Sunday, April 12, 2015

MAISHA NI KITU GANI ? PART 1

Asalaam Aleiykum

Nilimuuliza Rafiki yangu mmoja wa Dhehebu la (Kikatoliki) katika Dini ya (Kikiristo)akiwa katika (Kabila) la (Kizungu) nini Maisha ?
Akanijibu kwa lugha ya (Kabila) yake kama hivi,
(Life is those a few year's between Birth and Death).
Jawabu zuri, lakini halijakamilika, tena limejibiwa kwa urahisi sana kama kwamba hiyo miaka michache haina thamani yoyote, Lakini ukweli halisi hilo ndilo jawabu la watu wengi wenye kuishi katika Ulimwengu huu. Dhana hiyo ndio inayo tupelekea tukaona maisha si chochote, (One Life) endelea kuchapa maji, endelea kufanya uharibifu, endelea kudhulumu, endelea kumsahau huyo alokupa maisha haya.
Kama utasoma vizuri utaona mwanzoni nimesema jawabu la swali hili ni zuri, lakini sio sahihi kwa kuwa halijakamilika. Kwanini likawa zuri kwa sababu Mwenye kujibu kagundua hiyo miaka michache baina ya kuzaliwa na kufa, Mtu kama huyo kaonesha dalili kama akifanyiwa kazi ya kujulishwa zaidi anaweza kupata matumaini ya kuokoka. Lakini kwa watu wengine haoneshi hata dalili, moyo ushakufa na moyo ukifa ina maana moja tu kuwa (connection) na Mungu wako ishakatika, na hapo hakuna matumaini tena.
Ndio Utakuta Baadhi ya watu wanaishi mpaka kufariki kwao hawaupati ukombozi wa Roho zao, na kama hupati ukombozi huo ni vigumu kukijua kitu hichi muhimu kiitwacho maisha.
Nakuchukua katika safari hii ya maisha ili nipate kuwasiliana na Roho yako tuweze kulizungumza tukio hili la maisha, Nini Maisha?. Watu wengi wana (Confused) baina ya (Life and Living) ndio Waingereza wanamsemo huu (One life Live it) Hawajakosea katika msemo wao, ila wamekosea katika ufahamu wao, Maisha (Life) ni kitu cha Kudumu ila kuishi ndio kitu cha muda (Temporary), Kwa sababu ingekua (Life) yenyewe ni ya muda vitabu vingesema zamani, lakini vitabu vyote vya (Haki) vinasema Maisha ni Milele iwe kwenye (Pepo au Moto) kwa  hiyo kaa 
ukijua wewe ni wa kudumu kwa sababu umetokana na hiyo (Life).
Ama tukizungumza kuishi ndio tunazungumza hicho kipindi unachopita baina ya kuzaliwa na kufa kati kati yake ndio kuna hiyo fahamu ya kuishi ambayo ina mpito wa matendo yako katika Ulimwengu huu. Sasa tujiulize kwanini kwetu sisi kikawa kipindi hichi cha mpito kikawa muda mfupi sana.
Ndio nimeamua kukuchukua katika safari hii ili na wewe upate kugundua jambo ambalo pengine litakufanya uweze kuishi japo muda mchache ulobakisha katika Ulimwengu huu.
Endelea part 2.

No comments:

Post a Comment