Sunday, May 24, 2015

DUA YA KUANZIA SALA PART 2

Asalaam Aleiykum

Ukishamaliza kusema hivyo unaingia katika maneno ya pili nayo yanatamkwa hivi:
"Subhaanaka Allaahumma wa Bihamdika, Wa Tabaarakasmuka wa ta'aalaa jadduka, wa laa ilaaha ghayruka"
"Utukufu na Shukuran ni wako wewe Mollah wangu""Limetukuka Jina lako  lenye Utukufu"" na hakuna anaestahiki kuabudiwa isipokuwa wewe Mollah wangu".
"Umetukuka Mollah wangu kwa kuumba kila kitu katika Ulimwengu huu nikiwamo na mimi, sina cha kuongeza isipokua Shukurani ya kuniwezesha kuja mbele yako kwa ajili ya kukumbuka wewe Mollah wangu, Limetukuka Jina lako lenye Utukufu ambalo limenifanya mimi kusimama mbele yako na nikatamka hakuna anaestahiki kuabudiwa isipokuwa wewe Mollah wangu".
"Wajjahtu Wajhiya lilladhee fatara-samawati wal-ardhi haneefan wama ana minal mushrikeen, inna salatee wanusukee wamahyaya wamamatee lillahi Rabbil-Aalameen, la shareeka lahu wabidhalika umirtu wa ana minal-muslimeen, Allahumma antal-Maaliku laa illah anta, anta Rabbee waa-ana Aabiduk, Salamtu Nafsee waata'raftu bi-dhanmbi faghfirlee dhunubi Jameean innahu laa yaghfiruu-dhunuba ila anta, Wahidnee li-ahsanil -akhlaq laa yahdee li- ahsaniha ila anta, Wasrif aanne sayyiha laa yasrifu aannee saayyiha illa anta, labbayika wasaadiyk walkhaiyru kulluhu biyadak, washarru laissa ilayyka, Anaa bikka wailayka tabarakta wataa'alaita astakhfiruka wa'atubu ilaika".
"Nimeuelekeza Uso wangu Kwa Yule ambaye aliyevileta Mbingu na Ardhi Na mimi (Najitoa)sio katika wale wenye Kumshirikisha(Mollah)wangu na chochote, Hakika Sala yangu, (Muhanga)wangu, Maisha yangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mollah wangu, Mollah wa Ulimwengu wote, asiye na mshirika, Na kwa hilo najisalimisha(Kwa kutii)na mimi ni miongoni mwa Waislam, Mollah wangu hakika wewe ni Mfalme wa(Kila kitu)Hakuna apasawe kuabudiwa isipokua wewe, Wewe ni Mollah wangu(Mfalme) na mimi ni Mtumwa wako(Kiumbe)Nimeikosea Roho yangu na nimeyajua makosa yangu, Naomba(Kwa hilo)Nisamehe makosa yangu yote, hakuna awezaye kusamehe makosa isipokua wewe Mollah wangu, niongoze mimi kwenye ubora wa Tabia, kwani hakuna awezaye kuongoza isipokua wewe Mollah wangu, Na nitoe mimi katika Tabia mbaya, kwani hakuna awezaye kunitoa isipokua wewe Mollah wangu, Mollah wangu nimehudhuria Mbele yako, kujibu wito wako,(Wa kukuabudu)na niko tayari kuutumikia wito huu, Mazuri yote yapo kwenye uwezo wako, Na mabaya siyenye kutoka kwako, Na mimi naishi kwa ajili ya uwezo wako na marejeo yangu ni kwako wewe Mollah wangu, Baraka na Utukufu ni wako wewe, Naomba msamaha wako na kwako (Pekee)Mimi natubia (Makosa)yangu..

No comments:

Post a Comment