Sunday, April 12, 2015

MAISHA NI KITU GANI ? PART 3

Asalaam Aleiykum

Kwa sababu pale kwenye kitanda ndipo penye ukweli, kwenye kitanda ndio kwenye maisha, pale ndipo ulipo lala, ndipo ilipo (Body) yako imepumzika, Roho yako imetulia, lakini yenye kuhangaika ni hiyo Akili yako, ambayo inahangaika usiku na mchana wewe ukiamka unafatisha amri zake, siku utakayo amka na kuacha kusikiliza akili yako siku hiyo ndio utaanza kuishi, utaanza (Jihad Nafsi) kwa sababu Nafsi ikitawaliwa na Akili huna maisha mpaka Nafsi itawale Akili ndio hapo utakua unaishi.
Nini Maisha?
Maisha ni hali hiyo ulo nayo sasa hivi, zengine zote ulo nazo ni ndoto, na tafauti yake unaishi kwenye ndoto unayasahau maisha,
Maisha naweza kuyafananisha na neno moja nalo ni kuridhika na (Qadar) ya Mwenye enzi Mungu, Vipi kuridhika huko?(Mfano) Umepangiwa maisha yako pengine uko (Dubai), au Upo (Muscut) au uko Canada au unaishi Uingereza, ikawa katika moyo wako imekujia fahamu ya kuridhika Mollah wangu kanichagulia katika Ardhi hii ndio  nifanye maisha, na kazi hii japo ya Cleaner ndio iwe pato langu la halali, na mimi  kwa hilo nimeridhika, kwa hili nimekubali kwa Roho ya ukunjufu, na niko nasubiri na yale mengine ulo nipangia ambayo mimi sina uwezo wa kuyajua ila kwa kutaka wewe, Mimi nafurahi kila leo kwa neema za afya, na kipato ulichoniruzuku, ukanifanya pia niweze kusaidia wengine, ukanilinda mimi na ufisadi wa dini yangu na dunia hii ambayo wewe ni mfalme wake, Mollah wangu naishi kwa ajili yako kila siku ulonipangia niwepo katika Ulimwengu huu, nipo mimi katika kukumbuka wewe, kuyakumbuka Mauti, kukumbuka Ibada, kukumbuka kila kinachotokea siku nzima hii ya leo, natulia katika enzi yako nikishukuru pumzi zako ulizonijaalia, afya njema ulonitunikia, Mke au Mume mwema ulonipa niishi naye, pamoja na kizazi chema ulichonijaalia, basi nijaalie mimi niishi sasa hivi badala ya kutegemea ndoto za utajiri au kuwa nakhofu kesho itakuaje, na chochote kile utakacho nipa basi nipe na nguvu za moyo nikitoe kuwapa wengine, Pia Mollah wangu usininyime mimi Roho ya Imani na Wema na Ihsani kwa Binaadamu wenzangu, nijaalie mimi niwe Mwenye kuzikhofia kuja kuzikosa Pepo  mbili moja hii ya Duniani ninayo ishi na nyengine hiyo ya Enzi yako ya Akhera nitakayokuja ishi.
Sasa kama hujaridhika ndio unatoka kwenye Maisha na unaingia kwenye (Plan B) ambayo ndio yako Mwenyewe unayoishi nayo hivi sasa, sasa hapo unataka Ujenge Jumba la ghorofa (Tanzania) au Kenya, unataka na Biashara na kuongeza Mke wa Pili, unataka ununue Shamba, upeleke gari, Ewe ndugu yangu Kichwa chenyewe kimoja utaweza vipi kuyakidhi mahitaji hayo yote bila ya kuhangaika? Lakini siku utakayosema maisha yangu hapa hapa nilipo, na kazi yangu ndio hii nilonayo hapa, moja kwa moja nafsi yako itakushukuru (Alhamdullilah) sasa ndio tunaishi, sasa ndio tunaanza kufurahia maisha, Lakini kinyume cha hayo ni kualika matatizo, Na ukiamua kuikubali (Qadar) ya Mwenye enzi Mungu ukaanza kuishi kihalali na kama alivoamrisha Mollah wako katika muongozo wake alokuletea hapo maisha yatakua hayapiti mbele ya macho yako, ila utakua unapita nayo kila sekunde na dakika zilizomo kwenye maisha yenyewe.
