kuwaombea kwa kuwadanganya na kuchukua pesa zao ukiwa huna hakika na ufanyacho, Huku unajikita kuamini unafanya mambo ya kheri, basi Nabii Musa a.s kakugundua udhaifu wako huo ndio akaanza maneno yake ambayo nataka uyasikize kwa uzuri huenda yakaleta faida kubwa katika safari yako ya kuutafuta Ucha Mungu.
Endelea part 2

No comments:

Post a Comment