Asalaam Aleiykum
Talaka hiyo kwa jina la (Sheria) inaitwa (Khul). Nini maana ya Talaka, kwa lugha ya kiarabu neno hili limehusiana na kumpa mnyama uhuru wake(To set animal free). Sasa hii Talaka ya (Khul) imetokana na neno la (Khul-al-Thaub) na tafsiri yake ni kuvua nguo kutoka kwenye mwili, na asili yake imehusiana na aya katika Quraan inayosema "Hao Wanawake ni nguo zenu na nyinyi ni nguo zao kwao. Sasa kama wewe unavua na yeye pia ana uwezo wa kuvua, hapana maonevu haki sawa kwa nyote wawili.
Kama sheria inavoamrisha Mwanamme kuacha na Mwanamke kapewa uwezo huo wa Kisheria ikiwa itakua Mwanamme anamfanyia mateso ambayo hayasthamiliki, Uislam umefanya hivi ili isije kuwa mateso kwa (Family) nzima ikawadhuru mpaka watoto kwa magonvi na mapigano. Wanazuoni wa Madhehebu zote wameitaja Talaka hii ni kama tendo la kurejesha Mahari na kutamka neno hilo la (Khul). Quraan na Hadith imeweka muongozo wa jambo hili kama aya ilivosema (128 sura ya An-Nisaa)
"وَإِنِ ٱمۡرَأَةٌ خَافَتۡ مِنۢ بَعۡلِهَا نُشُوزًا أَوۡ إِعۡرَاضً۬ا فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡہِمَآ أَن يُصۡلِحَا بَيۡنَہُمَا صُلۡحً۬اۚ وَٱلصُّلۡحُ خَيۡرٌ۬ۗ وَأُحۡضِرَتِ ٱلۡأَنفُسُ ٱلشُّحَّۚ وَإِن تُحۡسِنُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرً۬ا
Na ikiwa kama Mwanamke akiona kuwa Mume wake kugombana(Kumezidi)au Anatekelezwa(anatupwa na Mume hatizamwi), Basi si vibaya kwao wakitengeneza baina yao Suluhu, maana Suluhu ni kitu bora, Japokua Nafsi za (Wanaume) zimewekewa ubakhili mbele, Na kama mkifanya mema na kumcha Mwenye enzi Mungu, Kwani Mwenye enzi Mungu anazo khabari za yote mnayoyatenda.
Wengine wakasema ama aya hiyo inamtaka Mwanamke asubiri afanye Suluhu, sasa suluhu ya nini? wakati anapigwa, mume ana mwanamke nje, anatengwa hatizamwi, anapata shida na watoto, hatimiziwi haki zake, mateso na matusi yamezidi, nini afanye? Suluhu yenye ndio hiyo (Khul) Amwite ewe Bwana fulani kutokana na hivi tunavoendelea mimi siwezi tena, kwa hiyo shika mahari yako niwachie mie huru(Ukitaka usitake) ndio Maana aya ikataja hapo (Wanaume kwa hamaki wanaweza kukutajia mapesa chungu nzima kutokana na Ubakhili wa Roho na hamaki za kupewa Talaka) Na kama ikiwa Mwanamme anajua haki na yeye Mcha Mungu basi anaridhia ombi hilo la Mwanamke.
Na Hadith iliyomo katika Sunnan al- Baihaqq "Inasema"
Mwanamke alikuja kwa Bwana Mtume s.a.w akamwambia"Namchukia Mume wangu nataka aniache" Bwana Mtume s.a.w "Akamuuliza jee utamrejeshea shamba alokupa kama Mahari yako"Yule Mwanamke akajibu Naam na hata zaidi ya hayo" Bwana Mtume s.a.w akasema usirejeshe zaidi ya hayo.
Na kesi ya Mwanzo ya Khul katika Uislam imehadithiwa na Imam Bukhari kama hivi "Mke wa Thabit bin Qais kenda kwa Mtume s.a.w akasema""Ewe Bwana Mtume s.a.w"Mimi sijamkasirikia Mume wangu Thabit, kwa ajili ya mahamaki yake au dini yake, Lakini nakhofia kuna kitu kinaweza kutokea kwangu mimi kinyume na dini ya Mwenye Enzi Mungu, kutokana na sababu hiyo nataka niachike kutoka kwa mume wangu, Bwana Mtume s.a.w akasema jee utamrejeshea Thabit shamba lake alokupa kama mahari ili uachike, akajibu naam, akamwambia Thabit chukua shamba lako na mpe Talaka yake.
hivyo ndivyo mambo yanavokwenda hakuna kuteseka kwenye ndoa ila kinachotakiwa ufate hiyo sheria ya (Khul) katika mahakama za (Qadhi) ili ipate kuthibitishwa, lakini huna haja ya kuteseka na jambo usilolipenda, kuvumilia madhila na kero na machungu Dini imekupa nafasi na wewe Mwanamke kuamua jambo hili, na huo ndio usawa na hiyo ndio haki aliyokutakieni Mollah wenu. Lakini ole wako usije kufanya mambo haya ukawa nyuma yake kumbe kuna (Kicheki Bobi) kinakusubiri uwachwe, uharibu maisha yako na ya watoto kwa ajili ya mambo machafu, utatiwa machungu na adhabu mpaka mwisho wa umri wako, hiyo ndio tahadhari ninayokupa, lakini kama hakuna sababu za udanganyifu ila humpendi mumeo, au mateso yamezidi, au kakutupa basi kamata peni na karatasi umalize udhia huo na Mungu atakusaidia.
No comments:
Post a Comment