Asalaam Aleiykum
Sura ya Nur aya 31.
وَقُل لِّلۡمُؤۡمِنَـٰتِ يَغۡضُضۡنَ مِنۡ أَبۡصَـٰرِهِنَّ وَيَحۡفَظۡنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبۡدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنۡهَاۖ وَلۡيَضۡرِبۡنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِہِنَّۖ وَلَا يُبۡدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوۡ ءَابَآٮِٕهِنَّ أَوۡ ءَابَآءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوۡ أَبۡنَآٮِٕهِنَّ أَوۡ أَبۡنَآءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوۡ إِخۡوَٲنِهِنَّ أَوۡ بَنِىٓ إِخۡوَٲنِهِنَّ أَوۡ بَنِىٓ أَخَوَٲتِهِنَّ أَوۡ نِسَآٮِٕهِنَّ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَـٰنُهُنَّ أَوِ ٱلتَّـٰبِعِينَ غَيۡرِ أُوْلِى ٱلۡإِرۡبَةِ مِنَ ٱلرِّجَالِ أَوِ ٱلطِّفۡلِ ٱلَّذِينَ لَمۡ يَظۡهَرُواْ عَلَىٰ عَوۡرَٲتِ ٱلنِّسَآءِۖ وَلَا يَضۡرِبۡنَ بِأَرۡجُلِهِنَّ لِيُعۡلَمَ مَا يُخۡفِينَ مِن زِينَتِهِنَّۚ وَتُوبُوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ جَمِيعًا أَيُّهَ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
"Na Waambie Waislamu wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasidhihirishe viungo vyao isipokuwa vinavyo dhihirika,Na waangushe shungi zao mpaka vifuani mwao,Na wasionyeshe mapambo yao ila kwa wanaume zao, au baba zao, au baba za waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao,au kaka zao, au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenziwao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kiume, au wafuasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yalohusu uwana uke, Wala wasipige miguu yao ili yajulikane wanayoyaficha katika mapambo yao, Na tubieni nyote kwa Mwenye enzi Mungu Enyi Waumini ili mpate kufaulu."
Nini kuinamisha?
Kuinamisha macho kwa Mwanamke ni kuenzi (Hayya) ya Mwanamke, kuwa siku zote unaona aibu, hiyo ndio silaha ya Mwanamke, daima macho yako chini, na macho yakiwa chini nini kinatokea? siku zote unaendelea kuwa (Biharusi), kila mtu anatamani ulinyanyue jicho la (Ghazzala) lakini halinyanyuki, kuinamisha macho siku zote unabakia na bashasha za mtoto mdogo, macho daima meupe yanangara kwa utiifu, na ukiwa hutizami ovyo ovyo ndipo unapata neema na nguvu ya kulinda(Kasha lako la dhahabu).
Halafu wasidhihirishe viungo vyao, kwa sababu maungo ya Mwanamke yote ni mapambo kwa wanaume, kwa hiyo ukidhihirisha ina maana umeweka (Window shopping), kila mtu atizame mimi niko hivi, na hapa kuko vile, inakua watu wanakujua kama (Map) ya dunia, wanajua kasoro na ukamilifu wako, halafu unauliza mbona wanashangilia wakati wewe ndio(Actress). Yote haya unafundishwa heshima na adabu ya kujilinda, ili ujijue thamani yako, ujijue wewe na wanawake wengine tafauti, wewe bakia na (Uharusi) wako daima, wewe kuwa Mwanamke usishindane na Wanaume.
Halafu tena kwa kuenziwa na Quraan unaambiwa wewe (Mwana kinda kindaki) Teremsha shungi lako mpaka kifuani, kwa sababu kifua chako kina (Madhara) kwa Wanaume, kuna wengine wamekatishwa (Kunyonya) walipokua wadogo kwa hiyo wakikiona kifua cha Mwanamke wanakua hawajiwezi, wanaweza kukufata njia nzima huku wamefadhaika na kifua cha Mwanamke, na hayo yatakuletea udhia, kwa sababu yanawapendezesha baadhi ya wanaume na unakua kivutio(Senema) ya siku nzima kwa ajili ya kifua chako, kwa hiyo utaona kifua chako wewe lakini wanakikatia (Ticket)watu wengine bila ya wewe mwenyewe kujijua, sasa ufanye nini? Hifadhi kifua chako usitoke kama una nyanyua vyuma, kuwa na aibu, wewe Malkia, angusha shungi lako na useme hapa hamuoni kitu, mimi Mwanamke wa Kiislam na hili ndilo vazi langu.
Na Mapambo yenu hizo (Piko na Hina) na mengineo msioneshe kwa sababu katika hayo kuna siri kubwa inayo kwenda (Deep) kwa wale wenye kujua mambo, ama kwa wasojua wanaona maandishi, lakini kwa wenye kujua (Siri) ya maandishi na hizo (Tatoo) za (Hina na Piko) wanajua na (Msg) zilizomo katika michoro hiyo, wanajua Mwanamke anasema nini? kwanini akachora hivyo, na anakusudia nini? kumwambia huyo alo mchorea kama anafahamu, Ntakupeni mfano mmoja(Kama yamechorwa Mawaridi kwenye Mwili)basi unaambiwa sasa acha kutizama Bustani nitizame mimi)sasa una hiyari yako kama utatizama ua moja moja au kwa jumla, halafu aya inaendelea kukufahamisha kwa watu gani unaweza kuyadhihirisha mapambo hayo ambayo hayataleta tafsiri nyengine kama walivotajwa watu hao wa aina gani.
Na Wala msipige miguu yenu ili kudhihirisha mapambo yenu, Mpaka mwendo unafundishwa kama utakua umevaa vitendea kazi, yaani hayo mapambo, sasa mapambo yepi yalotajwa hapa?(Ni yale yanotoa sauti)(Na sauti ina athari ya kila aina kwa mwanaadamu) siku hizi nadhani sio sana, katika karne hizi (Art) hii nadhani imepotea, siku hizi kuna watu wanajichora (Nyoka mara simba)(Art)ya mapenzi imepotea, kuna msemo mmoja kama mnausikia(Nani atomvika paka kengele) kwanini paka akavikwa kengele, paka anavikwa kengele kwa sababu anakamata ndege sana katika mawindo yake, kwa hiyo kwa kufanya hivyo wanashituliwa ndege wakisikia kengele wanajua paka huyo anakuja, kwa hiyo wanaruka, kwa hiyo zamani Wanawake walikua wakivaa kengele kwenye miguu yao si kwa ajili ya kumfanya Mwanamme akimbie laa, ni kwa ajili ya kuamsha au kushitua hisia fulani lakini kwa njia za mapambo, na hutungwa kengele hizi kwa milio tafauti kwa ajili ya mwendo wake wa haraka haraka na mwendo wa taratibu, (Vibration) za kengele hizo zina athari yake kwenye (Akili) ya Mumeo,ndio maana mkaambiwa msipige miguu (hatari kubwa) kuna watu waso husika watapata (taarifa) zisizo wahusu, msidhihirishe mapambo yenu na hizo ndizo sababu za kuambiwa mjisitiri, lakini Mwenye enzi Mungu anakujueni, anajua mtateleza ndio akakwambie katika aya ilotangulia mkiteleza mkaponyoka basi yeye atakusameheni, na atakushushieni Rehma ya kuweza kujistiri ili msije kuudhiwa na kuwashawishi watu kuanza kukuvunjieni heshima zenu, hayo yote ni kwa ajili yenu nyinyi kwa heshima na uzuri na adabu na aibu na kulinda enzi ya Malika za nafsi zenu.
No comments:
Post a Comment