Asalaam Aleiykum
(وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَـٰبِ ٱلۡيَمِينِ )
Na kama Ulikua Mwenye (Imani) basi salama itakua juu yako, kwa sababu (Imani) ni (Mapenzi) na mwenye mapenzi hatendi mabaya abadan, Lakini kuamini kwenyewe isiwe umekubali kwa kuwa umezaliwa ndani ya (Uislam) basi iwe umeamini, sio kwa kufata kundi kwenda Msikitini, Kuamini kwenye kunatakiwa kuwe katika Uhai wako, ushapata kitu katika moyo wako tayari kina kuongoza kwa Mollah wako.
Sio Imani ile ukiguswa ukucha ushamsahau Mollah wako, Mambo yakenda vibaya unatafuta Mtu akusafishie nyota, ukipatwa na misukosuko mara ushatoka dini, Imani inayotajwa hapo ni ile ya juhudi uliyoifanya kuwa karibu na Mollah wako, vipi ulikua unaubeba ukumbusho wa Mollah wako wakati wa kula na kunywa, jee ulikua ukimtaja wakati wa kulala na kuamka kwako, Jee alikuwepo moyoni Mollah wako wakati ukizungumza na kukaa kwako kimya?, Jee Imani hiyo ilikutupa kwenye kuwakumbatia Mayatima na Maskini, ilikua nini tabia yako pale alipokujia muombaji ukitoa kwa unyenyekevu au ulikua ukinyanyua midomo kwa dharau.
Imani yako hiyo ilikupelekea kuwasaidia Wajane, kuzishukuru neema zetu, vipi hali yako ilikua wakati ule tulipokupa Baraka za afya ulifanya vitendo gani vya kheri vyenye kuhusiana na Imani, Jee uliwasaidia wazee na watoto, ulijitolea nguvu zako kuinufaisha jamii ilokua karibu yako, Imani yako ilikufanya uishi vipi na Walimwengu wenzio, ulijua kwamba wanastahiki heshima, huruma na haki ya Ulimi wako, kutowasingizia mambo ya uongo ili waadhibike, Na kama uliyaamini maneno yetu tuliyoteremsha katika kitabu basi leo yakabili Mauti kwa salama, ondoka katika Mwili wako bila ya matatizo au mashaka yoyote.
Endelea part 3.
No comments:
Post a Comment