Sunday, March 1, 2015

FUNGUO 99 ZA IMANI PART 1

Asalaam Aleiykum

Utakapo kaa peke yako usione haya hebu jiulize Imani ni kitu gani?, Jee mimi ninacho kitu hicho kiitwacho Imani?, Angalia sana kifuani mwako useme mbona mimi Nasimamisha(Sala)siku zote, Najaribu kuwa msafi nisifanye Dhanmbi, lakini hayo yote nayatenda huku moyoni nikiwa mtupu, Hata nikitoa sadaka natoa ima nipate picha au watu wanishuhudie kuwa mimi mtoaji na mimi ni mfanya mema, lakini hakuna chochote chenye kutokea katika nafsi ya moyo wangu.
Walisema Waarabu tumeamini, Wakajibiwa(Quraan sura ya Hujraat aya ya 14)
"قَالَتِ ٱلۡأَعۡرَابُ ءَامَنَّا‌ۖ قُل لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ وَلَـٰكِن قُولُوٓاْ أَسۡلَمۡنَا وَلَمَّا يَدۡخُلِ ٱلۡإِيمَـٰنُ فِى قُلُوبِكُمۡ‌ۖ وَإِن تُطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُ ۥ لَا يَلِتۡكُم مِّنۡ أَعۡمَـٰلِكُمۡ شَيۡـًٔا‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ"
"Walisema Waraabu(Wakao Majangwani)Tumeamini, Sema (Uwaambie)Hamjaamini, Lakini semeni tumesilimu, Maana Imani haijaingia vyema Nyoyoni mwenu bado, Na mkimtii Mwenye Enzi Mungu na Mtume wake, hatakupunguzieni chochote katika vitendo vyenu, kwa yakini Mwenye Enzi Mungu ni Mwingi wa kusamehe na Mwingi wa Kurehemu".
Wewe hujasema lakini bado uko kwenye Jangwa la saruji, Umekubali leo pengine mwaka wa arobaini bado Imani haijaingia, usije ukanyanyuka na kusema mimi nishaamini, Imani ni kitu chengine kabisa ambacho kinatokezea kwenye Moyo.  Utajiri uko wa aina mbili wa kwanza ni ule wa Nje ambao kila mtu anauona wa magari, majumba, dhahabu na kadhalika, na ule wa pili ni wa ndani ambao ni wa thamani zaidi na huo ndio hiyo Imani.
Na dalili za hiyo Imani zina mfano kama wa (Mapenzi na Afya), sasa kama unajua nini Mapenzi na nini afya basi utakua tayari kujua nini Imani, Napenda kukufahamisha ikiwa utaupata utajiri huu wa Imani basi hakuna chengine chochote chenye kuweza kukushughulisha, hata mtu awe na utajiri wa aina gani wa mali basi utachofanya kikubwa ni kumcheka. Lakini kwa sasa bado usihangaike huna hicho kitu kiitwacho Imani, wewe umezaliwa tu kwenye dini umekuta watu wanafata na wewe umefata, umesomeshwa umejua kidogo kusali lakini huna taaluma ya hiyo Imani, ipo kwako kwa njia ya maandishi na bado haijafika moyoni.
Sasa umefika wakati na wewe kukipata kitu hichi ndio maana nakuletea funguo hizi 99 ili upate kuzitumia kuufungua huo moyo wako.
endelea part 2

No comments:

Post a Comment