Asalaam Aleiykum
Katika Mahusiano hayo kama kutatokea khitilafu ikawa hamkuweza kuishi pamoja basi hapo hakuna ndoa, ila kilichobaki ni ugonvi na kuwekwa kwa ndoa hiyo kwa kipande cha karatasi, Mnasahau kabisa kuwa nyinyi ndoa yenu mmefunga kwa Rehma ya Mwenye enzi Mungu, kwa upendo na makubaliano ya pande mbili za familia.
Sasa kinachobaki hapo ndoa inasahauliwa na unabaki ugonvi wa Talaka, Mwanamke anataka Talaka Mwaname hataki kutoa karatasi, na hapo inampelekea Mwanamke kujihisi ana makosa ya kujitenga na Mwanamme huyo, anazidi kumpa nguvu kwa kudhani Amri hiyo lazima itoke kwa Mwanamme, anasahau kabisa kwamba na yeye ana uwezo wa kutoa Talaka.
Vipi ana Uwezo huo?
Mwanamme kapewa nafasi chungu nzima za kutekeleza tendo la Talaka, Na Mwanamke kapewa(Chance)yake japo mara moja lakini yenye nguvu ya hoja pale ambapo jitihada zote zimefanyika za kuinusuru Ndoa hiyo zimeshindikana, yakatizamwa matatizo yote husika yanayoikabili ndoa hiyo ikawa hakuna uwezekano tena wa wawili hawa kukaa pamoja, Na mpaka ikapatikana taarifa sasa hata vitanda wanalala tafauti mwezi wa sita huu, hapo inaashiria mahusiano yameshakatika na ndoa ishavunjika, na hakuna haja ya mmoja wao kubakia mahabusu(Kinyume chake ni jela unayoichukia ya Ndoa).
Na ikiwa Wawili hawa ndio hawakutani Kindoa na mwanamke anasisitiza kutokana na vitendo viovu vya mumewe au Rehma ya mapenzi imemuondokea na hawezi tena kuishi na Mume huyo basi sheria inampa haki ya kutoa Talaka kama ilivyoamrisha Quraan na Hadith ya Bwana Mtume s.a.w inavosema..
No comments:
Post a Comment