Sunday, May 3, 2015

AJABU YA KIUMBE PART 3

Asalaam Aleiykum

Naipenda sana Hadith ya Nabii Adam a.s na Bibi Hawa  katika maisha yao ya peponi, hakika yana mazingatio makubwa ikiwa umepewa Hekima kutoka kwa Mollah wako, siku zote nikiwatizama wanyama wananikumbusha (Hadith)hiyo. Nakumbuka Kisa cha Baba yetu Adam, alivokua na Raha Peponi.
Watizame vizuri Wanyama hawana tafauti na sisi isipokua moja tu, tizama furaha walonayo, wanaamka wakiimba na kuita, wanamsabahi Mollah wao kila siku wala si wenye kuasi katika jambo hilo la (Ibada), Wanakula hichi na kile katika ardhi hii wanakwenda huku na kule wala hawana dhiki, Na wakishikwa na maradhi wanamtegemea Mollah wao ndie Mwenye kuwaponesha, hawana wasiwasi wowote, lakini sasa njoo kwa (Kiumbe cha Ajabu) Tafauti yetu na Wanyama ni moja lakini ni kubwa sana, Wanyama wana (Enjoy life) yao wanapata neema hizo na Baraka kutoka kwa Mollah wao wakiwa hawajui nini (Bliss)hawana (Awareness)Fahamu. Mwanaadamu yeye kapewa (Awareness)Fahamu za kuzijua neema na baraka za Mollah wake na hiyo (Bliss)Kwa hiyo Mwanaadamu aki(Enjoy) anazijua raha zake, akifanya Ibada anazijua fadhila zake alizotendewa na Mollah wake, na pia anaelewa yale yote yalowekwa ya kutoa sadaka, kufanya wema na hisani ni matendo ya mtihani wa kutizamwa vipi unaitumia hiyo (Awareness)Fahamu ulonayo.
Ukiwa utafanya jeuri ukatenda kwa makusudi basi juu yako hakuna kusamehewa, sababu unajua ukifanyacho na malipo yake ni yenye uhakika, lakini kwa mnyama yeye hajui na ndio maana na wewe ukifanya hujui unakua katika hali ya unyama, na kwa ajili hiyo unakua huna makosa, lakini ukitenda au kuacha Ibada wakati unajua basi malipo yake anayajua aliyekuumba, Na kama ukifanya alivyoamrisha basi utaanza kupata hicho kitu kinachoitwa (Bliss)hapa hapa duniani, na ukipata kitu hicho ndio utajua maajabu gani yanokusubiri huko akhera, Na ikiwa kakuumba wewe kwa njia ya ajabu, nini malipo yake yanayokusubiri, na malipo ya Mwenye enzi Mungu ni yenye ajabu isiyokatika ikiwa utayapata.
Lakini swali la kujiuliza jee unastahiki kuyapata kutokana na Ibada zako?, au Kwa Radhi zake?. Na kwa hilo inatosha ujiulize jee niyafanyao katika Ibada yanatosha?, jawabu unalo mwenyewe mimi kazi yangu ni kukuuliza kwa hilo nakutakia rehma za fahamu zikushukie.

No comments:

Post a Comment