Sunday, March 22, 2015

NDANI MCHA MUNGU NJE MCHA MUNGU PART 2

Asalaam Aleiykum

 يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ هَلۡ أَدُلُّكُمۡ عَلَىٰ تِجَـٰرَةٍ۬ تُنجِيكُم مِّنۡ عَذَابٍ أَلِيمٍ۬ 

"Enyi Mloamini Nikujulisheni Biashara mtakayofanya na Mollah wenu" Ili Muepuke adhabu iumizayo ya Mwenye Enzi Mungu.

Vipi iwe jambo hili wameambiwa Waumini? Kwanini isiwe wasoamini, Wale wenye kutenda Dhanmbi, kwanini iwe nyie mlokwisha amini? Kwa sababu unajulikana Udhaifu wetu, tunajulikana tumevaa majuba tumo kwenye Nyumba za Ibada lakini vifuani watupu, Ndani hakuna chochote(Debe Tupu) ndio tukaambiwa Jambo la mwanzo sasa" Muaminini Mwenye enzi Mungu",(Nini Tafauti ya Imani na kuamini) Kuamini ni jambo la urahisi sana, unaambiwa kitu unakubali(Hivyo ndivyo mlivyo sasa).
Lakini Imani ni kitu chengine kabisa, lazima ufanye mambo ndio Imani ipate kukuamini, Kwa sababu Imani ni (Double Arrow) Toa upewe, Nini Imani? (Mfano wa Imani) ni mapenzi, sina shaka sote tushaonja (Ladha) ya Mapenzi, lakini mapenzi ninayozungumza hapa ni ya aina nyengine kabisa, sio yale ya kawaida ya kila siku, haya ninayozungumza mimi kama yatakushukia moyoni ndio huo (Ucha Mungu).
Sasa hivi huna kitu kama hicho, Ndio unajaribu sikatai, lakini moyoni kuna mapenzi (Fake)yamejazana, unapenda mali, umejaa kiburi na tamaa, mapenzi ya uhasidi yamo humo, mpaka usafishe moyo wako mambo yote ya ujanja ujanja ulio nao, na uwe mweupe moyoni ndio mapenzi ya Allah yanapoanza kuteremka, Ndio Ucha Mungu unachukua nafasi yake. Unakua huna haja tena ya watu wakujue una Iman, au wewe Sheikh, unakua unajijua mwenyewe kilichomo ndani ya nafsi yako.
Nini kinatokezea ukiipata hali kama hiyo? Furaha juu ya furaha, zawadi tele zinateremka kutoka kwa Mollah wako(Bashara chungu nzima unazipata kutoka kwa Mollah wako) Watu watavutika na wewe kwa kutaka kuwa karibu na wewe, lakini kwa hivi sasa bado huna Ucha Mungu wa ndani, bado haujajitokeza, bado Imani haijashuka, bado huna ukaribu na Mollah wako, hujapata kujua dalili zozote, mawazo yako na fikra zako zote zimezama kwenye mali, kwenye pesa, kwa watoto, ndugu na hivi na vile, mapenzi yako umeyagawa mafungu robo hapa, robo pale.
Hebu Jitizame kama una chembe ya Ucha Mungu, akija Mlevi kukuomba shilingi ya kula, jione unakua vipi? Unavaa taji la hakimu, unaanza hukumu zako, au akujie (Mlemavu)unasema huyu kazidi  kuomba, lakini Mcha Mungu wa kweli akiombwa anatoa halimjii wazo lolote baya au zuri, hataki hata kujua huyu nani na dini gani, Moyoni kajaa mapenzi anajua moja kwa moja mja huyu katumwa na Mollah wangu ambaye anawapa wanomuamini na wasiomuamini, walevi na wacha Mungu, wasomuabudu na wenye kumuabudu, mie kama nani nipitishe hukumu yangu.
Ikikujia hali kama hiyo na kuweza kupambambanua  na kujua Qadar ya Mollah wako za kheri au za shari, ikawa unaridhika kujaribiwa kwa Mitihani na Mollah wako, Na kila ukijaribiwa wewe unazidisha mapenzi juu yake, hulalamiki wala hununguniki, huna hasira wala kuhamaki, ndio kwanza unazidisha shukurani, hapo wewe tayari ushamiliki(A loving heart) Ucha Mungu tayari, Unayo hiyo Iman, ukishapata hilo jambo la kwanza, ndio sasa unaruhusiwa uende kwenye jambo la pili, Kwa sababu sasa hivi ushakua na mapenzi ya Mollah wako, Na Mwenye Mapenzi hamkeri mpenzi wake, huwezi kutenda kero kwa Mollah wako wala kwa viumbe wenzako, sababu ushakua Mcha Mungu.
Inakua vigumu kwako kutenda dhanmbi kwa kusudi, haiwezekani tena Mcha Mungu akatenda maasi ya jambo lolote lile.
Endelea part 3




No comments:

Post a Comment