Kuishi sasa hivi ni kama (Hivi)"Unajua mwenyewe kwa yakini sasa hivi ni msimu wa Kiangazi wakati wake umefika, sio mpaka(Gazeti liandike mazao yaathirika kwa Jua kali) Na wewe ndio unanyanyuka usingizini(Kiangazi hicho) Ishi ndani ya Kiangazi, furahia neema ya Jua, ona Mollah wangu ananipa (Vitamin D na K) Na kupitia Majani wanayokula wanyama ananipa mengine ya siri nisiyoyajua, Wakati wenzangu kule Ulaya wamevaa (Bag) zima Barabarani kwa ajili ya Baridi, Mie nimevaa fulani (Bukheir wa Afya). Hayo ndio maisha unayotakiwa uishi lakini tafauti yake wewe jitizame maisha yako yote unaishi kwenye jana, au kesho, lakini kwenye leo hupo kabisa, na matokeo yake unakosa kuishi kwa ukamilifu, na maisha yanakupita mbele ya macho yako huku ukiwa umelala, ukiamka unauliza kimetokea nini, utadhani ndio kwanza umekuja Ulimwenguni.
Maana ya Maisha ni  kuwa Furahani hiyo ndio (Nature) yako, ukiona humo furahani basi jijue huishi vizuri, kuna tatizo fulani, pahala fulani, Maisha ni kuridhika na hali uliyonayo, kuridhika na ulichonacho, Maisha ni kuamini na kujua kila jambo limekuja na kutokea kwa Mwenyewe Mwenye enzi Mungu na wewe kazi yako ni kupokea, lakini ukenda kinyume na maelekezo na muongozo wa Mwenye enzi Mungu ndio utakua unaishi huku umetawaliwa na Akili.
Vipi kutawaliwa na Akili? 
Kutawaliwa na Akili ndio huko kuishi na Tamaa za ndoto, haikatazwi kutamani, ila inakatazwa kuzifanya hizo tamaa ni kweli na kuanza kuzifatilia, hapo ndio utakua unaingia hasarani, inakua hamna maisha tena, unahangaika pengine Family yako iko mbele yako huwezi hata kufurahi nayo, kila kitu mateso kwako, inakua mchana kutwa unapita na ndoto juu ya ndoto, unapita mjini huoni unakoroma, unakwenda Msikitini umejaa njozi tupu, unashindwa hata kusali mambo yanakujia kwenye Sala, Unakwenda Nyumbani usingizi hupati  umo katika mbinu za kesho, wakati leo hujaimaliza, Na hivyo ndivyo maisha yanavo kupita mpaka pale Mauti yanavokaribia ndio unakumbuka lahaullah sijatoa sadaka, hujapata ku(Enjoy)hujapata ku(Spend time with family) wewe ulikua unaishi kwenye ndoto mwanzo mpaka mwisho.
Na ukiacha Maamrisho ya Mwenye enzi Mungu kuna mambo matatu lazima yakufikie mapema, sababu huna maisha, hujui thamani ya maisha haya, umeamua unavotaka wewe,  ukawa unatenda mambo machafu basi ima Maradhi yanakushukia mapema, ukiacha kumuabudu Mollah basi dhiki za Roho zinakutawala, na kama huwatendei wema wanaadamu wenzio basi mashaka ya Akili yanakuzonga unakua huna furaha daima.
Lakini ukiwa katika njia ya Mwenye enzi Mungu Basi Furaha na Afya njema ndio vinafatia, Maisha ya salama na Roho inapata starehe za maisha, na utulivu kama ule wa utotoni, Ndio maana siku zote unakumbuka utotoni, kwa sababu ndio (Time) pekee uliyopata kuishi, Basi fanya mema, muabudu Mollah wako, kuwa msafi urejee utotoni upate kujua nini Maisha, na ukiyajua hivi sasa ni vizuri zaidi kwani utotoni ulipita na sasa hivi unakaribia kufika, basi ikiwa utaonja ladha ya utoto uzeeni ukaona raha yake, utawacha tabia yako ya hivi sasa kuwa kama (Robot) Kazini, nyumbani,kula,kulala,kazini tena. Utaanza kubadilisha mwenendo utaichukua siku kama inavokuja, kila siku itakua mpya kwako, (Walking)harusini, Msikitini, Darsani. Mpirani, Shamba, Baharini, kila siku utakua unapanga na Ku(Experience) mambo mepya, lakini ukiona umo kwenye tabia isobadilika basi pata wasiwasi nini kimekusibu, na jiulize mimi naishi au nasindikiza wenye kuishi.

No comments:

Post a Comment