Sunday, April 12, 2015

MAISHA NI KITU GANI ? PART 2

Asalaam Aleiykum

Basi kwenye Safari hii ya (Maisha ni Kitu gani) Nataka nizindue Akili yako kwa kukujulisha jambo ambalo huenda likawa msaidizi wako huko mbele katika somo hili, Nataka wewe Mwenyewe ufanye uchunguzi wa mambo mawili haya ambayo pengine yanaweza kukujulisha aina gani ya maisha unayoishi hivi sasa.
Angalia wakati wa dhiki au maradhi, Wakati wa shida au matatizo kwanini wakati yaani(Muda) unakwenda taratibu, unakua mrefu, miaka inakua mingi. Na wakati wa furaha au Raha (Muda) au wakati unapotea, au unakwisha haraka, kama unajua siri ya viwili hivi basi huna haja ya kusoma darsa hii ya nini maisha?.
Lakini kama hujui basi wacha nikuchukue katika dunia ya ufafanuzi wewe mwenyewe ili uwache kusubiri nani kasema, nani katoa (Fatwa) ili upate ufafanuzi wa kufahamu na uweze kuishi hiyo miaka michache ilobakia, kwanini nikasema hivyo pengine siku zote ulikua unaishi(Dead man walking).
Kuna Msemo wa (Waingereza)wanasema kwa lugha yao kama hivi "Inasemwa sana kabla ya kufa Maisha yako yanapita mbele ya macho yako, Kitu hicho ni kweli kinaitwa kuishi"(Mwisho wa kunukuu), Sasa wacha tuitizame jee kauli hii ina ukweli ndani yake?."Kwanini kabla ya kufa kwako ndio maisha yanapita mbele ya macho yako?" Na maisha kupita mbele ya macho yako ni kitendo cha majuto kama kilivotajwa kwenye Quraan aya ya 10 sura ya (Munafiqoon)

وَأَنفِقُواْ مِن مَّا رَزَقۡنَـٰكُم مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِىَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنِىٓ إِلَىٰٓ أَجَلٍ۬ قَرِيبٍ۬ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ 
Na toeni katika yale tuliyokupeni, kabla mmoja wenu hayajamjia mauti, ikisha akasema, Mollah wangu huniakhairishi muda kidogo, nikatoa sadaka, na nikawa miongoni mwa watendao mema.
Mauti yakishawasili ndio unaanza kukumbuka kuishi, unabubujikwa na machozi lau ningehairishiwa muda ningefanya hivi na vile, sasa swali la kujiuliza kwani siku zote ulikua wapi? kwani sasa hivi unafanya nini? wapi tena, wakati huu hufanyi unasubiri karibu ya kufa unasema ningejua ningetoa mali yote kwa yatima, ningejua ningekua siku zote nasafisha Msikiti, ningejua kuwa maisha yana umuhimu huu ningefanya ihsani kwa kila mtu, ningekua mtu mwema.
Swali la kujiuliza kwani ulikuwa wapi? huo ndio msemo wa maisha yanakupita mbele ya macho yako, ulikua unaishi lakini ndani ya (Memory) umelala katika godoro la kumbukumbu, kila kitu chako kimo kwenye ndoto, kama sizo zilopita unaota zijazo, ndio maana hata siku moja huoti kitanda ulicholalia, ushapata kujiuliza kwanini?
endelea part 3

No comments:

Post a Comment