Sunday, April 26, 2015

SABABU ZA KUJISTIRI MWANAMKE WA KIISLAM PART 2

Asalaam Aleiykum

يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّبِىُّ قُل لِّأَزۡوَٲجِكَ وَبَنَاتِكَ وَنِسَآءِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ يُدۡنِينَ عَلَيۡہِنَّ مِن جَلَـٰبِيبِهِنَّۚ ذَٲلِكَ أَدۡنَىٰٓ أَن يُعۡرَفۡنَ فَلَا يُؤۡذَيۡنَۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورً۬ا رَّحِيمً۬ا
"Ewe Mtume; Waambie wake zako, na Watoto wako wa kike, na wanawake wa Kiislam, Wajiteremshie uzuri nguo zao(Wajifunike)kufanya hivyo kutapelekea upesi wajulikane(Ni Wanawake wa heshima)(Ili)Wasiudhiwe, Na Mwenye Enzi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (Na) Mwingi wa kurehemu"
Kwanini Wajifunike? kwa sababu Wafunike hizo (Taa) nilizozitaja kwa vipi?Mwanamke akiacha (Maungo)yake wazi anakua anapeleka (signal) za hiyo taa nyekundu ndio maana ukaona rangi nyekundu imehusishwa na (Sex) kwa sababu imetokana na rangi ya (Damu) tulo umbwa nayo, na kutokana na (tendo hilo) sote ndio tunazaliwa, ndio utaona nguo nyekundu inahusishwa na (Sex) huoni hata siku moja Biharusi kavikwa nguo nyekundu, pia utakuta kwa wale wanawake wenye kuuza miili yao wanaweka (Taa) nyekundu au pazia jekundu kuwajulisha wateja wao hapa kuna (Bussines) sio (Love) kwa hiyo Mwanamke akenda bila ya kujisitiri utaona macho  yaso idadi yanamuangalia, na kutokana na ishara hiyo maudhi yanafatia, wanaume wanaanza kukukera, wako wanokukera kimya kimya na wale wenye kutoa sauti.
Hiyo ndio moja katika zile (Taa) mbili, Kwa hiyo Mwanamke akiamua kuzipunguza nguo ana amua akijua vizuri nataka kuwashughulisha watu(Conscious Heart) na ndio anatukuta na sisi wagonjwa maskini(Unconscious Mind)tunabubujikwa na mate, tunasahau kwamba haramu, hatukumbuki chochote tunaendelea kukodoa macho kuridhisha Mioyo yetu kwa aina ya kila mawazo, kwa hiyo muoneshaji na anaye ona wote tunaingia kwenye hasara ya nafsi zetu.
Ama akiamua Mwanamke kufata kama alivoamrisha na kufunika Mwili wake, kitu cha Mwanzo kinachotokea anawasha (Taa) nyeupe, Anaonesha Ishara ya Amani, hapo hapo anapata kuheshimiwa, anapata kujulikana yule Mke wa mtu au mtoto wa fulani, au ni Mwanamke asotaka mambo mambo ya kipuuzi, kajihifadhi, kashaleta msg usihangaike hata kutizama, hapa huoni kitu, Mimi sitibu maradhi ya watu njiani kwa kuonesha maungo yangu, lakini basi isiwe kujisitiri kwenyewe nusu nusu juu umevaa (hijab) chini Buibui limekubana, au umevaa nguo za ajabu, hapo utakua unapeleka (Wrong Msg) watu watababaika mbona kuna rangi nyeupe na nyekundu zinawaka, itakua kama (Traffic Light) ilo haribika watu watakua hawajui wavuke barabara au wasubiri, ukiamua kujifunika basi iwe Mwili mzima umejihifadhi ili upate kujulikana watu wasikuudhi.

No comments:

Post a Comment